Updates za Corona Tanzania

Updates za Corona Tanzania

Kwa wale wa moshi kuweni makini popote pale mlipo jioni hii mida ya saa 12 ambulance mbili toka kia zimeleta wageni toka kia wanasadikika wagonjwa wa corona maaana wamepelekwa lile jengo ambalo halijakamilika I mean jengo kubwa hivyo basi ....mtaarifu ndugu jamaa na rafiki popote pale alipo kama ana mgonjwa mawenzi aende kwa tahadhari ....every one kuwa makini kupigwa busu.. Kukumbatiana...na kunongonezana haswaa sisi wabongo ...corona ni hatari


Jr
 
Jana nilifanya tu kuulizia Bei ya mask pharmacy za Sinza, niliambiwa mask moja elfu 2, zile za surgical(ambazo kiuhalisia hazisaidii), Nikashikwa na butwaa.. hand sanitizer niliambiwa kichupa kidogo elfu Saba (hakizidi ml 100). Yaani ni hatari..Watanzania kila kitu kwao Ni fursa.
 
Kinachonisikitisha zaidi ni pale wanaposisitiza watu kutokushikana mikono lakini wanaongea na ku badilishana hewa na ugonjwa unaambukizwa sana kwa njia ya hewa.


Bagwell
Hawashikani mikono lakini wanaenda mazungumzo chumba kimoja chenye A.C.
 
Bill Gates katabiri vifo milion kumi kama virus vya huu ugonjwa vikifanikiwa kupenya Africa.. Manake hatufanyi juhudi zozote zaidi ya matamko yasiyo na tija2.. Na mengi yakiwa ni ya kisiasa zaidi

Jr

Mkuu huyo katumia software ipi ili nami niwe Sheikh Yahaya?
 
To me hata Africa ikawa wiped out completely sawa tu! Tuna faida gani?
Kama una faida n wewe alone mkuu,ila mim najivunia kuwa mwafrika na Nina faida mbele za Mungu.Elimu ya wazungu imeathiri ubongo wako Hadi hujitambui who you are
 
Tuliopo Mikoa ya kaskazini nawakumbusha tu nyuzijoto ni 21-23°C halafu virusi havikai kwenye nyuzijoto 30.
Muda wa kukimbilia Dar huu
 
Huu ugonjwa ulishapita nchini November December na January and population sasa iko immune. Yale mafua hatari wengi walihisi ni malaria fulani, ukienda hospitali hamna kitu kwa kuwa hatuna vipimo vya hawa virusi katika zahanati zetu. Mungu tu anasaidia.

Aliye nacho huongezewa na acha waongezewe. Sijui ikiwa hili tukio afya walieleza ilikuwa nini zaidi ya kusema stay hydrated. Kila kitu kiliuma vibaya hadi mifupa na kukosa nguvu kabisa. Una-sweat hadi hujawahi ona na hadi maumivu makali sehemu za kiuno na uti wa mgongo, kikohozi, ukiacha koo kuwasha na homa kali ssana inayodumu kwa siku tatu na kisha inaishia zake unarudia kazi.

Unajisikia kufa kufa. Kwa aliyeugua pia kipindi hiki ajieleze alivyojisikia haya mafua yalikuwa hatari na afya walikaa kimya nafikiri. Ingekuwa una kitu kama diabetes unapita kwa ile dehydration na homa kali balaa.

Waafrika nafikiri wana kinga ya mafua mengi linapokuja jambo la virusi vya mafua na pengine hata hii CORONA. Nawaza na kuunganisha dots tu.
Ni last week tu nimejiskia hizo hali i swear huwezi hata kula,unakohoa,huku kamasi,mara mgongo unauma,pumzi inabana,kichwa inauma kooni hapo balaa.
Nikachuna siku 4 job.
Kuanzia jana niko fiti kabisa
 
Tuliopo Mikoa ya kaskazini nawakumbusha tu nyuzijoto ni 21-23°C halafu virusi havikai kwenye nyuzijoto 30.
Muda wa kukimbilia Dar huu
Usidanganywe.
Australia na Iran mbona kina joto na mdudu yupo?
Wewe zingatia maelekezo ya wizara ya afya
 
kwa wale waliotumia kiasi kikuba cha
Chloroquine wapo safe zaidi
 
ANZA KUIFIKIRIA KORONA
-kisha fikiria Daladala za mbagala
-Kisha fikiria mwendokasi
-kisha fikiria mabasi ya mikoani
-kisha fikiria msikitini siku za ijumaa
-kisha fikiria kanisani siku za jumamos na jumapil
-kisha fikiria kwenye masoko yetu
-kisha fikiria kwenye vibanda umiza
-kisha fikiria kwenye mashule yetu ya serikali
- kisha fikiria tamaduni zetu watanzania
-kisha fikiria umakini wa wasimamizi wetu

Mdomo wangu unajizuia lakini Nausikia Moyo wangu ukiniambia R. I. P

-fikiria umakini wa marekani lakini umeshindwa kuzuia korona
-fikiria teknolojia ya China lakin imeshindwa kuzuia Korona
-Fikiria nguvu ya Italy lakin nao wameshindwa kuzuia Korona

KILA MTU KWA IMANI YAKE AMUOMBE MUNGU ANAYEMUAMINI ILI NCHI YETU HII ISIGUSWE NA GONJWA HILI

Amen.

Jr
 
.
IMG-20200315-WA0028.jpeg


Jr
 
Mshana Jr,
Zaidi fikiria siku serikali itakapotamka watu kubaki majumbani ili kudhibiti kasi ya maambukizo. Wengi wanaoishi hand to mouth(asilia mia kubwa ya watanzania) watapata shida kubwa kweli kweli.
 
Zaidi fikiria siku serikali itakapotamka watu kubaki majumbani ili kudhibiti kasi ya maambukizo. Wengi wanaoishi hand to mouth(asilia mia kubwa ya watanzania) watapata shida kubwa kweli kweli.
Tuombe Mungu hili lisitokee.. Watz hatuna utamaduni wa kuhifadhi chakula ndani ama kuwa na hakiba ya dharura

Jr
 
Back
Top Bottom