DOKEZO Kunguni wanatutesa Wanafunzi tunaolala kwenye mabweni ya UDOM

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
A

Anonymous

Guest
Sina haja ya kutaja jina langu wala kuandika maelezo mengi, lakini kwa ufupi mimi ni Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM). Kwakweli suala la kunguni UDOM limekuwa linasumbuwa na lina kera kwa muda mrefu.

Ajabu ni kuwa hakuna hatua zinazochukuliwa kwa sasa wadudu hao wamekuwa wengi sana yaani nahisi hata Ufaransa tunaposikia wamefunga vyuo hawajafikia huku, ni kero sana.

Kunguni hao wanapatikana kwenye mabweni tunapolala, mfano kwenye college ya Education ndio balaa.

Siku za nyuma uongozi wa chuo ulikuwa na kawaida ya kupuliza dawa kwenye mabweni, lakini ndani ya miaka hii miwili hali imekuwa tofauti.

Tulipofunga Chuo Juni na Julai 2023 tulitegemea tukirudi tutakuta wamepuliza dawa lakini hali imekuwa tofauti, matokeo yake watu tumeanza kulazimika kutandika na kulala chini kwani vitandani hakulaliki.

Changamoto hii sio kwenye college yetu pekee bali karibia zote Wanafunzi tumekuwa tukilalamika kunguni.


Majibu ya UDOM yako hapa: Uongozi wa UDOM wajibu madai ya kuwepo kunguni kwenye mabweni ya Wanafunzi
 
Acha kudeka,

Chukua heater, chemsha maji mengi ya moto, osha hivyo vitanda kwa maji moto kila kona,

Chukua godoro lako, kung'uta vizuri kabisa, toa folonya ulifue, fua mashuka yako then pasi kwa moto mkali,
You are good to go,

Short cut, nunua dawa za kuua wadudu, pulizieni humo ndani, hazizidi buku 5, kwa watu wanne ni 1250 each,

Tuache kulalamikia vitu vidogo tunavyoweza solve wenyewe, sisi sio toddlers bana
 
pole sana. Dawa ni 3500. Bando ni 2100 beer ni 1500 kumuhonga dem ni 50000 na mpo zaidi ya 100 kwani mkijichanga mkaamua kutokomeza kunguni mnashindaa?

Kweli kama uongozi haupigi dawa ndio wasomi muamje kujitesa? Haya tufanye hawapigi na awamu ijayo mtaendelea kulala chini wasomi.

Msikubali unyonge tena nyie wasomi hapo ndio mnafanya kama sehemu ya kutoa malalamiko yenu japo kunguni mnawaleta wenyewe.

Alafu muda mwingine na hao kunguni watakula wapi sasa😂😂
 
Acha kudeka,

Chukua heater, chemsha maji mengi ya moto, osha hivyo vitanda kwa maji moto kila kona,

Chukua godoro lako, kung'uta vizuri kabisa, toa folonya ulifue, fua mashuka yako then pasi kwa moto mkali,
You are good to go,

Short cut, nunua dawa za kuua wadudu, pulizieni humo ndani, hazizidi buku 5, kwa watu wanne ni 1250 each,

Tuache kulalamikia vitu vidogo tunavyoweza solve wenyewe, sisi sio toddlers bana
Sawa, tumekuelewa "mkuu wa chuo"
 
Sina haja ya kutaja jina langu wala kuandika maelezo mengi, lakini kwa ufupi mimi ni Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).

Kwakweli suala la kunguni UDOM limekuwa linasumbuwa na lina kera kwa muda mrefu.

Ajabu ni kuwa hakuna hatua zinazochukuliwa kwa sasa wadudu hao wamekuwa wengi sana yaani nahisi hata Ufaransa tunaposikia wamefunga vyuo hawajafikia huku, ni kero sana.

Kunguni hao wanapatikana kwenye mabweni tunapolala, mfano kwenye college ya Education ndio balaa.

Siku za nyuma uongozi wa chuo ulikuwa na kawaida ya kupuliza dawa kwenye mabweni, lakini ndani ya miaka hii miwili hali imekuwa tofauti.

Tulipofunga Chuo Juni na Julai 2023 tulitegemea tukirudi tutakuta wamepuliza dawa lakini hali imekuwa tofauti, matokeo yake watu tumeanza kulazimika kutandika na kulala chini kwani vitandani hakulaliki.

Changamoto hii sio kwenye college yetu pekee bali karibia zote Wanafunzi tumekuwa tukilalamika kunguni.
UDOM?🙆🙆🙆🙆🙆
Duh!!
Kwa hadhi ilee!
 
Back
Top Bottom