Utaratibu wa Kumhudumia Mama baada ya Kuzaa

figganigga

JF-Expert Member
Oct 17, 2010
25,492
54,895

5. Utaratibu wa Kumhudumia Mama baada ya Kuzaa​

Kipindi cha 5 Utaratibu wa Kumhudumia Mama baada ya kuzaa​

Utangulizi​

Huduma baada ya kuzaa kwa mama inapaswa kukabiliana na mahitaji yake maalum, kuanzia saa moja baada ya kutoka kwa kondo na kuendelea kuwepo kwa wiki sita zinazofuata. Huduma hii ni pamoja na uzuiaji, kugundua mapema na kutibu matatizo, na utoaji wa ushauri kuhusu unyonyeshaji, upangaji uzazi, chanjo, na lishe bora wakati wa ujauzito. Ili kufanya huduma baada ya kuzaa kwa mama iwe ya kawaida, unashauriwa kutumia uchunguzi, ushauri na kadi za kurekodi huduma baada ya kuzaa. Hizi kadi huhakikisha kwamba umepitia hatua zote muhimu katika kila ziara ya nyumbani.
Katika Kipindi hiki cha somo, tutaangazia hasa kwa kimsingi utaratibu wa uchunguzi unayohitaji kufanya ili kuhakikisha kwamba mama anapata nafuu baada ya kuzaa, kimwili na kihisia. Tutakushauri pia jinsi unapaswa kumpa mawaidha juu ya kutunza afya yake na kupata nafuu, kudumisha usafi wa mwili wake ili kupunguza hatari ya maambukizi, na kile anachopaswa kula - hasa anaponyonyesha.

Malengo ya Somo la Kipindi cha 5​

Baada ya Kipindi hiki, unafaa kuwa na uwezo wa:
5.1 Kufafanua na kutumia kwa ufasaha maneno yote muhimu yaliyochapishwa kwa herufi nzito.(Maswali ya Kujitathmini 5.1 na 5.2)
5.2 Kuelezea vipimo vya mwili unavyopaswa kufanya kwa mama aliyezaa baada ya kuzalisha, na katika ziara inayofuatia baadaye, ili kuhakikisha kwamba anapata nafuu vizuri. (Swali la Kujitathmini 5.2)
5.3 Kueleza jinsi utamshauri mama kuhusu lishe bora katika kipindi baada ya kuzaa na ni virutubishi vidogo gani za nyongeza ungempa. (Swali la Kujitathmini 5.2)
5.4 Kuelezea aina za usaidizi utakazompa mama baada ya kuzaa ambayo ungemshawishi mpenzi wake na familia yake kumpa, ikiwa ni pamoja na kutafuta huduma ya mara moja iwapo watagundua kuwepo kwa dalili za hatari. (Swali la Kujitathmini 5.2)

5.1 Kiini cha utaratibu wa huduma kwa mama baada ya kuzaa​

Huduma zinazotolewa mara kwa mara kwa mama wakati wa kipindi baada ya kuzaa hasa zinajumuisha hatua za kuzuia zinazolenga kutambua mapema visababishi vya kawaida vya maradhi kwa kina mama na vifo katika jamii vijijini. Wakati wa kila ziara, baada ya kuzaa, hakikisha kuwa unafanya shughuli zifuatazo za kawaida, hata wakati mama halalamiki kuhusu chochote.

