Uraia pacha kwa taifa changa ni kifo kuliko faida

kavulata

JF-Expert Member
Aug 2, 2012
12,316
12,614
Kuna sababu dhaifu sana za kuhalalisha uraia pacha. Nchi zetu hizi zina mifumo legelege sana ya kudhibiti uhalifu na wizi wa mali na rasilimali za taifa.

Hata bila uraia pacha mali zetu zinaibwa na watanzania na viongozi wetu na kwenda kufichwa nje ya nchi (ulaya, marekani na Asia (Dubai, oman, Singapole, Malaysia, nk) itakuwaje kama wezi hawa watakuwa na fursa ya kuwa na uraia pacha?

Hata nchi ndogo/changa zenye uraia pacha hatuoni faida za maana wanazozipata kwa kuwa na uraia pacha zaidi ya kuongezeka kwa wizi na utapeli ndani ya nchi zao tu. hata nchi zilizoruhusu uraia pacha (diaspora) naazo ni masikini pia, zinapigana, na wizi mwingi na mkubwa wa rasilimali zao. hatuna cha kujifunza kutoka kwa nchi hizo.

Faida tutakayopata kama tutaruhusu uraia pacha ni ndogo sana by far kuliko hasara tutakayoingia. Sababu ziliwafanya Nyerere, karume, mzee Mwinyi, Mkapa, Kikwete na magufuli kuukataa Uraia wa nchi mbili bado zipo hadi kesho.

Kuna watu wanatoa sababu dhaifu sana za kuruhusu uraia pacha za kupata wachezaji wa mpira na wawekezaji, ni za kipuuzi kabisa. Tutapanua lango la kupitia wezi wa mali zetu na kutumia barabara pana kuzisafirisha huko Swiss na visiwa vya Jersey kwa urahisi kabisa mchana kweupe.

Siungi mkono upuuzi huu.
 
Uoga wenu ndio maana ya huu umaskini

We fanya kazi kwa bidii Sana, kuwa muungwana, kuwa mstaarabu, kuwa mkweli acha unafiki utafanikiwa bila kuogopa sijui taifa changa sijui matakataka gani.

Yaani unaogopa raia pacha kwa watanzania wasiozidi 5000 dunia nzima wakati unaiba kura, unaiba mali ya umma, unafisadi hadi hela ya dawa vijijini, wanyama wanauzwa wazima wazima kwenda Dubai na kuuwa mimamba ya mita 10 una akill kweli?
 
Kuna sababu dhaifu sana za kuhalalisha uraia pacha. Nchi zetu hizi zina mifumo legelege sana ya kudhibiti uhalifu na wizi wa mali na rasilimali za taifa.

Hata bila uraia pacha mali zetu zinaibwa na watanzania na viongozi wetu na kwenda kufichwa nje ya nchi (ulaya, marekani na Asia (Dubai, oman, Singapole, Malaysia, nk) itakuwaje kama wezi hawa watakuwa na fursa ya kuwa na uraia pacha? Hata nchi ndogo/changa zenye uraia pacha hatuoni faida za maana wanazozipata kwa kuwa na uraia pacha zaidi ya kuongezeka kwa wizi na utapeli ndani ya nchi zao tu. hata nchi zilizoruhusu uraia pacha (diaspora) naazo ni masikini pia, zinapigana, na wizi mwingi na mkubwa wa rasilimali zao. hatuna cha kujifunza kutoka kwa nchi hizo.

Faida tutakayopata kama tutaruhusu uraia pacha ni ndogo sana by far kuliko hasara tutakayoingia. Sababu ziliwafanya Nyerere, karume, mzee Mwinyi, Mkapa, Kikwete na magufuli kuukataa Uraia wa nchi mbili bado zipo hadi kesho. Kuna watu wanatoa sababu dhaifu sana za kuruhusu uraia pacha za kupata wachezaji wa mpira na wawekezaji, ni za kipuuzi kabisa. Tutapanua lango la kupitia wezi wa mali zetu na kutumia barabara pana kuzisafirisha huko Swiss na visiwa vya Jersey kwa urahisi kabisa mchana kweupe.

Siungi mkono upuuzi huu.
Usisahau ugaidi. Magaidi watatumia mwanya huo.Nchi zenye uraia pacha,zinasumbuliwa sana na ugaidi.
 
