Unajua kama raia una wajibu kwenye ulinzi wa uhuru, mamlaka na umoja wa Taifa? Timiza nafasi yako

Unajua kama raia una wajibu kwenye ulinzi wa uhuru, mamlaka na umoja wa Taifa? Timiza nafasi yako

Joined
Sep 17, 2024
Posts
26
Reaction score
28
Wewe kama raia una wajibu wa kuhakikisha unadumisha uhuru,amani na umoja katika nafasi mbalimbali ili kuimarisha huduma za kijamii na kiuchumi.

Kama raia unatakiwa kudumisha uhuru,amani,umoja na kulinda rasilimali za nchi

Ikiwa raia hatalinda hatotekeleza wajibu huo basi anaweza kushtakiwa kwa mujibu wa Sheria ya Utekelezaji wa Haki na Wajibu wa Msingi (Basic Rights and Duties Enforcement Act).
 
Nyie tume ningewashauri mpiganie kwanza mabadiliko ya sheria yenu muwe na uwezo wa kushtaki mamlaka pale haki zinapokiukwa.
Kwa mfano hivi watu wanavyotekwa na kupotezwa mngetakiwa muwe na uwezo wa kisheria kumpeleka IGP Mahakamani ili kuwajibishwa kwa makosa hayo.
Kwa kifupi mpiganie mpewe meno kama pccb muwe mnapeleka watu mahakamani wanaohusika na ukiukwaji wa haki za binadamu.
Kwa mlivyo sasa mmekuwa tume jina , hamna mamlaka yeyote ya kumbana mtu hata kumfunga mtu kama takukuru.
Nyie mmekuwa tume ya kutoa matamko tu ambayo hayana tija sana kwenye jamii.
Kama hilo halitawezekana ni kheri mfutwe tu kwani mnatumia hovyo fedha za umma au kwa maneno mengine matumizi ya bajeti yenu ni matumizi yasiyokuwa na tija kwa wananchi na taifa kwa jumla
 
Wewe kama raia una wajibu wa kuhakikisha unadumisha uhuru,amani na umoja katika nafasi mbalimbali ili kuimarisha huduma za kijamii na kiuchumi.

Kama raia unatakiwa kudumisha uhuru,amani,umoja na kulinda rasilimali za nchi

Ikiwa raia hatalinda hatotekeleza wajibu huo basi anaweza kushtakiwa kwa mujibu wa Sheria ya Utekelezaji wa Haki na Wajibu wa Msingi (Basic Rights and Duties Enforcement Act).
No reform no election.
 
Back
Top Bottom