Mchambuzi
JF-Expert Member
- Aug 24, 2007
- 4,850
- 9,405
Mjadala wetu utakuwa na sehemu SITA kama ifuatavyo:
Kufuatia utangulizi, sehemu ya kwanza itaangalia kwa kifupi historia ya nafasi ya Makamu wa Rais katika jamhuri ya muungano wa Tanzania. Katika hili tutaangazia vipindi viwili muhimu katika historia ya Jamhuri ya Muungano Tanzania:
-Kipindi cha mfumo wa chama kimoja (1965 – 1995) na
-Kipindi cha mfumo wa vyama vingi (1995 – hadi sasa).
Sehemu ya pili itajikita katika mjadala juu ya mfumo wa mgombea mwenza nchini Marekani. Hii ni kwa sababu urais wa Mama Samia Suluhu Hassan ni matokeo ya kazi ya tume ya Jaji Bomani iliyopendekeza nchi yetu iigie mfumo wa mgombea Mwenza, Marekani.
Sehemu ya Tatu itajikita katika mjadala kuhusu ushiriki wa Makamu wa Rais katika maamuzi na shughuli za kila siku za Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania. Lengo kuu hapa ni kuangalia ushiriki wa Makamu wa Rais anayetokana na mfumo wa mgombea mwenza.
Sehemu ya nne itaangazia uzoefu wa Marekani, hasa kujifunza kuhusu ‘legacy’ inayowezwa jengwa na Rais aliyerithi kiti cha urais kilichoachwa wazi na rais aliyefariki dunia. Lengo kuu hapa pia itakuwa ni kuangalia hayo katika muktadha wa Rais ambae awali alikuwa ni mgombea mwenza.
Sehemu ya tano na itajikita katika muktadha wa uongozi wa sasa chini ya Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuangalia fursa alizonazo Rais Samia Suluhu Hassan.
Sehemu ya sita na ya mwisho itajikita katika mjadala juu ya changamoto zilizopo.
Kufuatia utangulizi, sehemu ya kwanza itaangalia kwa kifupi historia ya nafasi ya Makamu wa Rais katika jamhuri ya muungano wa Tanzania. Katika hili tutaangazia vipindi viwili muhimu katika historia ya Jamhuri ya Muungano Tanzania:
-Kipindi cha mfumo wa chama kimoja (1965 – 1995) na
-Kipindi cha mfumo wa vyama vingi (1995 – hadi sasa).
Sehemu ya pili itajikita katika mjadala juu ya mfumo wa mgombea mwenza nchini Marekani. Hii ni kwa sababu urais wa Mama Samia Suluhu Hassan ni matokeo ya kazi ya tume ya Jaji Bomani iliyopendekeza nchi yetu iigie mfumo wa mgombea Mwenza, Marekani.
Sehemu ya Tatu itajikita katika mjadala kuhusu ushiriki wa Makamu wa Rais katika maamuzi na shughuli za kila siku za Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania. Lengo kuu hapa ni kuangalia ushiriki wa Makamu wa Rais anayetokana na mfumo wa mgombea mwenza.
Sehemu ya nne itaangazia uzoefu wa Marekani, hasa kujifunza kuhusu ‘legacy’ inayowezwa jengwa na Rais aliyerithi kiti cha urais kilichoachwa wazi na rais aliyefariki dunia. Lengo kuu hapa pia itakuwa ni kuangalia hayo katika muktadha wa Rais ambae awali alikuwa ni mgombea mwenza.
Sehemu ya tano na itajikita katika muktadha wa uongozi wa sasa chini ya Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuangalia fursa alizonazo Rais Samia Suluhu Hassan.
Sehemu ya sita na ya mwisho itajikita katika mjadala juu ya changamoto zilizopo.