Uongozi wa UDOM wajibu madai ya kuwepo kunguni kwenye mabweni ya Wanafunzi

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,812
11,989
Baada ya memba wa JamiiForums.com kudai kuwa kuna changamoto ya Wadudu aina ya Kunguni kwenye mabweni ya Wanafunzi wa Chuo Kukuu cha Dodoma (UDOM), ufafanuzi umetolewa kutoka kwenye mamlaka ya chuo hicho.

Taarifa ya awali ya Kunguni hii hapa - Kunguni wanatutesa Wanafunzi tunaolala kwenye mabweni ya UDOM
KUNGUNI UDOM.jpg

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Masoko wa UDOM, Rose Mdami anajibu madai hayo kwa kusema:

“Ukweli ni kwamba suala hilo halina kweli japokuwa sisi kama Chuo tunaelewa kunapokuwa na wingi wa watu kunakuwa na tishio la magonjwa mbalimbali ikiwemo uwepo wadudu hao aina ya Kunguni, ndio maana kila Wanafunzi wanapotoka Chuo tunaingia gharama kubwa ya kupuliza dawa ili kuhakikisha kila kitu kipo sawa.

“Ukija chuoni hata sasa utaona tumefanya kazi kubwa na kila kitu kipo sawa lakini changamoto kubwa tunayoipata ni suala la kusisitiza usafi kwa Wanafunzi wetu, wanapokuja wanakuta mazingira masafi, wanapoanza kuweka vyakula kwenye mabweni ndipo wanapoanza kufuga hao wadudu.

“Uchafu unapokithiri ndipo Kunguni nao wanavyopata nafasi, sisi hatufugi Kunguni ila wanatokana na uchafu.

“Chuo tumeweka watu wanafanya usafi kila kukicha kupitia kampuni, suala la kufanya usafi binafsi ni la mtu binafsi kama kwenye chumba chake anacholala atashindwa kuwa msafi itakuwa sio sawa kwa mtu kwenda kumtandikia kitanda.

“Suala la kunguni ni letu sote, ni wajibu wa Wanafunzi kuwajibika na kuchukia kuwa na hao wadudu, tunatimiza wajibu wetu kwa kupuliza dawa upande wetu kama tulivyofanya, wanapokuja Wanafunzi waendeleze kwa kila mmoja kuchua tahadhari binafsi.

“Tunaomba Wanafunzi wanapokuta mazingira safi waendelee kuyatunza kama walivyoyakuta.”
 
Kweli wanachuo,hasa wa kiume ni wachafu sana.

Hostel za kike hazina hiyo kadhia,,asilimia kubwa ni wasafi.

Ukiingia Dom la kiume,koridoni tu unakutana na hewa nziito
Hadi unajiuliza sijui wanaishije
Na hapo vyoo,makorido yoote kuna wafanya usafi, wanafanya usafi always.
 
Baada ya memba wa JamiiForums.com kudai kuwa kuna changamoto ya Wadudu aina ya Kunguni kwenye mabweni ya Wanafunzi wa Chuo Kukuu cha Dodoma (UDOM), ufafanuzi umetolewa kutoka kwenye mamlaka ya chuo hicho.

Taarifa ya awali ya Kunguni hii hapa - Kunguni wanatutesa Wanafunzi tunaolala kwenye mabweni ya UDOM

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Masoko wa UDOM, Rose Mdami anajibu madai hayo kwa kusema:

“Ukweli ni kwamba suala hilo halina kweli japokuwa sisi kama Chuo tunaelewa kunapokuwa na wingi wa watu kunakuwa na tishio la magongwa mbalimbali ikiwemo uwepo wadudu hao aina ya Kunguni, ndio maana kina Wanafunzi wanapotoka Chuo kinaingia gharama kubwa ya kupuliza dawa ili kuhakikisha kila kitu kipo sawa.

“Ukija chuoni hata sasa utaona tumefanya kazi kubwa na kila kitu kipo sawa lakini changamoto kubwa tunayoipata ni suala la kusisitiza usafi kwa Wanafunzi wetu, wanapokuja wanakuta mazingira masafi, wanapoanza kuweka vyakula kwenye mabweni ndipo wanapoanza kufuga hao wadudu.

“Uchafu unapokithiri ndipo Kunguni nao wanavyopata nafasi, sisi hatufugi Kunguni ila wanatokana na uchafu.

“Chuo tumeweka watu wanafanya usafi kila kukicha kupitia kampuni, suala la kufanya usafi binafsi ni la mtu binafsi kama kwenye chumba chake anacholala atashindwa kuwa msafi itakuwa sio sawa kwa mtu kwenda kumtandikia kitanda.

“Suala la kunguni ni letu sote, ni wajibu wa Wanafunzi kuwajibika anachukia kuwa na hao wadudu, tunatimiza wajibu wetu kwa kupuliza dawa upande wetu kama tulivyofanya, wanapokuja Wanafunzi waendeleza kwa kila mmoja kuchua tahadhari binafsi.

“Tunaomba Wanafunzi wanapokuta mazingira safi wayaendele kama walivyoyakuta.”
Majibu yake hayajapinga uwepo wa kunguni..!!!
 
Kweli wanachuo,hasa wa kiume ni wachafu sana.

Hostel za kike hazina hiyo kadhia,,asilimia kubwa ni wasafi.

Ukiingia Dom la kiume,koridoni tu unakutana na hewa nziito
Hadi unajiuliza sijui wanaishije
Na hapo vyoo,makorido yoote kuna wafanya usafi, wanafanya usafi always.
Kweli kabisa mabweni ya kiume, watu ni wachafu kupita kiasi.

Nakumbuka tulipokuwa chuo, watu walikuwa wanashangaa jinsi room yetu(tulikuwa wawili) tunavyodeki kila siku.
Tunazuia watu wasiingie na viatu.

Room nyingine ukiingia hata oxgyen tuu unaitafuta kwa taabu.

Ushauri wangu:
swala la usafi lisisitizwe sana kuanzia primary, hadi sekondari. Ukienda advance ndio kuna watu wachafu kama si watu.

NB. Mara nyingi mtu mchafu hana maendeleo, maana akili yake nayo inakuwa haina mpangilio.
 
Kweli kabisa mabweni ya kiume, watu ni wachafu kupita kiasi.

Nakumbuka tulipokuwa chuo, watu walikuwa wanashangaa jinsi room yetu(tulikuwa wawili) tunavyodeki kila siku.
Tunazuia watu wasiingie na viatu.

Room nyingine ukiingia hata oxgyen tuu unaitafuta kwa taabu.

Ushauri wangu:
swala la usafi lisisitizwe sana kuanzia primary, hadi sekondari. Ukienda advance ndio kuna watu wachafu kama si watu.

NB. Mara nyingi mtu mchafu hana maendeleo, maana akili yake nayo inakuwa haina mpangilio.
Udom kumezidi🙌
Ukikatiza tu korido karibu na choo
Mungu wangu, unaweza utapike.
.mijitu imeshusha mizigo,, wengine wanalengesha tu wadada wa usafi wakimaliza tu, huyo anaenda tua mzigo wake, hataki kujichosha kwenda kisimani kuvuta maji ya kutosha.

Room za wakaka 90%zinanukaa.. 10% ndio pekee Kuna hali nzuri kiasi.

Wanafunzi ni wachafu kwa kweli.
 
Kweli wanachuo,hasa wa kiume ni wachafu sana.

Hostel za kike hazina hiyo kadhia,,asilimia kubwa ni wasafi.

Ukiingia Dom la kiume,koridoni tu unakutana na hewa nziito
Hadi unajiuliza sijui wanaishije
Na hapo vyoo,makorido yoote kuna wafanya usafi, wanafanya usafi always.
Chakushangaza na uchafu wao ni vipanga balaa hao hao ndio wakina mwingulu wa baadae kweli muumba hakupi vyote
 
Kweli kabisa mabweni ya kiume, watu ni wachafu kupita kiasi.

Nakumbuka tulipokuwa chuo, watu walikuwa wanashangaa jinsi room yetu(tulikuwa wawili) tunavyodeki kila siku.
Tunazuia watu wasiingie na viatu.

Room nyingine ukiingia hata oxgyen tuu unaitafuta kwa taabu.

Ushauri wangu:
swala la usafi lisisitizwe sana kuanzia primary, hadi sekondari. Ukienda advance ndio kuna watu wachafu kama si watu.

NB. Mara nyingi mtu mchafu hana maendeleo, maana akili yake nayo inakuwa haina mpangilio.
SAWA, KWAMBA OXYGEN INASHUKA HADI 2%, lakini je, kunguni wapo au hakuna ?
 
Back
Top Bottom