Ikiwa arab springs unaowasema, waliandamana pamoja na kwamba walikuwa na maisha mazuri, huoni kama unajenga hoja nzuri na ya msingi kwa Watanzania wasiokuwa na mavazi, malazi, chakula, wala kesho yao hawaifahamu kama ipo wanahaki zaidi ya kuandamana ili wajikomboe? Kumbuka hawakupenda kuwa maskini kama walivyo. Ni serikali lya ccm ndiyo ime breed Tanzania hiyo unayoidhihaki. Bahati nzuri umesema hadharani tumekusikia. Sasa tunaandamana hata sisi tusio wana CHADEMA, ili kuunga mkono harakati za ukombozi.
Ni dhahiri kabisa ninyi mnashangilia matabaka ya watu duni wanaoishi katika maisha yasiyostahiki kwa binadamu na ambayo mmeyategnezza kwa utawala wenu wa miaka 50. Sasa hao unaowafanya si binadamu, ndio wenye nchi. Wazazi wao walilipa kodi za maendeleo ya nchi, ninyi mmebinafsisha maendeleo na kuwaacha vijana wakiishi kama nguchiro pori. Mmetumia raslimali za taifa kujinufaisha ninyi na watoto wenu. Mnatengeneza utawala wa kifalme kinyume na democrasia. mnatumia ubabe kuzidi kuwadidimiza na sasa mnawazomea hadharani. Elimu bora mmewanyima. Huduma za afya ni zenu tu, wao wanateketea kwa maradhi yanayozuilika na kutibika kwa sababu hamjali maisha yao.
Wanadai haki zao, unaasema bila haya, eti kwa kuwa ni maskini sana, hawana hata haki ya kudai kitu. Afadhali wangekuwa na maisha isha kama angalau Arab springs, wangekuwa hata na hadhi ya kusikilizwa.
Hata mwehu kuna siku huwa anajitambau. Fahamu zinamrudia anaanza kutaja majina ya rafiki zake walikuwa wanacheza wote.
Sasa Watanzania maskini, wajinga, wafu watarajiwa, waliotolewa muhanga kwa ufisasi na umangi meza wenu, wameamka. Wanajua kufa watakufa wakati wowote. Hata msipowapiga risasi, watakufa kwa kukosa huduma za afya, watauawa kwa uharibifu wamiundo mbinu mibovu, watakufa kwakukosa makazi bora, watakufa kwa kukosa elimu sahihi ya maisha, watakufa kwa uharifu unaoongezeka kila mara, kama si leo ni kesho. Hata msipowapiga risasi, wanajua watakufa kwa madawa fake na vyakula vyenye sumu vinavyoingizwa kifisadi.
Wanajua seriakli ingekuwa makini, maisha yao yasingekuwa yalivyo na wangeona mwanga na mwelekeo wa njia ya kupita. Sasa hawana cha kupoteza. Wameamua ni afadhali wauae na mkono wa serikali inayowadharau, kuwanyonya na kuwaona hawafai kama uliyvosema hapa, wakidai haki zao, kulilko kukaa wasubiri kufa kwa umaskini uliokithiri bila jitihada.
Sasa waueni. Lakini pia mtafute mahali ya kujificha maana bila shaka vituo vya polisi si vingi kiasi cha kuwaweka polisi na koo zao zote, pamoja na watu kama wewe mnaojitangaza hadhari kuwa ni adui wa Watanzania.
Bora hata arabs spring movement waandamanaji walikuwa na vyakula na maji ya kutosha ya kuweza kuandamana hata kwa mwezi mzima bila kuchoka wla kuhisi njaa maana wana food, shelter, na pia clothes, ila nyie wahuni, vibaka, wanywa viroba, wavuta unga wa arusha hamna hata mia mnataka muandame ili mkakwapue vitu vya raia wapenda amani...hamwezi andamana hata kwa masaa manne!
Nnavyowatamani mkijichanganya ntawachakaza huko frontline!!