Black Opal
Senior Member
- Jan 22, 2023
- 199
- 253
Wakuu katika vitu vinanifanya nisile nyama au samaki za kuunga ni vile unavyokaanga halafu mafuta yanakurukia. Yaani unakuwa unapika sura umeweka Magharibi mkono unaogeuza mboga kwenye mafuta uko mashariki.
Mimi huwa napaka unga wa ngano, lakini wakati mwingine huwa sitaki kupata ladha na muonekano ule wa unga wa ngano.
Je, kuna njia nyingine ya kukaanga samaki au nyama bila kurukiwa mafuta? Wewe unatumia njia gani?
Naombeni ujuzi wenu wadau.