hii ni kazi isiyo na shukrani hata kidogo kwahiyo kama mtu unawaza kuingia huko ili uingie kwenye vitabu vya kumbukumbu kwa mchango wako kwa taifa inabidi usahau.. ni kazi ambayo unapoteza kila kitu ili wananchi wengine wengi waishi kwa amani na furaha na hao hao ndo watakua wa kwanza kukusimanga jambo dogo linapoenda ndivyo sivyo. ni kama mdau mmoja hapa anaamini kumtolea bastola nape ndo kazi pekee wanayofanya usalama wa taifa!!.. ni wangapi wapo tayari kutoa michango hata ya maisha yao ila isitambuliwe wala kujulikana na watu wanaowasaidia?! kazi ambayo tokea unaianza unajua kabisa sponsor hatokupa msaada wowote, atakukana (plausible deniability) na utakua tayari kufa kuliko kuweka wazi uhusiano wako nae siku utakapoangukia kwenye mikono ya adui!! una infiltrate kikundi cha majambazi sugu wanaofanya organized crime, unaua nao watu, unafanya nao matukio ili wasikushtukie, unajua kabisa wakikushtukia tu ndo umeenda na maji na upo tayari.. acheni utani bana