Unataka kujikinga dhidi ya Wachawi au unataka Kuwaona?

Njia ingine rahisi ni kuchukua tongotongo za paka mweusi, unapaka machoni mwako halafu unaenda kwenye mizunguko yako.
Hapa njiani utawaona wanga, majini, vizuka na vigagula vyoote wanaowanga mchana na hata wale wanaopaa na ungo mchana utawaona ila wewe hawatakuona.
Ila madhara ya dawa hii ni unaweza kupata mshtuko na kuzimia au kupata lolote maana kuna majini wana sura za kutisha sana au maumbile mabaya na ya kutisha.
Kwahiyo paka anatuzidi stamina ee!?
 
Ukishawaona na wewe hakikisha unawaua hapo happy mnamalizana nao wote.

NI muhimu kuwa na panga karibu ili wakishatokea tu unamalizana nao hapo hapo
 
Sina uhakika, maana nahisi labda mshana jr atakua ameshawaandikia hili, kama ndivyo basi iunganishwe tu maana hakutakua na namna tena.

Miaka hiyo huko vijijini kulikua na masimulizi ya kila aina kuhusiana na mambo mbalimbali. Ilikua ni aina ya elimu kupitia fasihi simulizi.

Leo napenda niongelee hili:

Wachawi ni kundi watu wasumbufu ambao hupenda kufanya mambo yasiyo ya kawaida na yenye kuogofya sana. Sababu zinazopelekea watu kujiunga na makundi ya wachawi ni visasi, udhaifu, upweke, urithi/historia na wakati mwingine kulazimishwa/mateka.

Katika simulizi hizo tulipata kusimuliwa baadhi ya mbinu za kujikinga na wachawi ukiondoa zile mbinu za kiimani/DINI.
Kuna mbinu mbili ambazo tulipata kusimuliwa.

Ya kwanza tuliambiwa ili kujikinga na wachawi, chukua mkaa wa moto ambao umekolea moto pande zote na ni mwekundu hasa na uudumbukize kwenye maji. Ukiudumbukiza kwenye maji utasikia mlio 'chaaa', yaani hapo maji yanazima ule moto na moto unajaribu kuyapasha maji lakini moto ndiyo huishia kuathirika zaidi maana huzimika kabisa.

Moto ukishazimika unatakiwa kuuchukua ule mkaa na kuuweka kichwani wakati wa kulala (chini) ya mto. Hapo mchawi akikujia usiku ataishia kuona moto tu pale kitandani na wewe utalala salama kabisa bila ya kusumbuliwa. Lakini hautafanikiwa kumuona au kumjua mchawi wako.

Mbinu hii ilitumika mpaka kwenye kuvikinga vyakula, kule vijijini ilikua ni jambo la kawaida sana kukuta mtu kaanika unga kwenye mkeka ila katika unga huo unaona donge la mkaa. Hufanya hivyo hata wanapokua wameuhifadhi unga huo kwenye vikapu.

Mbinu ya pili, hii ni rahisi sana na inatisha. Mbinu hii unatakiwa kuchukua mwiko uliosongewa ugali jioni hiyo halafu wakati wa kulala unauchukua mwiko huo bila ya kuuosha na kupanda nao kitandani na kuuweka kichwani. Utakapofika muda wa wachawi kupita 'round' utawaona wote kama walivyo ila na wao watajua kuwa umewaona, hapo ndipo ilipo hatari ya mbinu hii ya pili, maana baada ya kugundua kuwa umewaona (na ni lazima wajue) watakushambulia kichawi ili kukuzuia usitoe siri hiyo na katika mashambulizi yao huwa hawakuui, bali watakufanya u-paralise mwili/viungo au akili au mdomo na utabaki kama ndondocha.

Hiyo mbinu ya kwanza tuliweza kuijaribu ila ndiyo hivyo tena...you can't tell maana hatukuona chochote kile wala haina bifu nao wala ushahidi, kuupata ushaihidi ni kama wachawi hao waliongozana na mtoto katika shughuli zao, ndiyo utasikia mtoto akisema "Usiku tulienda kumroga yule lakini pale kitandani tukakuta moto tu".
Ila hii mbinu ya pili, kwa kweli hakuwahi kutokea 'Mkwawa ' shujaa miongoni mwetu aliyethubutu kuijaribu. Maana kila tulipouliza zaidi ili kujua ukweli tukaishia kupata jibu lile lile kuwa ni HATARI na tusijaribu.

