Updates za Corona Tanzania

Updates za Corona Tanzania

Natambua umahiri wetu wa kuvifanya vitu serious kuwa mizaha. Natambua ujuzi wetu wa kuyageuza majanga kuwa manufaa ya kisiasa.

Hivi ni kipi kikubwa tumekifanya kama taifa cha serious kujikinga na hili gonjwa linalotaka kuwa janga la dunia?

Nimemsikia Waziri wa Afya akikutangazia umuhimu wa kutoshikana mikono wala kukumbatiana wakati wa kusalimiana kama ilivyo jadi yetu. Wanasiasa wakalibeba hili mzobe mzobe. Mengine yote sidhani kama yamepewa kipaumbele.

Waziri katangaza kila mkoa utenge maeneo maalum ya kuchunguza wenye dalili na viashiria vya huu ugonjwa.

Je, hili limetekelezwa?
Je, kuna vifaa ya kutosha kwenye hili?
Je, bajeti imetoka wapi?
Je, kuna wahudumu wa dharura wenye uelewa na huu ugonjwa wameandaliwa?
Je, sahihi ni kutenga vituo kila mkoa ama kila wilaya?
Je, mpaka sasa ni mikoa mingapi imelitekeleza hili?
Je, kuna changamoto yoyote?
Je, kuna kipindi maalum kwenye vyombo vya habari kutoa mapya ya kila siku kuhusiana na huu ugonjwa?

Hakika maswali ni mengi sana. Lakini nilichokiona kwenye huu ugonjwa ni mizaha na kukosa umakini. Hatuna takwimu rasmi zozote mpaka sasa za chochote kuhusiana na huu ugonjwa. Hatujaona umakini wowote kwenye maandalizi ya dharura. Chukulia mfano mkoa wa Pwani kutoka Mkuranga mpaka Bagamoyo utenge kituo kimoja tu cha ukaguzi wa corona, inawezekana kweli!?

Kinachopigiwa chepuo sasa ni kusalimiana bila kushikana mikono, eti kugongesha miguu. Mmh! Tumeiona kwa viongozi, lakini nyie msioshikana mikono sasa si mlikaa chumba kimoja kwa madakika mengi tu? Je, mlitumia viziba midomo na pua?

Hivi kwani corona ni ugonjwa wa ngozi? Iweje wachezaji uwanjani wazuiwe kusalimiana kwa kushikana mikono eti ni mojawapo ya kampeni ya kupambana na corona wakati huo huo wachezaji haohao watakuwa pamoja uwanjani kwa dakika 90+ wakishikana, wakivutana, wakiangukiana wakipumuliana? Vipi na wale mashabiki watazamani kwa maelfu walio majukwaani? Tuna abiria kwa maelfu wanasongana kwenye vyombo vya usafiri. Kwenye masoko. Kila mahali.

Bado hatuko serious na mizaha ndio imetawala kupitia siasa. Mungu pekee ndio anatubeba. Kitengo cha dharura kitaifa hakijasema chochote. Kipo kimya kabisa. Vyombo vyetu vya habari ni siasa na wanasiasa mwanzo mwisho. Viziba pua na midomo vimepanda bei maradufu. Box lilikokuwa linauzwa elfu 10 piece 50 sasa hivi linauzwa elfu 40 na hapo ugonjwa haujachanganya. Ukithibitika upo nchini na tukatakiwa kutumia hivyo vifaa tutafanyaje?


Jr

Watanzania katika Ubora wao. Hawana jema. Badala ya malawama mtandaoni andika hata Paragraph moja ya kuelimisha.

Unadhani ugonjwa huu Serikali ndo yenye majibu yote. Ni mapambano ya nyumba kwa nyumba. Information ulizopata toka Serikalini Ni hatua Kubwa pia. Awareness ni jukumu letu sote. Ndo tukumbushane. Mjifunze kuwa Part Solution. Consumers wa hapa sio Serikali, nini sisi.

Ulaya Sasa tumeombwa kubaki Ndani. Je wewe utakubali. OSHA mikono nk. Ukipata dalili sio utoke uende Hospital. NO. piga simu. Waje wakupime hapo ulipo. Hata huyu mwanamke aliyejitenga kakosea sana kwenda mwenyewe Hospital. Ila yameshatokea. Tusaidiane mambo haya madogo Madogo. Hizo maski hazina uhakika wa kusaidia mapambano. Kubaki nyumbani Ni Option bora. Akitoka baba au mama Basi awe mwangalifu.

Tuelimishe sio kuleta mbwembwe. Do your part.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Muone huyu, eti ulaya tumeombwa kubaki ndani..... Nyenyenyenyeeee
Watanzania katika Ubora wao. Hawana jema. Badala ya malawama mtandaoni andika hata Paragraph moja ya kuelimisha.

Unadhani ugonjwa huu Serikali ndo yenye majibu yote. Ni mapambano ya nyumba kwa nyumba. Information ulizopata toka Serikalini Ni hatua Kubwa pia. Awareness ni jukumu letu sote. Ndo tukumbushane. Mjifunze kuwa Part Solution. Consumers wa hapa sio Serikali, nini sisi.

Ulaya Sasa tumeombwa kubaki Ndani. Je wewe utakubali. OSHA mikono nk. Ukipata dalili sio utoke uende Hospital. NO. piga simu. Waje wakupime hapo ulipo. Hata huyu mwanamke aliyejitenga kakosea sana kwenda mwenyewe Hospital. Ila yameshatokea. Tusaidiane mambo haya madogo Madogo. Hizo maski hazina uhakika wa kusaidia mapambano. Kubaki nyumbani Ni Option bora. Akitoka baba au mama Basi awe mwangalifu.

Tuelimishe sio kuleta mbwembwe. Do your part.


Sent using Jamii Forums mobile app

Don't make a promise you can't fulfill...
 
Adjustments.jpg



Sent from my iPhone using Tapatalk
 
Namba za kupiga simu bure endapo utaona una dalili au utaona mtu mwenye dalili za Ugonjwa wa Korona

0800110124
0800110125
Namba hizi kupiga Ni bure hata kama hauna salio kwenye simu yako.

DALILI ZA UGONJWA WA CORONA

Dalili zionekanazo mara kwa Mara:
• Homa
• Kikohozi kibichi
• Uhemaji wa tabu
• Maumivu ya mwili
• Kuuma kwa koo mfano wa
matonses (tonsillitis)
• Kukosa hamu ya kula

Dalili za mara chache:
• Kuhara
• Kutapika
• Kichwa kuuma
• Kukohoa damu
• Maumivu ya kifua

Nani hupatwa na korona?

• Watu wote (wakike kwa kiume) waweza
kudhurika na korona
• Wenye maradhi yanayoshusha kinga mwili huwa na hatari kubwa Zaidi.
• Wazee pia wapo katika hatari kubwa kupatakorona kwani wana kingamwili hafifu.

KINGA:

• Kuosha mikono vizuri kwa maji safi na sabuni
• Tumia vikinga pua na mdomo (masks) ikiwa unahudumia washukiwa wa korona.
• Epuka kugusa na kurekebisha kikinga mdomo na pua (mask) na uso.
• Zingatia walau umbali wa futi 6 kutoka kwa mgonjwa mwenye korona
• Hakuna chanjo mpaka sasa

Kirusi cha korona katika mwili wa
binadamu:

• Huchukua siku 2 mpaka 14 (wastani siku 5) kwa binadamu kuanza kuonesha dalili baada ya kuambukizwa na virusi vya korona (incubation perion)
• Huambukizwa kwa njia ya matone yatokanayo kwa kukohoa au kugusana moja kwa moja.
• Epuka kusalimiana kwa mikono

Jr
 
halafu kibaya zaid kumbe hata maabara ni mpk kipimo kije Dar mbona mwanzo kulikuwa na majibu mepesi sana kwa washukiwa wasiwasi wangu waathirika wanaweza kuwa wengi maana huyu mama kama kajitambua tu ila angeamua kujichanganya mtaani kama wanavyofanya wachina hakuna wa kujua
 
.
halafu kibaya zaid kumbe hata maabara ni mpk kipimo kije Dar mbona mwanzo kulikuwa na majibu mepesi sana kwa washukiwa wasiwasi wangu waathirika wanaweza kuwa wengi maana huyu mama kama kajitambua tu ila angeamua kujichanganya mtaani kama wanavyofanya wachina hakuna wa kujua
IMG-20200316-WA0082.jpeg


Jr
 
Kama sisi watanzania tulioko China tupo wazima, tangia mwezi wa 12 mpaka leo mwezi tatu, na sio watanzania tu waafrica wote, basi nyie mlioko TZ mtakua wazima mara 100000, embu ondoeni hofu msitishike na matangazo ya redioni, mitandaoni na kwenye TV, tunapo sema corona ina enea zaidi kwenye nchi za baridi kali hii point iamini kwa asilimia zote (nchi zenye majira ya WINTER ndizo zinazopata shida, hiyo ni bayolojia mhimu kwa corona kwa sababu anaenea zaidi kwa njia ya hewa, kukiwa na baridi kali membrane za kwenye pua zinaingilika kiurahisi na huyo kirusi) na baridi inayo zungumziwa hapa ni ile kali ambayo unapatikana kwenye nchi za SUBTROPICAL Asia na ulaya, Africa nchi zake zipo TROPICAL joto lipo juu, sisi tuliopo China baridi tunayo izungumzia hapa ni ile ya 1, 2, 3 mpaka 10, yaani ikifika 13 hiyo siku mnafurahi, jua likiwaka basi lazima mfurahi.Hivyo ndivyo navyo elewa kuhusiana na huyo kirusi. Kama ukisikia mwaafrica kapata corona basi ujue katoka nao nchi mojawapo yenye baridi kali lkn immunity za waafrica zipo very resistive kwa hiyo hawezi chukua muda kupona. Immunity ya waafrica iko resistive kwasababu ya hali ya maisha magumu tuliyo pitia, mazingira tunayo ishi Africa ni machafu, tunaishi na vimelea vya magonjwa ya kila aina, mtu anaweza kuumwa mafua na kupona bila kwenda hospitali, maana yake kinga yake imekua ikipambana yenyewe bila kumeza dawa. Vumbi ndio usiseme, vumbi linaingia mwilini likiwa na vimelea kibao lkn mtu anaendelea kuishi. Mazoezi tuliyo fanya kila siku tangia tukiwa wadogo kwa kutembea kwa miguu bila kupanda magari kwenda sehemu mbalimbali labda ni shuleni hayo yote yanaongeza metabolic rate ya mwili. Tofauti na wenzetu wamezaliwa kwenye magari kwa hiyo muda wote ni magari no time ya kufanya mazoezi. Na ndio maana japo kuwa kirusi huyo anaaishi kwa baadhi ya wanyama lakini hana uwezo wa kuwadhuru kwasababu ya miili ya hao wanyama ina high metabolic rate. Na hapa ndipo inapokuja concept ya kunywa MAJI YA MOTO mara kwa mara ili kuongeza metabolic rate ya mwili. MAJI YA MOTO yanazo faida nyingi tu mbali na hiyo ya kuongeza metabolic rate ya mwili.

Jr
 
Back
Top Bottom