Marekani ni mbabe na mjeuri.
Ukiangalia vita alivyovisha na alivyo shindwa ukiachalia mbali uwezo wake mkubwa kijeshi.
Vita alivyo shindwa ni vingi.Sijui hype yote hii kuhusu Marekani inatokana na nini.!?!?
Mtazamo wangu juu ya hili.
Marekani anatakiwa atambue Iran sio Waarabu wale ni Wa-Persia wajukuu wa wafalme Darius na Xerxes.
Wale hawana unafiki wa kiarabu na hata wakiwa na mgogoro linapokuja suala la kutetea nchi yao wanakua kitu kimoja.
Marekani anajeshi kubwa la maji na anga lakini Iran anauzoefu wa vita. Kapigana ardhini, angani kapigana na vita ya majini anaijua vizuri. Hapa kwenye vita ya majini ndio tatizo linapo anza kwa mmarekani.
Iran wana sub-marine nyingi kiidadi zinakaribiana na alizo nazo mmarekani. Mtu yeyote anajua vita vizuri atakuambia kupigana na adui mwenye nyambizi ni hatari sana.
Marekani anajivunia vita haiwezi pelekwa kwake lakini uhalisia Iran anauwezo wa kupeleka vita USA na akapiga maeneo na miji muhimu maana vitendea kazi anavyo.
Nyambizi inauwezo wa kusafiri bila kuonekana na kufanya mashambulizi ya kushtukiza wakiwa karibu na nchi ya marekani.
Hivyo USA asidharau mwiba Iran haitakua rahisi kama anavyojipa moyo. Alipigwa Vietnam, Afaghnstan, Iraq ya kwanza, Iraq ya pili mpaka leo inamsumbua, Syria inamsumbua mpaka leo,Korea ilisha kwa stalemate, Somalia alipigwa hivyo ajiangalie.
Iran ni mkubwa kuliko wote hao. Mbaya zaidi Pakistani ndugu katika imani wa Iran ambaye anamiliki silaha na technology ya nuclear anamuunga mkono ndugu yake.
Trump acheze chess yake vizuri maana pawns nao wameshtuka hawata kubali waende kichwa kichwa meanwhile Pawns wa Iran ni reliable akina Taleban, Hezbollah etc.
Yote kwa yote kila mtu anajua namna ya kuanzisha vita, namna inavyoisha ndio haijulikani.