Labda mmoja ajitolee kujaribu ili atuletee mrejesho, otherwise tutaendelea kuamini hivyo.
Thread haijakamilika no research no right to speak unazungumziaje Habari Za kuweka mwiko hali ya kuwa hujawahi kujaribu Nend kaweke mwiko Kisha njoo na mrejesho
Sio unatuletea vitu nusunusu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Thread haijakamilika no research no right to speak unazungumziaje Habari Za kuweka mwiko hali ya kuwa hujawahi kujaribu Nend kaweke mwiko Kisha njoo na mrejesho
Sio unatuletea vitu nusunusu

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkisikia misemo kazi yenu ni kuirukia na kuanza kuiimba tu bila ha ya kuielewa.
unaposema "Nyo nyichechi nyo raiti chu chipiki" hivi unaelewa hata maana ya huo msemo???
Mimi nimeandika kiuwazi kabisa kuwa ni MASIMULIZI, wewe unakuja na mambo ya "nyo richechi" wapi na wapi!!!
 
Mkisikia misemo kazi yenu ni kuirukia na kuanza kuiimba tu bila ha ya kuielewa.
unaposema "Nyo nyichechi nyo raiti chu chipiki" hivi unaelewa hata maana ya huo msemo???
Mimi nimeandika kiuwazi kabisa kuwa ni MASIMULIZI, wewe unakuja na mambo ya "nyo richechi" wapi na wapi!!!
Wazungu wanatushinda vitu vichache tu wanapoona kitu ambacho hawakielewi wanakifanyia research wakiisikia Story wanaifanyia uchunguzi wanakuja na conclusion ya kila jambo dogo na kubwa ki ukweli Kuna chunguzi nyingine zimegharimu maisha ya watu watu wamekua vilema waliopoteza mali na sifa zao lakini mwishowe hawa watu tunawasoma katika vitabu kama malegendary heroes philosophers na majina mengi mazuri sasa mkuu umeleta swala zuuuuuuri kabisa nimelipenda watu wamelipenda lakini halijakamilika kukuambia ufanye uchunguzi nimekosea ?
Hapana lazima uwe shujaa mkuu consigliere.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wazungu wanatushinda vitu vichache tu wanapoona kitu ambacho hawakielewi wanakifanyia research wakiisikia Story wanaifanyia uchunguzi wanakuja na conclusion ya kila jambo dogo na kubwa ki ukweli Kuna chunguzi nyingine zimegharimu maisha ya watu watu wamekua vilema waliopoteza mali na sifa zao lakini mwishowe hawa watu tunawasoma katika vitabu kama malegendary heroes philosophers na majina mengi mazuri sasa mkuu umeleta swala zuuuuuuri kabisa nimelipenda watu wamelipenda lakini halijakamilika kukuambia ufanye uchunguzi nimekosea ?
Hapana lazima uwe shujaa mkuu consigliere.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu, hii issue kama utafuatilia vizuri huu mjadala hata mimi nimeomba watu kama wataweza basi wakajaribu halafu watuletee mrejesho. Mimi nimelileta kama Simulizi, maana yake hata mimi limenishinda kulijaribu na kuja na majibu ya kina.
Labda na mimi nikuombe ujitolee kujaribu hili😆😆
 
hii thread inachekesha sana daaah.
Mm naona hakuna kitu kibaya kitafanyika kama utakua na Imani/Nguvu
Ww amini kabisa kutoka katika uvungu wa moyo wako hakuna cha kuniweza na imani yako isitetereke hata sekunde moja, na itakua kama unavyoamini..
Haina haja ya kuviona visivyponekana..tukajitafutia stroke,vilipoumbwa visivyoonekana ujue sio vyetu havipaswi kuviona pia msijipe majukumu ambayo ubongo hautayaweza.
Mm naamini Mungu katupa nguvu zetu za asili na muongozo ila mambo mengi ya maisha yanatuzonga.
Waswahili wenzangu "Mungu hakupi kilema akakunyima mwendo"
Ndugu zangu wakristo Zaburi :125 "Wamtumaniao bwana ni kama mlima sayuni,hawatatikisika milele Daima"

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Simple_unalala na kaa la moto kama ulivyosema pia unalala na mwiko I,e unawaona na hata wao wanakuona ila wakitaka kuja kukudhuru ili usitoe siri wanakuta moto tu coz umelala na mkaa....hapo je mkuu...?
usisahau kuweka na mfupa wa nguruwe chini ya mto nao ni kinga na uvute bangi kabla ya kulala
 
Kwani Wachawi wanakula unga? shida yote ya nini hadi kuweka mkaa katikati ya unga. Mbona tangu mimi nazliwa hadi leo sijawahi kushudia hilo la mkaa na mimi binasfi sijawahi kuweka na unga nakaa nao hadi wakati mwingine unaharibika kwakikaa kwa muda mrefu.
 
Back
Top Bottom