Update: Mashtaka dhidi ya makampuni manne ya simu

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Bravooo Arawa usiangalie nyuma songa mbele sisi tupo nyuma yako wanao kutisha ni waoga wa fikra mbadala na ni wahujumu haki za wananchi Mungu atakulinda Haki huinua Taifa
 
Komaa mzee, maana kuna malalamiko mengi ya watu kukatwa pesa zao bila kutumia na hata vifurushi kuisha bila kutarajia. Kama TCRA wameshindwa kazi ya kuthibiti haya makampuni ya simu kuwaibia wateja, ni bora sasa watu kama nyie mpewe hiyo kazi
 
Kumbe inawezekana aisee, endelea kukomaa naona mahakama ya Kenya tayari imeweka precedent nzuri
#MITANDAONI Baada ya
@SafaricomPLC
ya Kenya kuondoa "ukomo wa vifurushi" vya muda wa maongezi na intaneti kwa wateja wake, naibu waziri wa Mawasiliano, Atashasta Nditiye ameelezea msimamo wa Serikali kuhusu vifurushi. Bashir Yakub
 
Hapo umejiona umeongea point kabisa.
 
Narudia tena kusema, kugusa makampuni ya simu ni kugusa maslahi ya moja ya chanzo kikuu cha mapato cha serikali...

Terms zozote zitazofikiwa kama muafaka bado zitaegemea kwa makampuni ya simu
Na haohao wakubwa wataguswa moja kwa moja.

Hawatakubali.

Hii vita ni kubwa sana. Inatakiwa wanasheria nguli wahusishwe moja kwa moja.
 
Hivi mnalazimishwa kujiunga vifurushi? Mbona haya ni masuala yaliyo wazi sana kibiashara? Vifurushi ni mkataba wa hiari wenye vigezo na masharti yake unayoyakubali kuyazingatia!!!B
Hivyo vimekuwa ni mahitaji muhimu/ msingi (basic needs) katika dunia ya sasa. Hivyo huwezi amua kuweka bei kadiri unavyojisikia. Ndio maana zinawekewa hadi mamlaka ili kulinda na maslahi ya walaji.
 
Hivi mnalazimishwa kujiunga vifurushi? Mbona haya ni masuala yaliyo wazi sana kibiashara? Vifurushi ni mkataba wa hiari wenye vigezo na masharti yake unayoyakubali kuyazingatia!!!B
Tatizo hujaelewa maada inahusu nini,narukia tu ili mradi wewe ni mtumiaji wa simu,nenda mwanzo kasome mtoa maada anakusudia nini?
 
Zero
 
Umesoma contract law umemaliza, hukutaka kujua kuna sheria zingine za mawasiliano...

Mfano. Ukiwapigia wana kupa alert kuwa simu yako ita rekodiwa, kwa maana kumrekod mtu bila hidhini yake ni kosa...
 
We jamaa ni kiazi. Huwezi kuniuzia chipsi unipangie muda wa kula. Kwamba nisipokula mpaka saa fulani unaninyang'anya sahani.
 
Pambana mkuu na Mungu akuajaalie maana haya makampuni ya mitandao ni janga mfano Tigo ile saizi yako huwezi angalia hata salio la kifurushi chako ni mwendo wa kukalili muda uliojiunga na siku
 
Angalizo mkuu, pesa haijawahi kushindwa jambo kwa binadamu anaepumua, angalia usije ukatusaliti kwa kupokea mlungula wa maana na kuyoyoma kusikojulikana.
Kupitia hili jambo naamini utakutana na vitisho kama vilivyoanza theni ukikomaa utakutana na mlungula wa haja kitu ambacho naamini kukikwepa inahitaji moyo wa pekee maana hata yuda eskarioti ilimshinda.
Sisi Watanzania tupo nyuma yako na tutakukumbuka daima kama utalifanikisha jambo hili muhimu linalotunyonya uchumi wetu mifukoni na kuhamishia kwa wezi/wahuni wachache.
 
Umesoma contract law umemaliza, hukutaka kujua kuna sheria zingine za mawasiliano...

Mfano. Ukiwapigia wana kupa alert kuwa simu yako ita rekodiwa, kwa maana kumrekod mtu bila hidhini yake ni kosa...
Rejea post #82 utaona nimeeleza kanuni za terms za mkataba zina apply kama offer ilivyokuja isipokuwa pale ambapo kuna sheria inasema matakwa fulani lazima yazingatiwe.

Halafu humu hoja ni mkataba wa vifurushi sio kuingiliwa kwa mawasiliano hilo sasa ni swala la katiba na mambo ya faragha za mtu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…