Update: Mashtaka dhidi ya makampuni manne ya simu

Update: Mashtaka dhidi ya makampuni manne ya simu

UPDATE MASHTAKA DHIDI YA MAKAMPUNI MANNE YA SIMU.

Bashir Yakub, WAKILI
0714047241
.

Niliwaahidi kwamba nitakuwa nikiwaeleza kila tukio kuhusu mchakato wa kuyashitaki makampuni ya simu kwa unyonyaji.

Mnakumbuka kuhusu yale mambo yetu matano, vifurushi kutokuwa na muda wa kuexpire,ruhusa ya kuhamishiana vifurushi, kutochanganya vifurushi na muda wa kawaida wa maongezi bila ruhusa ya mtumiaji, vifurushi vya watu kuisha wakati mtu hajatumia au ametumia kidogo, na utaratibu wa kutoa taarifa kifurushi kinapokaribia kuisha na si kinapoisha.

Muda wa siku thelathini niliowapa haujaisha ukiisha nitawaambia.

Aidha, niliitwa na ndugu wa TCRA kitengo cha walaji. Nilifanya nao majadiliano kuhusu mambo haya na kuwaeleza nia yangu ya kuhakikisha Mtanzania analindwa. Nimeelewana nao vizuri.

Zaidi, wanaandaa kikao ambacho kitakuwa kati yangu, TCRA kitengo cha walaji, na makampuni yote ya simu. Mimi nilikusudia kuyashitaki makampuni manne(the big 4) lakini wao wamependekeza kikao kijumuishe wote. Ni jambo zuri na nimelipokea.

Na nimewaeleza kuwa hatua yoyote ambayo inalenga kuondoa unyonyaji wa aina hii na usumbufu mwingine wowote wanaoupata Watanzania wakati wakitumia simu, ninaupokea kwa mikono miwili. So far, kikao kinaweza kuandaliwa wiki ijayo ili kuona tunafikia wapi.

Zaidi, leo nimepata taarifa ambazo sijathibitisha kuwa Airtel wamefanya mabadiliko kwenye utumiaji wa data ambapo muda wa kifurushi cha data ukiisha hawaunganishi tena moja kwa moja na salio, bali sasa wameweka chaguo(option) ambapo wana kuuliza ikiwa unataka kuendelea kutumia muda wa kawaida au ungetaka kujiunga upya. Mnaotumia Airtel angalieni hili likoje.

Hata hivyo, Airtel kama wamefanya hivyo nawaambia haitoshi. Ni LAZIMA watekeleze na hayo mengine. Lakini pia ni LAZIMA watoe taarifa ya masaa 72 kabla ya mabadiliko yoyote kama Kanuni ya 5(5) ya Kanuni za Kielektroniki na Mawasiliano ya Posta GN No.61/2018 kuhusu kumlinda mlaji inavyotaka.

Wasifanye mabadiliko kwa kujifichaficha hii nchi sio yao, mtumiaji ana haki ya kujulishwa mabadiliko.

Pia, kwa wale mnaonipigia simu kunitisha nitumie jukwaa hili kuwaambia kwamba nitafurahi sana, tena sana, kufia kwenye vita hii kuliko kufia sehemu nyingine yoyote. Mwanaume kamili hafi kwa malaria bali hufia mambo kama haya.

Mwisho, niwashukuru nyinyi Watanzania kwa namna mlivyopokea jambo hili. Sijawahi kuona jambo ambalo Watanzania wote wanaunga mkono kama ilivyo kwa hili. Hii inadihihirisha ni kwa namna gani mlikuwa mmechoka.

Niishie hapa, nitawapa taarifa za kikao cha wiki ijayo.

Pia Soma

Kama kila mtaalamu wetu angetumia utaalamu wake kwa maslahi ya wote, kama ulivyoamua wewe kufanya, nchi hii ingekuwa mbali sana kimaendeleo. Ahsante kwa kujitoa kwa ajili ya wote!
 
Safi sana kaka malalamiko yalikua mengi mno na hivi vifushi jamani unapewa gb kibao lakini zina isha fasta kama zina peperushwa na upepo wa kisulisuli tumechoka kuonewa kaka hongera sana naunga mkono juhudi.
Ikiwezekana kama kitakua kikao huru kwa walaji wote sitakosa kuhudhuria Barikiwa sana.
 
Kweli inapoona mambo flani katika nchi yanakwenda sahihi jua kuna watu waliopigania na pengine wao kua katika matatizo ili wewe unufahike
Haya mambo sikuwai kuyaona hata sikumoja ila eatel wameanza kutekeleza maagizo
Yani ukiishiwa bando sasahivi kabla ya kuendelea unaulizwa kama utatumia salio la kawaida au unajiunga
Screenshot_2019-11-15-17-07-52.jpeg
 
Safi sana kaka malalamiko yalikua mengi mno na hivi vifushi jamani unapewa gb kibao lakini zina isha fasta kama zina peperushwa na upepo wa kisulisuli tumechoka kuonewa kaka hongera sana naunga mkono juhudi.
Ikiwezekana kama kitakua kikao huru kwa walaji wote sitakosa kuhudhuria Barikiwa sana.
M sign hii petition, Wakili Bashiri Yakub ameianzisha....

Wakili Bashir Yakub anayashitaki makampuni manne ya simu. Kusoma maelezo ya petition na kuweka sahihi yako, tumia link ifuatayo:

Signez la pétition

Sambaza ujumbe huu kwenda groups zako zote na mitandao ya kijamii.
 
Kuna mwanasheria alikuja na wazo la kuyashtaki makampuni ya simu tz kwa sababu ya kuweka kikomo(Limited time) kwenye manunuzi ya bando baada ya kununua,alifikia hatua nzurii kidogo na alitupa mrejesho sisi wanajukwaa na kongole nyingi tulimpa.
Siku hizi hatujuzi kafikia wap na kesi inaendaje,Tafadhari braza kokote uliko tuambie kipi kinaendelea.
 
Back
Top Bottom