Unasaidia wengi kujikwamua kiuchumi na wengi juu it’s majina tofauti, wengine wanaita mchezo, upatikanaji, kibati..

Sky Eclat

JF-Expert Member
Oct 17, 2012
57,595
215,272
Faida yake kubwa ni kuwa haina riba, tofauti na mkopo wa benki. Unafundisha nidhamu ya kuweka pesa. Ni watu wengi wanaucheza katika viwango tofauti.

Kuna wapika maandazi na vitumbua, au wenye biashara ndogo ndogo, huwekeana kiasi cha kukusanya kila siku, wengi hukusanya faida ya siku. Hii inakusaidia kutokula faida, wengine wanachanga 1,000 kila siku, kuna wanaochanga 10,000 hata 100.000.

Nineongea na watu wa tabaka tofauti na wengi wamenifahamisha wanafahamu kibati. Wengi huwasaidia kujenga nyumba, kununua gari, kubadilisha furniture za ndani hata kununua ticket za kuwapeleka watoto kuwasalimia bibi na babu kijijini.
 
Faida yake kubwa ni kuwa haina riba, tofauti na mkopo wa benki. Unafundisha nidhamu ya kuweka pesa. Ni watu wengi wanaucheza katika viwango tofauti.

Kuna wapika maandazi na vitumbua, au wenye biashara ndogo ndogo, huwekeana kuasi cha kukusanya kila siku, wengi hukusanya faida ya siku. Hii inakusaidia kutokula faida, wengine wanachanga 1,000 kila siku, kuna wanaochanga 10,000 hata 100.000.

Nineongea na watu wa tabaka tofauti na wengi wamenifahamisha wanafahamu kibati. Wengi huwasaidia kujenga nyumba, kununua gari, kubadilisha furniture za ndani hata kununua ticket za kuwapeleka watoto kuwasalimia bibi na babu kijijini.
Vijumbe wanakuaga na majaribu sana

Huku uswazi mchezo/kibati hauwezi kuisha bila mtifuano.
 
mimi hiyo ya kijumbe kushika hela ndo sitaki kabisa kila mtu apokeee hela zake
Mimi michezo inanishinda hapo kwenye kushikiana hela. Kijumbe sometimes huwa anajikopesha humo humo kwenye hela zenu Sasa siku ya kupokea mtu ndio longolongo inaanzia hapo.
Ukiwa mtu wa mwishoni kupokea ndio kabisaa.

Inahitaji nidhamu Sana na watu wanaojielewa nini wanafanya. Wengine wanatoboa na hii michezo wanapata mitaji, wanapata kodi n.k
 
Mimi michezo inanishinda hapo kwenye kushikiana hela. Kijumbe sometimes huwa anajikopesha humo humo kwenye hela zenu Sasa siku ya kupokea mtu ndio longolongo inaanzia hapo.
Ukiwa mtu wa mwishoni kupokea ndio kabisaa.

Inahitaji nidhamu Sana na watu wanaojielewa nini wanafanya. Wengine wanatoboa na hii michezo wanapata mitaji, wanapata kodi n.k

Yeah mi nina wa laki mbili kwa mwezi, laki moja kwa mwezi, elf mbili kila siku na elf 10 kila wiki yote hatushikiani kila mtu anapokea yake siku yake ikifika
 
Ewaaa ikifika zamu ya muhusika anaweka namba ukitula unasema jina unatikiwa fresh
Tumeweka rules kwenye group yetu, anaechelewa kufikisha anakuwa exposed kwenye group na anamlipa mpokeaji double. Maximum tarehe 30 mpokeaji anatakiwa awe amepokea pesa yake.
 
Ndugu yangu kacheza mchezo huo kanunua alphard inamsaidia biashara yake ya kupika chakula.

Ila tukumbuke uu mchezo ndo chachu ya watoto kulishwa matembele magumu makavu na madagaa ya hovyo ili mama apeleke pesa kwa kijumbe, usiku sababu baba yupo ananunua nyama robo.
 
Back
Top Bottom