Uoga wenu ndio maana ya huu umaskini

We fanya kazi kwa bidii Sana, kuwa muungwana, kuwa mstaarabu, kuwa mkweli acha unafiki utafanikiwa bila kuogopa sijui taifa changa sijui matakataka gani.

Yaani unaogopa raia pacha kwa watanzania wasiozidi 5000 dunia nzima wakati unaiba kura, unaiba mali ya umma, unafisadi hadi hela ya dawa vijijini, wanyama wanauzwa wazima wazima kwenda Dubai na kuuwa mimamba ya mita 10 una akill kweli?
Magaidi wengi wana uraia pacha.
 
Uchanga wa Tanzania uko wapi?
Watu wake bado ni mazuzu, hawezi kumkamata mwizi wa rasilimali zao kikamilifu. Jitu linaiba hela zao kwa mabilioni halafu likigundulika linasema ni vijisent tu, ni hela ya mbonga tu halafu wananchi wanabaki wanakenua na kulitazama likiendelea na shughuli zake. Wanaposema kuwa ni vijisenti tu na hela ya mboga maana yake ama watu hawa wanawafahamu watu wengine walioiba hela nyingi zaidi kuliko zao mlizoziona, au wameiba hela nyingi zaidi ambazo hamjaziona.
 
Unazungumza hoja za kutunga bila ushahidi wowote na una mawazo finyu sana. Huonyeshi cause na effect.
Niambie mfano wa taifa dogo kama letu ambalo linafaidika sana na uraia pacha kiasi cha kutamani kuiga maisha na hali yao kiuchumi, kijamii na kisiasa. Mnatafutia majizi njia nyepesi ya kutoroshea nje mali zetu.
 
Naunga mkono hoja! Labda ungetupa mifano ya nchi ambazo zina uraia pacha na zinapata hasara kwa kuruhusu uraia pacha!

Hata hivyo Wizi na Uharifu unatokana na udhaifu wa Serikali kusimamia Sheria!
Kwahiyo wewe umeiona Tanzania iko imara kwenye kusimamia sheria na utawala wa sheria? Uraia pacha ni kilio cha mchana kweupe jua linawaka. Sasa hivi majizi yetu yanapata shida kidogo kufungua accounts kwenye mabenk ya nchi za kigeni, lakini ukiyapa huu mwanya, looo ni kilio kitupu kaka.
 
Niambie mfano wa taifa dogo kama letu ambalo linafaidika sana na uraia pacha kiasi cha kutamani kuiga maisha na hali yao kiuchumi, kijamii na kisiasa. Mnatafutia majizi njia nyepesi ya kutoroshea nje mali zetu.
Hili ni thread yenye mawazo finyu sana. Waarabu wametorosha wanyama mpaka wameanzisha mbuga kwao, walikuwa na uraia pacha? Tena ni rahisi zaidi kuzuia utoroshaji wa mali iwapo wanaotorosha wana uraia pacha kuliko ambao hawana. Mabaye hana uraia akiiba anajua atakimbia na hutampata. Anyways, watu kama wewe ni hawa raia wasio na exposure na wameshakata tamaa ya kusafiri nje ya nchi hivyo wanabaki kufa kwa vijiba vya roho.
 
Naunga mkono hoja! Labda ungetupa mifano ya nchi ambazo zina uraia pacha na zinapata hasara kwa kuruhusu uraia pacha!

Hata hivyo Wizi na Uharifu unatokana na udhaifu wa Serikali kusimamia Sheria!
Nipe faida ya maana ya uraia pacha. Kinachohitajika sio uraia pacha bali sheria, taratibu na kodi zinazovutia wawekezaji kutoka nchi yoyote.
 
Uoga wenu ndio maana ya huu umaskini

We fanya kazi kwa bidii Sana, kuwa muungwana, kuwa mstaarabu, kuwa mkweli acha unafiki utafanikiwa bila kuogopa sijui taifa changa sijui matakataka gani.

Yaani unaogopa raia pacha kwa watanzania wasiozidi 5000 dunia nzima wakati unaiba kura, unaiba mali ya umma, unafisadi hadi hela ya dawa vijijini, wanyama wanauzwa wazima wazima kwenda Dubai na kuuwa mimamba ya mita 10 una akill kweli?
Kaeni hukohuko umanambani na vijisent vyenu, sisi amani kwetu ni zaidi ya fedha, hatutaki magaaidi wenye passport za nchi tofauti.
 
Uoga wenu ndio maana ya huu umaskini

We fanya kazi kwa bidii Sana, kuwa muungwana, kuwa mstaarabu, kuwa mkweli acha unafiki utafanikiwa bila kuogopa sijui taifa changa sijui matakataka gani.

Yaani unaogopa raia pacha kwa watanzania wasiozidi 5000 dunia nzima wakati unaiba kura, unaiba mali ya umma, unafisadi hadi hela ya dawa vijijini, wanyama wanauzwa wazima wazima kwenda Dubai na kuuwa mimamba ya mita 10 una akill kweli?
Mzee tulia, umeukana uraia wako mwenyewe kwa mambo ya kupita tu, you have uprooted yourself the pumpkin at your own home state. hatutaki hata maiti zao huku.
 
Hili ni thread yenye mawazo finyu sana. Waarabu wametorosha wanyama mpaka wameanzisha mbuga kwao, walikuwa na uraia pacha? Tena ni rahisi zaidi kuzuia utoroshaji wa mali iwapo wanaotorosha wana uraia pacha kuliko ambao hawana. Mabaye hana uraia akiiba anajua atakimbia na hutampata. Anyways, watu kama wewe ni hawa raia wasio na exposure na wameshakata tamaa ya kusafiri nje ya nchi hivyo wanabaki kufa kwa vijiba vya roho.
Hoja zenu za uraia pacha Tanzania hazina mashiko, unataka kufanya nini, kuleta nini na kuidia nini cha maana kama ukiwa na uraia pacha? una hela kiasi gani za kuwekeza huku zinazohitaji mpaka uwe na uraia pacha?

Mifumo yetu humu ndani ya nchi haisomani, sembuse huko nje ya nchi? Huku watu wana vyetu vya kuzaliwa na data zake, kitambulisho cha taifa na data zake, kitambulisho cha kupiga kula na data zake, driving license na data zake, NSSF na data zake kwa mtu huyohuyo, bank kuna data zake na kwa mwajili kuna taarifa zake kwa mtu huleyule. Msituongezee shida.
 
Kuna sababu dhaifu sana za kuhalalisha uraia pacha. Nchi zetu hizi zina mifumo legelege sana ya kudhibiti uhalifu na wizi wa mali na rasilimali za taifa.

Hata bila uraia pacha mali zetu zinaibwa na watanzania na viongozi wetu na kwenda kufichwa nje ya nchi (ulaya, marekani na Asia (Dubai, oman, Singapole, Malaysia, nk) itakuwaje kama wezi hawa watakuwa na fursa ya kuwa na uraia pacha?

Hata nchi ndogo/changa zenye uraia pacha hatuoni faida za maana wanazozipata kwa kuwa na uraia pacha zaidi ya kuongezeka kwa wizi na utapeli ndani ya nchi zao tu. hata nchi zilizoruhusu uraia pacha (diaspora) naazo ni masikini pia, zinapigana, na wizi mwingi na mkubwa wa rasilimali zao. hatuna cha kujifunza kutoka kwa nchi hizo.

Faida tutakayopata kama tutaruhusu uraia pacha ni ndogo sana by far kuliko hasara tutakayoingia. Sababu ziliwafanya Nyerere, karume, mzee Mwinyi, Mkapa, Kikwete na magufuli kuukataa Uraia wa nchi mbili bado zipo hadi kesho.

Kuna watu wanatoa sababu dhaifu sana za kuruhusu uraia pacha za kupata wachezaji wa mpira na wawekezaji, ni za kipuuzi kabisa. Tutapanua lango la kupitia wezi wa mali zetu na kutumia barabara pana kuzisafirisha huko Swiss na visiwa vya Jersey kwa urahisi kabisa mchana kweupe.

Siungi mkono upuuzi huu.
Na ndio akina waziri wa mambo ya nje, waziri wa utalii wote wana pacha ila kwa kuwa ni ccm, haionekani.

Sent from my moto g 5G (2022) using JamiiForums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom