democratic
JF-Expert Member
- Nov 21, 2011
- 1,642
- 295
yeye kuutaka urais sio jawabu la wananchi nao kumtaka rais mkigoma,naona kwa hiyo cd ya ukigoma aliyoamua kucheza ndo itamharibia zaidi
We nae vipi mie hapa si nimetoa maoni yangu au unataka nitoe ya kwako?Inatakiwa kuheshimu maoni ya wengne c kila kitu upinge tu.
Zitto anatakiwa kutubu katika chama chake kuwa amekosea.
Napata wasiwasi na mienendo ya Zitto kwa sasa kwani inaonesha imekisa hekima na busara.
Ni hayo tu yangu
Kwa vile Zito katangaza wazi kuwa "urais" anaupenda, kwa vile watu wake wa karibu wamesema kuwa lazima rais wa 2015 atoke Kigoma, kwa vile kwa nyakati mbalimbali tumeona kuwa Mh Zito amekuwa na matamshi ya kung'ata na kupuliza; kukana na kukiri baadaye kuwa kasema, kwa vile hata uenyekiti wa Chadema aliwania akanyamazishwa na Chama, ....
nadiriki kusema Chadema haitapona kuvurugwa na Zito Kabwe, na hatimaye kusambaratishwa kama vilivyokuwa vyama vya NCCR Mageuzi, na CUF....
kisha Zito atatimkia chama kingine dhaifu ili atimize azma yake ya kuwania urais kupitia chama hicho au ugombea binafsi. Chadema ikitaka kubaki imara isiyapuuze sana yanayoendelea.
Huu ni mtazamo wangu tu... ninaweza kupingwa..
tukipanga vijana wawili wenye ujasiri wa kula rushwa kubwa zitto hawezi kukosekana
Clinton na Harper wamejiandaa kwa muda gani?..Kina Putin, Kibaki, Kagame M7 na wengine kibao walianza toka enzi za Uhuru..Kichuguu mkuu wangu watu hawa wote huandaliwa nyuma ya pazia na sii watu wanajitokeza tu kama unavyosikia ktk Tv na magazeti..Mtoto wangu miye alikuwa shule ktk hafla ya shule aliulizwa swali - Utataka kuwa nani ukikua?.. mtoto alijibu - " I wonna be The Prime Minister of Canada.." Watu walimpigia makofi na kushangilia badala ya kumpuuza... Mkuu wangu huyu ni mtoto wa miaka 8 tu, walokuwepo sii wajinga kumshangilia na kumpa moyo na heko japokuwa wanajua ni ndoto haiwezekani kiurahisi, lakini it's the message behind it ndio wenzetu wanacho kitazama. Nguvu ya majibu kama yale na sii kufadhaika..Mijinga kina sisi tunamtazama Zitto na kuanza kupiga mahesabu...
well said mkuu...
Zitto is very smart, but not a presidential material!! he is not strategic, and most of all, zitto ANAWASHWA-WASHWA SANA na tamaa zisizofichika hadi kuparamia lile mama fisadi ili apate pesa
Funguka zaidi mkuu, una maana naye ni Marioo?!
unalolidai si sahihi sana kwani kabwe ni mzuri sana wa kujenga hoja na kusimamia anachokiona kuwa kiko sahihi...Hii tabia amekua nayo toka akiwa pale UDSM na sidhani kama ni unafiki kuwa na different opinion against the majority......
Clinton na Harper wamejiandaa kwa muda gani?..Kina Putin, Kibaki, Kagame M7 na wengine kibao walianza toka enzi za Uhuru..Kichuguu mkuu wangu watu hawa wote huandaliwa nyuma ya pazia na sii watu wanajitokeza tu kama unavyosikia ktk Tv na magazeti..Mtoto wangu miye alikuwa shule ktk hafla ya shule aliulizwa swali - Utataka kuwa nani ukikua?.. mtoto alijibu - " I wonna be The Prime Minister of Canada.." Watu walimpigia makofi na kushangilia badala ya kumpuuza... Mkuu wangu huyu ni mtoto wa miaka 8 tu, walokuwepo sii wajinga kumshangilia na kumpa moyo na heko japokuwa wanajua ni ndoto haiwezekani kiurahisi, lakini it's the message behind it ndio wenzetu wanacho kitazama. Nguvu ya majibu kama yale na sii kufadhaika..Mijinga kina sisi tunamtazama Zitto na kuanza kupiga mahesabu...
Sana sana aanze kufikiria uwaziri mkuu baada ya Dr Slaa kuchukua nchi 2015.. Zito anabweteka bure!!! Iwapo ana akili timamu atang'amua kuwa kasi ya watanzania kuipenda CHADEMA ni kwa ajili ya Dr Slaa!!
Nina imani kuwa huwa hawajiandai kama ambavyo mwenzetu Zitto anavyojiandaa; tunaweza kujadiliana hilo. Kati yao wote uliotaja hapo, hakuna hata mmoja aliyewahi kutangaza nia za kuwania ukuu wa nchi miaka mitano kabla ya uchaguzi. Wote wamakuwa wanatangaza wakati wa mchakato wa uchaguzi tu; na wengine wao huwa wanapata ukubwa wa nchi kwa sababu ya kuwa viongozi wa vyama vyao. Kupiga kampeini na kuunda organization za uchaguzi muda mrefu kabla ya uchaguzi huwa ni dalili ya udhaifu mkubwa sana kwa candidate.
Halafu kumbuka kuwa kumshangilia mtoto na kumpa moyo katika jambo lolote ni jambo la kawaida sana na ni tofauti na kumshangilia mtu mzima ambaye unajua kuwa analofanya si sahihi. Zitto angeweza kukaa kimya akiwa na plani zake akisubiri wakati wa mchakato wa uchaguzi ndipo atangaze nia yake. kwa nini afungulia mode ya uchaguzi mapema namna hiyo. Ninaweza kuwa ni mjinga kwa macho yeawengine lakini naamini kuwa nina busara za kutosha sana kuona mapungufu ya Zitto katika swala hili la urais.