UNAFIKI unatawala Bavicha...

UNAFIKI unatawala Bavicha...

Status
Not open for further replies.
nasikitika kuchangia uzi huu , maana kiongozi wetu wa juu kabisa ameufunga rasmi , asanteni na kwaherini .

Kwa lugha nyepesi ni kwamba Slaa amekushikia akili na ana mamlaka ya kukuamulia nini uongee na nini usiongee. Wewe ni mlaghaika...
 
onyo - chadema aihujumiki ! Kama umechukua hela ya watu rudisha ! Vinginevyo utaadhirika vibaya sana !

Hahahahahahahahaha

Tatizo lenu mmeshazoea kuwa hamfanyi kitu mpaka mlipwe pesa.

Ndio maana Slaa alisema hagombei Urais mpaka ahakikishiwe mshahara wa mamilioni baada ya kushindwa kwa sababu alijua kabisa kuwa atashindwa...
 
Mwanaume anayeamua kujipa jina la kike ni lazima awe na matatizo kichwani. Mungu kamuumba mwanaume yeye anaona Mungu amekosea!!!

Huyo matola amewatukana sana waislamu humu ndani halafu anataka kugombea ubunge sas sijui anaenda kuwaomba kura watu wa iman yake tu? Alivyoona tunaamua nguo kaja kivingine.
 
Kuna unafiki Tanzania kama huu, "Ari mpya, nguvu mpya na kasi mpya" "Maisha bora kwa kila Mtanzania yanawezekana" "Tumethubutu tumeweza na sasa tunasonga mbele" kwi kwi kwi kwi MACCM banaa mapumbavu kweli!!!! LoL!!!!


Kaka,

Hivi Ludovick ndio mmeshamchinjia baharini?
 
Huyo matola amewatukana sana waislamu humu ndani halafu anataka kugombea ubunge sas sijui anaenda kuwaomba kura watu wa iman yake tu? Alivyoona tunaamua nguo kaja kivingine.

Laani huwa inakuja kwa namna mbalimbali...
 
Huyo matola amewatukana sana waislamu humu ndani halafu anataka kugombea ubunge sas sijui anaenda kuwaomba kura watu wa iman yake tu? Alivyoona tunaamua nguo kaja kivingine.

si wamezoea kufanyia kampeni zao kanisani? Atapewa kura na wakristo wenzake, kuna mwingine anaitwa tayadi ni mbaguzi mdini na mhafidhina wa kutosha
 
-Sijawahi kuwasiliana na naibu mkurugenzi wa TISS

-Sijawahi kushiriki kuuza majimbo yetu ya uchaguzi

-Sijawahi kushirikiana na Naibu Katibu Mkuu CCM kumhujumu Lwakatare kwenye sakata la ugaidi fake n.k

"Mida Eight anatumiwa na Dr. Slaa kugombanisha viongozi" - waraka

Ndicho ulichoshiriki hicho. Au unakataa?
 
Ni mipango ya Mungu,sisi kuzaliwa kanda nyingine,angetaka wote tungezaliwa ya kaskazini,Kwa nini munatubagua????
 
Unajua kiswahili?

umeambiwa lete ushahidi usio na shaka,


Mods simamieni huyu ndugu ahakikishe analeta ushahidi alioamriwa na bwana Ben aulete ndani ya masaa matatu.

Wewe umeshaleta ushahidi?

Sasa hivi huna lugha nyingine ispokuwa; ushahidi, mahakama, mtuhumiwa. Unalo!

Hata "mida eight" ni "bwana" kwako? makubwa haya! amma kweli Waswahili wamenena "mtumwa hasadifiki".
 
Wewe umeshaleta ushahidi?

Sasa hivi huna lugha nyingine ispokuwa; ushahidi, mahakama, mtuhumiwa. Unalo!

Hata "mida eight" ni "bwana" kwako? makubwa haya! amma kweli Waswahili wamenena "mtumwa hasadifiki".

Yericko anafuta sympathy tu. Hana mpya.
 
Dr Slaa amesema suala la zitto na CDM limefugwa sasa tuongelee suala la rasilimali zetu kama gesi, Umeme kupanda, hali mbaya ya maisha na wizi wa mali , wabakaji kama yle mbunge wa huko Tabora. kwahiyo tusubiri siku 14 tusikilizie maamuzi magumu ya CC
Wewe endelee kukipigia chapuo hilo lichama, mwenzio Mtoi tushampoteza kwenye anga hizi za siasa..
 
Last edited by a moderator:
WanaJF,

Nimetoa majibu yangu katika Thread aliyoanzisha mtu anayejiita Zemarcopolo.Pamoja na kuwaomba Moderators wapandishe majibu yangu katika thread ile,sijaona response yoyote nami nimeamua kuchukua hatua maana Moderators niliwaandikia Inbox kabisa lakini hadi page ya 7 hakuna response.Zemarcopolo ameandika:

Chadema ni chama kinachoendeshwa katika misingi ya kilaghai.

Miezi kadhaa iliyopita jumuiya ya vijana ya Chadema, Bavicha, ilitangaza kumvua uongozi na kumfukuza uanachama aliyekuwa makamu mwenyekiti wa jumuiya hiyo Bi. Juliana Shonza. Kosa lake lilitangazwa kuwa ni "usaliti".

Aliyefichua "usaliti" huo ni Ben Saanane a.k.a Mida Eight ambaye alielezwa kuwa alipewa kazi maalum ya kuspy vijana wenzake.

Katika katiba na kanuni za chama HAKUNA kazi hii ya uspy aliyopewa Ben Saanane.

Vijana wengi wa bavicha hasa hapa JF walimpongeza Ben Saanane na kumuona shujaa. Mpaka leo uspy huo alioufanya Ben Saanane ndio jambo pekee linalomfanya aonekane insider wa Chadema.