5.1.1 Chunguza ishara muhimu kwa mama​

Ulijifunza jinsi ya kuchunguza ishara muhimu katika Kipindi cha 9 cha Moduli ya Utunzaji katika Ujauzito.
Chunguza ishara muhimu kwa mama, yaani, joto lake, kiwango cha mpigo kwa mshipa, na shinikizo la damu, na kuhakikisha kwamba ziko katika kiwango cha kawaida. Mara tu baada ya kuzaliwa, chunguza mipigo yake kwa mshipa na shinikizo la damu angalau mara moja kila saa, na joto lake angalau mara moja katika saa sita za kwanza.
  • Je, ishara muhimu za kawaida zinapaswa kuwa aje ikiwa mama anaendelea kupata nafuu vizuri tangu wakati wa kuzalisha?
    Reveal answer
stop_sign.jpg
Mpatie mama rufaa ya haraka ambaye anaonyesha dalili ya mshtuko na/au kutokwa na damu baada ya mtoto kuzaliwa.
Ikiwa shinikizo la damu yake iko chini mno na inashuka, na mipigo ya mshipa yake inaenda haraka na inaongezeka, anaelekea kuwa na mshtuko. Huenda kinasababishwa na utokaji wa damu wa kuhatarisha maisha. Kama hakuna dalili ya kutokwa na damu kutoka ukeni, anaweza kuwa anapoteza damu ndani ya mwili.

5.1.2 Chunguza kama uterasi yake ina mikazo ya kawaida​

Gusa (hisi) fumbatio lake kupima mikazo ya uterasi ili kuhakikisha kwamba iko imara. Mara tu baada ya kuzaa, unapaswa kuwa na uwezo wa kuhisi mikazo karibu na kitovu cha mama, na kuteremka chini katika pelvisi yake kwa mwendo wa kasi zaidi kwa wiki mbili zijazo. Chunguza uterasi yake kila baada ya dakika 15 kwa ya masaa mawili ya kwanza baada ya kuzaa na kila dakika 30 kwa saa ya tatu. Ikiwezekana, chunguza kila saa kwa saa tatu zifuatazo. Iwapo uterasi iko ngumu, iwache wakati wa vipimo. Ikiwa utahisi ikiwa laini, sugua fumbatio juu ya uterasi ili uisaidie iwe na mikazo. Mfunze mama kujifanyia hivi (Mchoro 5.1).

View larger image
Mchoro 5.1 Uterasi inaweza kusaidiwa kupata mikazo baada ya mama kuzaa kwa kusugua fumbatio.
Dawa ulizompa mama (kwa mfano, misoprostol au oxytocin) kusaidia kutoa plasenta na kuzuia kuvuja damu pia itasaidia uterasi kupata mikazo. Kwa hivyo hunyonyesha mtoto wake. Mama pia anaweza kuwa na haja ya kukojoa ikiwa kibofu chake cha mkojo kimejaa, kinachosaidia uterasi kujikaza vizuri. Chunguza mikazo ya uterasi katika ziara zote baada ya kipindi cha kuzalisha.

5.1.3 Safisha tumbo ya mama, viungo vya uzazi na miguu​

pnc_session5_fig2.jpg

Mchoro 5.2 Kuosha eneo la viungo vya uzazi vya mama ni mojawapo ya huduma ya kimsingi baada ya kipindi cha kuzaa katika ziara ya kwanza.
Msaidie mama kujisafisha baada ya kuzaa. Badilisha matandiko yoyote yale chafu na usafishe damu iliyo mwilini mwake. Nawa mikono kwanza na uvae glavu kila mara kabla ya kugusa viungo vya uzazi vya mama, kama ulivyofanya kabla kuzalisha. Hii itamlinda kutokana na bakteria yoyote ambayo inaweza kuwa kwa mikono yako. Safisha viungo vya uzazi vyake kwa utaratibu, kwa kutumia sabuni na maji safi sana na kitambaa safi (Mchoro 5.2). Usitumie kemikali ya kuua viini vya maradhi yoyote ambayo inaweza kuwasha tishu zake zilizonyororo. Osha kuelekea chini, mbali na uke. Kuwa mwangalifu ili usipeleke chochote kutoka mkundu kuelekea ukeni. Hata kipande kidogo cha kinyesi kisichoonekana kinaweza kusababisha maambukizi.

5.1.4 Chunguza uvujaji wa damu nyingi (hemoreji)​

Baada ya kuzalisha, ni kawaida kwa mwanamke kutokwa na damu kiasi sawa na ya hedhi. Damu lazima pia ionekane kama ile ya hedhi - utusitusi, au waridi. Mara ya kwanza, damu hutoka katika mbubujiko mdogo au kumwagika wakati uterasi inakazika, au wakati mama atakapokohoa, kusonga, au kusimama. Baada ya siku mbili hadi tatu, mtiririko unapaswa kupungua na kuwa mchozo mwekundu ulio majimaji zaidi inayojulikana kama lokia (Kipindi cha 2).
Kutokwa na damu nyingi sana ni hatari. Ili kuchunguza utokaji wa damu nyingi katika saa sita za kwanza baada ya kuzalisha, chunguza pedii ya mama mara kwa mara – milimita 500 (karibu vikombe viwili) ya kupoteza damu ni nyingi mno. Ikiwa atalowesha pedii moja kwa saa, inachukuliwa kama kutokwa na damu nyingi. Ikiwa mama anatokwa na damu nyingi, na hauwezi kuizuia, mpeleke hospitalini. Chunguza kwa ishara za mshtuko. Kumbuka kwamba kutokwa na damu baada ya kuzaa ni kisababishi kikubwa cha vifo vya wajawazito na kinaweza kutokea wakati wowote katika kipindi cha huduma baada ya kuzaa - ingawa ni ya kawaida katika siku saba za kwanza.

5.1.5 Chunguza viungo vya uzazi vya mama iwapo kuna miraruko na matatizo mengine​

pnc_session-5_fig3.jpg

Mchoro 5.3 Fungua vulva kwa utaratibu kuchunguza viungo vya uzazi kwa ishara za jeraha.
Tumia mkono ulio na glavu kwa utaratibu kuchunguza viungo vya uzazi vya mama (Mchoro 5.3) kwa miraruko, vibonge vya damu, au hematoma (kutokwa na damu ndani ya ngozi). Ikiwa mwanamke ana mraruko unaohitaji kushonwa, weka shinikizo juu yake kwa dakika 10 kwa kutumia kitambaa safi au pedi na kumrufaa kwa kituo cha afya. Ikiwa mraruko ni mdogo, pengine unaweza kupona bila kushonwa, bora tu iwe imetunzwa kwa safi ili kuzuia maambukizi katika jeraha.
Mweleze apumzike iwezekanavyo na umwambie kuwa hapaswi kupanda juu au kushuka milima yaliyowima. Mtu mwingine anapaswa kufanya kazi za kifamilia za kupika na kusafisha kwa siku chache. Ili apate nafuu haraka, anapaswa pia kula vyakula vingi vyenyewe afya, kuweka sehemu ya viungo vya uzazi viwe safi (kuosha na maji baada ya kutumia choo) na kufunika kwa kitambaa au pedi safi.

Kuvuja damu ndani ya ngozi (hematoma) au maumivu ukeni​

Wakati mwingine uterasi hukazika na kuwa ngumu na utokaji wa damu huwa ni kiasi, Ilhali mama bado anahisi kizunguzungu na mdhaifu. Iwapo hii itatokea, anaweza kuwa anatokwa na damu chini ya ngozi ukeni mwake ambapo huitwa hematoma (Kielelezo 5.4). Ngozi katika eneo hili mara nyingi huvimba, huwa na rangi ya utusitusi, nyepesi kwa kudhurika, na nyororo.
pnc_session-5_fig4.jpg

Mchoro 5.4 Hematoma ni mkusanyiko wa damu ndani ya ngozi katika eneo la viungo vya uzazi vilivyo na uchungu.

Seviksi iliyochomoza​

pnc_session-5_fig5.jpg

Mchoro 5.5 Seviksi iliyochomoza inaweza kuonekana kwa ufunguzi wa uke.
Chunguza kama seviksi imechomoza (imeshuka chini kwa ufunguzi wa uke; Mchoro 5.5). Tatizo hili si hatari, na seviksi kwa kawaida hurudi ndani baada ya siku chache. Msaidie mama kuinua nyonga ili iwe juu kuliko kichwa chake. Mwambie afanye mazoezi ya kukaza misuli ya uke na kuta za pelvisi angalau mara nne kwa siku.
Ikiwa seviksi itabaki katika ufunguzi wa uke zaidi ya wiki mbili, anapaswa kupewa rufaa. Seviksi ambayo itakaa ikiwa imechomoza inaweza kutatiza iwapo mama atapata mtoto mwingine

5.1.6 Msaidie mama kukojoa​

pnc_session-5_fig6.jpg

Mchoro 5.6 Mama anaweza kuchuchumaa kwa bakuli ili akojoe ikiwa ni rahisi kwake.
Kibofu cha mkojo kiliojaa kinaweza kusababisha uvujaji wa damu na matatizo mengine. Kibofu cha mkojo kinaweza kuwa kimejaa baada ya kuzaa, lakini anaweza kuwa hana hamu ya kukojoa. Mwambie akojoe katika saa mbili au tatu za kwanza. Ikiwa amechoka sana kwa kuamka na kutembea, anaweza kuchuchumaa kwa bakuli kitandani au sakafuni (Mchoro 5.6). Anaweza pia kukojoa kwa taulo au kitambaa nene wakati amelala chini. Ikiwa hawezi kukojoa, unaweza kumsaidia kwa kumwagia maji safi, iliyo na joto kwa viungo vya uzazi wakati anapojaribu kukojoa.
Ikiwa mama hawezi kukojoa baada ya saa nne, na kibofu chake cha mkojo hakijajaa, anaweza kuwa na upungufu wa maji mwilini. Msaidie anywe viowevu. Ikiwa kibofu chake kimejaa na bado hawezi kukojoa, lazima aingizwe katheta ili kutoa mkojo ulio kwa kibofu cha mkojo wake. Ikiwa umepata mafunzo ya kufanya hivi, tumia katheta kama ilivyoonyeshwa katika Kipindi cha 22 cha Moduli ya Utunzaji katika Ujauzito na masomo yako ya ujuzi tendaji. Kisha mpatie rufaa kwa kituo cha afya au hospitali kilicho karibu.
  • Je, ni jambo gani muhimu unapaswa kufanya kabla ya kumpima mama ambaye amezaa wakati huo?
    Reveal answer

5.2 Lishe baada ya kuzaa​

5.2.1 Kukula na kunywa katika masaa machache za kwanza​

pnc_session5_fig7.jpg

Mchoro 5.7 Mshawishi ale mara tu, ndani ya masaa machache za kwanza, na anywe viowevu mara kwa mara.
Kina mama wengi huwa tayari kula mara baada ya kuzaliwa, na ni vizuri kwao kula aina yoyote ya lishe bora wanataka. Ikiwa mama ambaye anazaa mara ya kwanza hahisi njaa, angalau anapaswa kuwa na kitu cha kula. Maji ya matunda au chai atmit ni nzuri kwa sababu itawapa nguvu (Mchoro 5.7). Wanawake wengi hutaka kunywa kitu kilicho na joto, kama chai. Baadhi ya maji ya matunda, kama maji ya machungwa, pia huwa na vitamini C, ambayo inaweza kumsaidia kupata nafuu. (Lakini anapaswa kujiepusha na soda kama Coke, ambayo ina sukari nyingi na kemikali lakini haina lishe.)
Iwapo mama hawezi (au hataweza) kula au kunywa ndani ya saa tatu baada ya kuzaa:
  • Anaweza kuwa mgonjwa. Chunguza kama anavuja damu, joto jingi mwilini, shida ya haipatensheni, au ishara zingine za magonjwa ambazo zinamtoa hamu ya kula.
  • Anaweza kuwa na huzuni (anasikitika, hasira, au bila hisia zozote). Mshawishi aongee kuhusu hisia zake na mahitaji yake. Moyo wake kwa majadiliano juu ya hisia zake na mahitaji. (Baada ya kuzaliwa kwa mtoto 'hali ya kuwa na huzuni' ilielezwa katika Kipindi cha 3.)
  • Anaweza kuamini kwamba baadhi ya vyakula ni vibaya kula baada ya kuzaa. Mweleze kwa upole kwamba lazima ale ili apate nafuu kutokana na kuzalisha na kupata uwezo wa kumpa mtoto wake huduma bora.

5.2.2 Ushauri juu ya lishe baada ya kuzaa​

Baada ya kuzaa, ulaji wa mara kwa mara inapaswa kuongezwa ili kurudisha nguvu ya kunyonyesha pamoja na nguvu na afya yake. Anapaswa kula takriban 10% zaidi kuliko kabla awe mjamzito ikiwa hana shughuli nyingi au anafanya kazi yake ya kawaida na takriban 20% zaidi kama yuko na uwezo. Katika hali halisi, anashauriwa kuchukua angalau mlo mmoja au miwili zaidi kila siku. Ushauri wa lishe bora ni pamoja na:
Familia nyingi vijijini hawana uwezo wa kununua chakula cha ziada kwa kina mama ambao wamezaa kwa mara ya kwanza. Kipindi cha 14 katika Moduli ya Utunzaji katika ujauzito kinatoa ushauri kuhusu kula vizuri kwa kutumia pesa kidogo
  • Kushauri mama kula baadhi ya vyakula vilivyo na protini, nishati ya juu (kama vile familia inaweza kumudu), kama vile nyama, maziwa, samaki, mafuta, karanga, mbegu, nafaka, maharagwe na jibini, ili awe na afya pamoja na nguvu. Ushauri wako wa lishe bora itategemea na kile kilichoko nyumbani na kile wanakula kama chakula chao kikuu. Kile muhimu zaidi ni kuwaambia kwamba lazima ale zaidi kuliko kawaida.
  • Kuchunguza iwapo kuna miiko za kitamaduni ambazo ni muhimu kuhusu kula vyakula ambavyo ni lishe bora zaidi kiafya. Kwa mfano, katika baadhi ya tamaduni kula vyakula vilivyo na protini nyingi huchukuliwa vibaya, vyakula vilivyotiwa viungo, au vyakula baridi baada ya kuzaa. Mshauri kwa heshima dhidi ya miiko haya na hayapaswi kujizuia na chakula chochote chenye lishe bora.
  • Kuzungumza na wanafamilia, hasa mpenzi na/au mama mkwe, na kuwahimiza wasaidie kuhakikisha kwamba mwanamke anakula vyakula vya aina mbalimbali vya kutosha na kujiepusha na kazi ngumu ya kimwili.
Mshauri mama kuchukua virutubishi vidogo kuongeza lishe mara kwa mara ili kuzuia matatizo ya upungufu na anemia, kama tutakavyoeleza.

5.2.3 Kuzuia upungufu wa iodini​

pnc_session-5_fig8.jpg

Mchoro 5.8 Tezi ni uvimbe ulio mbele ya shingo, unaosababishwa na upanuzi wa glandi ya thiroidi.
Kuongeza madini ya iodini kwa chumvi huitwa iodination na inapendekezwa utumie chumvi iliyo na iodini kwa upishi katika kipindi baada ya kuzaa, hasa katika maeneo ya nchi ambazo tezi ni ya kawaida kama matokeo ya madini ya iodini kidogo sana katika mlo (Mchoro 5.8). Uongezaji wa madini ya iodini kwa chumvi imeonekana kuwa njia yenye ufanisi mno ya kuzuia upungufu wa iodini. Kutumia mafuta yenye iodini kwa njia ya kunywa au kudungwa sindano inaweza kutumika kama hatua ya muda mfupi katika maeneo endemiki ambapo ni vigumu kupatikana kwa chumvi iliyo na iodini. Mshawishi mama atumie chumvi iliyo na iodini kila siku wakati wa kipindi baada ya kuzaa, kama inapatikana. Hata hivyo, kama tezi inapatikana hapo, mama anaweza kupewa dosi ya mafuta iliyo na iodini baada tu ya kuzaa.

5.2.4 Kuzuia upungufu wa vitamini A​

Mshauri mama jinsi ya kuzuia upungufu wa vitamini A, ambayo si tishio tu kwa kuona kwake, lakini pia ni kisababishi kikubwa cha upofu utotoni mwa watoto walionyonyeswa na mama aliye na upungufu wa vitamini A. Vitamini A katika mlo huongezea kinga dhidi ya maambukizi na ni muhimu hasa kwa utengenezaji wa maziwa ya mama yaliyo na virutubishi.
  • Mshauri mama jinsi ya kuzuia upungufu wa vitamini A, ambayo si tishio tu kwa kuona kwake, lakini pia ni kisababishi kikubwa cha upofu utotoni mwa watoto walionyonyeswa na mama aliye na upungufu wa vitamini A. Vitamini A katika mlo huongezea kinga dhidi ya maambukizi na ni muhimu hasa kwa utengenezaji wa maziwa ya mama yaliyo na virutubishi.
    Reveal answer
Kumbuka kwamba kipimo cha upeo wa vitamini A kwa wajawazito ni IU 500,000; zaidi ya hapo ni sumu
Mojawapo ya huduma ya kawaida baada ya kuzaa ni kuchunguza kama mama amepata kapsuli ya vitamini A. Kipimo kilichopendekezwa kwa kina mama wanaonyonyesha ni kapsuli moja ya vitamini A, IU 200,000 mara moja baada ya kuzaa au ndani ya wiki sita baada ya kuzaa. Mweleze kwamba vitamini A humsaidia kupata nafuu vizuri na mtoto anapata kupitia maziwa yake. Mweleze iwapo anahisi kichefuchefu au ana maumivu ya kichwa baada ya kutumia kapsuli hii, itaacha baada ya siku kadhaa.

5.2.5 Kuzuia upungufu wa ioni na folate​

Upungufu wa damu kutoka mwanzo inaweza kuchochewa na madhara ya kuvuja damu kwa mama na ni moja ya kisababishi kikubwa cha vifo vya wajawazito katika kipindi baada ya kuzaa. Shawishi kina mama kula vyakula vilivyo na madini ya ioni (kwa mfano, mboga zilizo na rangi ya kijani kibichi, maharagwe, mbaazi na dengu, kuku na nyama nyekundu, nyama ya ogani kama vile ini na figo, na bidhaa za nafaka nzima), na vyakula ambavyo huongeza ufyonzaji wa ioni (matunda na mboga zilizo na vitamini C). Mshauri kukunywa tembe moja iliyo na miligramu 60 ya ioni na mikrogramu 400 cha folate (folic acid) kila siku kwa muda wa miezi mitatu baada ya kuzaa, na umpatie kiasi kinachotosha kwa miezi mitatu. (Baadhi ya maeneo yanaweza kuwa na tembe zilizo na ioni na folate zikiwa mbalimbali, lakini kipimo ni sawa.) Mshauri kuhifadhi tembe salama pahali ambapo watoto hawawezi kupata kwa urahisi.
  • Huduma bora ya kawaida baada ya kuzaa kwa mama ni pamoja na kumshauri kuhusu mahitaji yake ya lishe. Je, utamshauri kuhusu nini?
    Reveal answer

5.3 Usaidizi wa kihisia kwa mama​

Baada ya kuwasili katika nyumba, jambo la kwanza unahitaji kuhakikisha ni kwamba mama na mtoto hawajatengwa na wanafamilia wengine kwa sababu za kitamaduni. Unaweza kuwa ulitatua tatizo hili wakati wa mazungumzo ya awali na wanafamilia, lakini kila unapomtembelea hakikisha kwamba mama ana usaidizi anayohitaji kutoka kwa jamii na kuwa wanafamilia wanamtembelea mara kwa mara. Ukiwa pamoja na viongozi wa jamii, unapaswa kujaribu kukomesha mazoea ya kutenganisha, kwa kumweka mama aliyezaa na mtoto wake kado na jamii, ikiwa bado hili linatekelezwa katika jamii yako. Badala yake, mshauri mama kuwa kila siku awe karibu na mtu kwa masaa 24 ya kwanza. Washauri wanafamilia kuwasiliana mara kwa mara kila siku wakati wa wiki ya kwanza ili kuchukua hatua haraka iwapo ishara zozote hatari zitatokea katika hali yake.

