Ni shida sana kuelewa.Picha unayojaribu kuijenga hapa na pengine ndiyo iliyo ktk akili yako ni kuwa kwa wewe unajua na kuamini kwamba, kila siku ni alhamisi...
Unadhani kwamba, kwa kuwa jana ilikuwa hivi, basi na leo itakuwa hivyo hivyo. Unajidanganya..!
Mimi nakuambia hivi👇
Ilikuwa hivyo wakati huo, ilishapita hiyo...
Lakini haitakuwa hivyo kesho wala keshokutwa...
Kesho au keshokutwa itakuja na yake..
Unaweza kupenda au usipende...
Hakuna aliyewahi kudhani kuwa ipo siku Watanganyika wangekuja kuandamana na kugomea zoezi la upigaji kura katika uchaguzi mkuu unaoitishwa nchini...!!
Lakini ilitokea hivyo 29/10/2025 na CCM hawakuamini na hawaamini mpaka leo. Nawe u miongoni mwao bila shaka...!
Hakuna aliyewahi kudhani kuwa ipo siku itatokea serikali iliyochini ya CCM ingeua maelfu ya raia watoto, kinamama, kinababa, kinadada na kinakaka wasio na hatia kwa risasi za moto kama wanyama ili tu kupata madaraka ya urais, ubunge au udiwani...
Samia Suluhu Hassan na genge lake la CCM lilifanya hivyo 29/10/2025...
Sio kila siku ni alhamisi...!
Kila nyakati na majira huja na mambo yake...
Kuna wakati wa kufa na kushindwa pia...
Huu umeshaipata CCM...
Unakuja wakati wa ukiri na kuamini kwako kuwa, NI KWELI ILISEMWA..!
Mantiki ya andiko hili hasa ni nini?Kila nyakati na majira huja na mambo yake...
Kwamba wakati huu ni wa Samia na Genge lake kunyanyasa na kuua waTanzania?