Mkakati wa siri wa kumpa Ben Saanane kazi ya kuspy ndani ya chama haukuhusisha vikao halali vya chama. Ndio maana viongozi wakuu wa Chama na wajumbe wa Kamati Kuu hawakuwa na taarifa yoyote juu ya kazi hii ya Ben Saanane. Hii ilikuwa ni kazi binafsi ya Dr. Slaa. Ben Saanane alikiri kwenye kikao halali cha Bavicha kuwa alifanya kazi ya uspy na kikao hicho kikampongeza kwa kazi nzuri!

Ni UNAFIKI wa hali ya juu kuona vijana waliounga mkono uwepo wa mikakati ya siri ya Dr. Slaa kumtumia Ben Saanane wakipinga mwanazuoni Dr. Kitila Mkumbo kuwa na mikakati ya siri.

Je, kuna mtu mwenye hati miliki ya mikakati ya siri ndani ya Chadema?

Jumuiya ya vijana katika chama chochote ndio nguzo na dira ya chama. Unafiki huu unaotawala Bavicha unadhihirisha kuwa Chadema sasa haina dira na nguyo yake imeliwa na mchwa.




XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX

MAJIBU YANGU

XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX

ZeMarcopolo na WanaJF,

Mosi,Hakuna mahali popote iwe kwenye vikao au mahali pengine nilipowahi kutamka haya yaliyoandikwa hapa.Labda mleta mada alete ushahidi hapa.JF ikiwa mleta mada hataleta ushahidi wa haya ikiwa ni pamoja na minutes za vikao achukuliwe hatua kwa kusema uongo.Nampa masaa 3 .

Pili,Tamko langu kuhusu PM-7 lipo huku.

Tatu,Kama nilipongezwa kwa kiwango anachodai mleta mada hapa sasa iweje nipewe adhabu ya kusimamishwa kugombea nafasi yoyote kwa muda wa mwaka 1 sambamba na onyo kali

Nashukuru Mungu uchaguzi haukufanyika mwaka huu kama ilivyopangwa maana ningekosa haki ya kuchaguliwa.Mipango ya Mungu si kama mipango yetu wanadamu


Nne,Naomba niweke hili very clear.Sijawahi kuwa au kutumiwa na Dr.Slaa au kiongozi yeyote wa CHADEMA kwa maslahi binafsi.

Hizi ni hoja mufilisi na visingizio vya washirika wangu wa Zamani katika mkakati haramu waliokasirishwa na kitendo changu cha kusimamia maslahi ya chama na kuwaanika hadharani baada ya mimi binafsi kufanya kazi kubwa ya kuwasihi waache mpango huo maana wangekivuruga chama


Kwa muda wa takribani siku 345 hadi leo hii wamekua wakinishambulia na kunitukana lakini mwisho wa siku walikiri kupanga njama chafu.Ukweli siku zote husimama juu ya unafiki,usaliti na njama ovu za kuuficha ukweli.Kilichotokea Alhamisi iliyopita ni Matokeo ya jitihada za ukweli uliofanikiwa kulipa kisasi baada ya kupuuzwa kwa muda mrefu

Tano,WANACHADEMA,Wapendamabadiliko na watanzania kwa ujumla nawaahidi kuendeleza mapambano na wale wote wanaozuia harakati za mabadiliko ndani na nje ya chama chetu

Nitaendelea kusimamia misingi ya chama chetu na taifa bila kuchoka hadi tone langu la mwisho la damu.Namuomba mwenyezi Mungu anipe nguvu na ujasiri katika mapambano haya.Tuwapuuze wale wote wanaojaribu kututoa katika mstari wa mapambano.

Katika harakati hizi za mabadiliko na malengo ya CHADEMA kitaasisi katika kuongoza vuguvugu hili Doctrine yangu ni 'It's either you are with us or against us'.Hakuna middleground hata kama dunia ni three dimension.Kipimo nitakachompimia msaliti yeyote wa mabadiliko haya ndani ya chama hakitakua na tofauti na kile nitakachotumia dhidi ya wapinzani na maadui wa mabadiliko nje ya chama.

CC: Invisible, Fang, Buchanan, Paw, PainKiller Moderator
 
Last edited by a moderator:
zemarcopolo yuko kwenye mission na kwa sababu madola yale yaliyotoka NMB kwenda ujerumani na kurudi Tanzania hayajaisha ze marcopolo yupo mpaka October 2015 watakapozabwa za uso
 
Mkuu ZeMarcopolo tena umewapaisha sana. Bavicha haina hadhi ya kuanzishiwa uzi na mtu maarufu kama wewe in short bavicha is too low, sio saiz yako.

Habari njema:
Usiwe na wasiwasi, Zitto hakuna wa kumg'oa chadema. I said hapa kuwa hii vita ni laini sana. Nakuhakikishia tayari tumeshinda. Habari zitawajieni.
 
Last edited by a moderator:
Usingehangaika kujibizana na wahuni kina LUKOSI mwenye jukumu la kumuogesha ajuzi pale london.Maccm hao ndio wamekula rambirambi ya MWANGOSI.
 
Mkuu ZeMarcopolo tena umewapaisha sana. Bavicha haina hadhi ya kuanzishiwa uzi na mtu maarufu kama wewe in short bavicha is too low, sio saiz yako.

Habari njema:
Usiwe na wasiwasi, Zitto hakuna wa kumg'oa chadema. I said hapa kuwa hii vita ni laini sana. Nakuhakikishia tayari tumeshinda. Habari zitawajieni.

Mkuu,

Nakusoma. Hawa vijana wamethibitisha kuwa hawana principles maishani.

Tuendelee kuwa pamoja...
 
Last edited by a moderator:
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom