Kisima
Platinum Member
- Oct 8, 2010
- 4,793
- 6,557
Yerico umeongea vitu vya maana sana. Kama kweli sasa vita ni kati ya MAKO na Jaji, basi narudia rai yangu kwa watanganyika wenzangu. Nchi isiende Zanzibar hata kama JK anataka hivyo.
Wazanzibari wameshatutenga na wana dola yao na rais wao ambaye hupigiwa mizinga 21 kwenye sherehe za Taifa lao. Iweje leo aje mtu kutoka Zanzibar na kutaka mizinga 21 ya Tanganyika. Hii maana yake ni kwamba Zanzibar itakuwa inapigiwa jumla ya mizinga 42!
Sie tutakuwa tumejikunyata pembeni tukishuhudia moshi wa mizinga hiyo 42 ambayo haituhusu. Tusikubali kupokwa mizinga yetu 21 kighiliba jamani.
Naunga mkono hoja ya wengi. Wakimpa jaji kura yangu inakwenda UKAWA pasi na shaka yoyote, hata kama MAMVI atahamia huko!
Nikwabie kitu, Jaji mahaba yake yapo Tanganyika licha ya kuishi na kukulia mdebwedoni!!!
Wazenji wenyewe wanatamani bora awe Gharib kuliko Rama japo wanashauku kubwa ajaye awe mwenzao.
Mako ataenda hadi mwisho wa mchakato ila hataibuka kidedea!!
Jamani mteule ni Jaji Agustino watu gani nyie hamsomi hata mbinu za mchezo??
Kikwete alimshawishi Membe agombee ili amtingishe Lowassa.. tatizo jamaa lilijipanga tangu asubuhi halikujari unasaba wao!!