Unahitaji kuwa Afisa Usalama? Give it a try

Unahitaji kuwa Afisa Usalama? Give it a try

Aisee , lengo lako nini?! Unataka watu waache kuonyesha uzalendo kwa nchi yao, kisa wanaweza kuwa asset? Wakati huo unasisitiza kuwa asset ni kuishi 'kwa wasiwasi '!?

Mimi, mkuu usinitishe, nitaendelea kuwa mzalendo kwa nchi yangu Tanzania kwa uwazi bila woga.
======
Mkuu isome post yangu hii kwa taratibu utaelewa vizuri wapi pa kurekebisha kwenye post namba moja ya uzi huu. Vinginevyo, uzi "una kwenda na muda "
Eeeh,,,,,sawa noted
 
Hao washawasha ni police au???

Wapo watu wanapata kazi za kula viapo vya kutunza siri ni lazima wawe wanausalama kabla ya kuchukua majukumu yao? Au kamati kama ya bunge ya ulinzi na usslama mbunge raia tu wa kawaida anaingia humo?

Na washawasha!
 
hii ni kazi isiyo na shukrani hata kidogo kwahiyo kama mtu unawaza kuingia huko ili uingie kwenye vitabu vya kumbukumbu kwa mchango wako kwa taifa inabidi usahau.. ni kazi ambayo unapoteza kila kitu ili wananchi wengine wengi waishi kwa amani na furaha na hao hao ndo watakua wa kwanza kukusimanga jambo dogo linapoenda ndivyo sivyo. ni kama mdau mmoja hapa anaamini kumtolea bastola nape ndo kazi pekee wanayofanya usalama wa taifa!!.. ni wangapi wapo tayari kutoa michango hata ya maisha yao ila isitambuliwe wala kujulikana na watu wanaowasaidia?! kazi ambayo tokea unaianza unajua kabisa sponsor hatokupa msaada wowote, atakukana (plausible deniability) na utakua tayari kufa kuliko kuweka wazi uhusiano wako nae siku utakapoangukia kwenye mikono ya adui!! una infiltrate kikundi cha majambazi sugu wanaofanya organized crime, unaua nao watu, unafanya nao matukio ili wasikushtukie, unajua kabisa wakikushtukia tu ndo umeenda na maji na upo tayari.. acheni utani bana
Mkuu bora wakuue aisseh kuliko wakupake mafuta
 
Upande wa pili wa shilingi ya asset ni liability ni lini afisa anakuwa liability? Si alichukuliwa kuruta kama asset.

Je mtu au kitu gani kinakuwa asset ya kufuatiliwa nyendo zake?

Pale kitu au mtu anapotumiwa bila kujijua si inakuwa dhuluma maana kwa mfano mnatumia akili ya mtu kutimiza malengo yenu bila kumpa ujira hata bila kumjulisha. Ukiangalia kama huyu marehemu Ngosha (rip) akili na ubunifu wake katika uchoraji umetumiwa, nembo inaendelea kutumika yeye kafa maaskini kaambulia jeneza tu la maana na mazishi ya heshima.

Na washawasha!
 
Nina plan ya kuja kuvamia na kuua wana usalama wilaya fulani hii imekaaje?? Am not serious kiasi hicho aisee
 
Nahitaji kuwa kwani nafikiri naweza tena napenda sana kushiiriki katika ujenzi wa taifa letu nikiwa na nafasi yangu kama msomi wa ngazi wa uzamivu na ninayetembelea mataifa mbalimbali. Najihusisha na sayansi ya asili na huku kwa kweli kunahitaji usalama na uzalendo sana kwani watanzania wengi ikiwa ni pamoja na viongozi wa taifa hudanganywa na watu wasio wazalendo kuhusu mambo ya maslahi ya taifa. Tafadhali nijulishe nifanye nini niweze kutoa mchango wangu kupitia usalama wa taifa. 0686997270
Namba ya nn ungemtumia inbox
 
Kitu chochote chenye usiri huongeza hamasa ya watu kukijua ama hata kuwa aehemu ya hiyo jamii.Lakini kiukweli hakuna lolote la maana..watu wanatamani kuwa miongoni mwa jamii ya freemason,usalama nk.Lakini hamna kitu.Kuna jamaa yangu alikuwa usalama na ameacha.Hakuna la maana,tafuteni pesa,acheni illusion..
 
ndugu,so unataka na wewe uwe mng'oa kucha na meno bila ganzi huku ukiminya ikulu za watu,omba upate kazi itakayokusogeza na huruma na upendo kwa jamii na sio kazi za kujutia uliyoyafanya kwa kusudi au kutokusudia​
 
Fazil,

Binafsi sina uwezo wa kufanya connection yoyote huko (wewe na Usalama)

Lakini naamimi wahusika wapo humu na kama wanaona inafaa
basi watakutafuta kwa hiyo namba yako...

Lakini kuwa makini na matapeli.!!

Daah MAGAZIJUTO kweli mweee
 
Mkuu The bold umegusa point nyingi muhimu, asante sana kwa dondoo muhimu.

Naomba kuuliza kwa wadau mbali mbali hili jambo:
  • Je, Hivi hawa jamaa wakimuita mtu kwenye usaili wao (akafanya written na oral interview) yao, halafu wakamwambia muhusika watamuita ila unapita muda mrefu ukapita (Karibu 2yrs) na mawasiliano(simu ,postal adress,makazi ya muhusika,) na wakaja kumfatilia hadi kitaa muhusika kisha wakapotea ghafla, Je ina maanisha Nini?? Je bado wana muhitaji au ndo anakuwa haja kidhi vigezo??
  • Je wale referee anaowajaza muhusika wanaweza kuwa kigezo cha kufanya muhusika asije qualified to be recruited na hao jamaa..?
 
Back
Top Bottom