Ukamanda wa kwenye mitandao tu, nendeni uwanja wa mapambano tuone nani mwanaume, mliokuwa mnasema mnaenda mbona bado mko ktk mitandao tu mkiuliza kinachoendelea?
By Emma.
lazima tuandamane bila kuogopa vitisho vya polisi kesho lazma tujitokeze kwa wingi hakuna mwenye uwezo wa kushindana na nguvu ya umma ..WAZALENDO WENZANGU MSIKATE TAMAA MUDA WA UKOMBOZI UMESHAKARIBIA VIVA CDM DAIMA
Kwa taarifa za maandalizi ya kufanyika kwa maandamano ya amani yatakayofanyika kesho tarehe 20/9/2014 yatakayofanyika kesho nchi nzima kupinga bunge la katiba linaloendelea mjini Dodoma, ambalo halina uhalali wa kuendelea, kwa upande wa Arusha kesho kutakuwa na njia sita tofauti kuanza maandamano yasiyo na kikomo.
Kwa taarifa hizo maandamano yataanzia Phillips-Mount Meru Hotel kupitia AICC, Central Police hadi Kilombero, Mengine yataanzia maeneo ya Sakina Machinjioni kuelekea mianzini, yatashuka na Kaloleni, Mwenge hadi Kilombero, Mengine yataanzia Majengo, Mbauda hadi Kilombero, Mengine yataanzia Kwa Morombo-Olasiti kuelekea Ngusero, Sonbetini, Corner Nairobi hadi Kilombero, Mengine yataanzia Kijenge, Uzunguni, Clock Tower hadi Kilombero.......
Kwa upande wa Arumeru maandamano yataongozwa na Dogo Janja, tutawajuza kila kitakachokuwa kikijiri, na upande wa Arumeru Magharibi maandalizi ni makubwa, wananchi wanatamani yaanze leo kama ilivyo kwa Arusha mjini.....
Wao wamebeba bunduki, mabomu, marungu na pingu kuwaziba midomo wanaodai haki kwa amani,..... sisi tumebeba vitambaa vyeupe mikononi kuashiria tunadai haki kwa amani..... Dunia itashuhudia maandamano haya ya amani kesho..
By Henry Kilewo
Jeshi la polisi Wilayani Mwanga limesitisha maandamano ya Chadema ambayo yanapaswa kufanyika kesho Wilayani Mwanga.
Tunapenda kuliaarifu jeshi hilo ya kuwa maandamano yatafanyika kama tulivyopanga kwakuwa tulitoa Taarifa kwa muda unaotakiwa kisheria na sasa ni utekelezaji , vile vile tunatimiza wajibu wa kikatiba.
Polisi watakao jaribu kuingia Barabarani kuzuia maandamano hayo amabayo nihitaji la Katiba tutawachukulia hatua sitahiki za kisheria.
Wanamwanga wote msimamo wa maandamano ni ule ule mfike kwa wingi kama ambavyo tumekubaliana.
Hakuna wa kumtisha wala kumzuia Lema katika utekelezaji wa maagizo ya chama.
Kamuulize Mwigamba anaijua shughuli yake baada ya kufumwa na waraka wao wa kusaliti chama.
Ova.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.