5.3.1 Kina baba na wanafamilia wengine wanaweza kumsaidia​

pnc_session-5_fig10.jpg

Mchoro 5.9 Kina baba wanaweza kumtunza mtoto mchanga wakati mama anapumzika.
Mshawishi mwenzake kuwa karibu na mama angalau kwa wiki ya kwanza katika kipindi baada ya kuzaa ili ampatie usaidizi wa kihisia na kumtunza yeye na mtoto (Mchoro 5.9). Katika mazingira ya Afrika, utunzaji wa mama kawaida ni wajibu wa nyanya na/au mama mkwe. Kwa vile tayari wamepitia haya, wako katika hali bora wa kumpatia usaidizi wa kimwili na kihisia kwa mama na mtoto wake. Wanaweza kumwondoa kutoka shughuli za nyumbani za kawaida, ambayo inahitaji kuhamashishwa.

5.3.2 Wakati mama hana haja na mtoto wake​

Baadhi ya kina mama hawahisi vizuri kuhusu watoto wachanga (Mchoro 5.10). Kunaweza kuwa na sababu nyingi kwa hii. Mama anaweza kuwa amechoka sana, au ni mgonjwa au anatokwa na damu. Anaweza kuwa hakutaka mtoto, au kuwa na wasiwasi kwamba hawezi kumtunza. Kama ulivyojifunza katika Kipindi cha 3 cha Somo, anaweza kuwa anafadhaika sana: ishara kama hizi ni kama mama anaonekana kuwa na huzuni, utulivu, na hana hamu ya kitu chochote. Pia chunguza ishara zingine za tabia isiyo kuwa ya kawaida ambayo ni tofauti na ile yake ya kawaida.
pnc_session-5_fig11.jpg

Mchoro 5.10 Mama ambaye anakataa mtoto wake anaweza kuwa na masumbuko baada ya kuzaa.
La kufanya iwapo unajishughulisha na mama kukosa haja na mtoto wake:
  • Mchunguze kwa makini kwa ishara za uvujaji wa damu au maambukizi, au ugonjwa wa shinikisho la damu. Anaweza kuwa mgonjwa, badala ya kufadhaika au wasiwasi.
  • Unaweza kuzungumza na mama kuhusu hisia zake, au huhisi kuwa ni bora kuangalia na kusubiri.
  • Ikiwa unajua kwamba alikuwa amefadhaika sana baada ya kuzaa hapo awali, washauri wanafamilia kumtunza na kumsaidia zaidi kwa wiki chache zijazo. Kawaida mfadhaiko huu huisha, lakini wakati mwingine inachukua muda wa wiki chache au hata miezi, na inaweza kuhitaji rufaa kwa utathmini na matibabu zaidi. Kama anaonyesha dalili zozote za kichaa baada ya kuzaa (Kisanduku 5.1), mpee rufaa haraka.
  • Hakikisha kwamba mtu katika familia anamtunza mchanga iwapo mama hawezi au hataweza.
stop_sign.jpg
Kichaa baada ya kuzaa kinaweza kutisha maisha, hivyo ichukue kama hali ya dharura. Utajifunza zaidi kuhusu kichaa katika Moduli juu ya Magonjwa yasiyo kuwa ya Kuambukiza, Huduma za Dharura, na Afya ya Akili.

Kisanduku 5.1 Dalili za kichaa baada ya kuzaa​

Hali hii ni nadra (inayoathiri takribani mmoja kati ya wanawake 1,000), lakini ni kali sana na mama lazima apewe rufaa kwa haraka kwa matibabu maalamu kama anaonyesha dalili yoyote kati ya zifuatazo:
  • Kusikia sauti au mlio wakati hakuna mtu pale
  • Kuona mambo ambayo si ya kweli
  • Kuhisi kama mawazo yake si yake mwenyewe
  • Kuhisi uoga kuwa anaweza kujidhuru au mtoto wake
  • Kupoteza uzito kwa ghafula na kukataa kula
  • Kukosa usingizi kwa masaa 48 au zaidi.

5.4 Kuhimiza mazoea utafutaji wa huduma​

Mhimize mama, mwenzake, na wanafamilia wengine kupata huduma mara moja wakiona dalili yoyote hatari, ikiwa ni kwa hali yake ya kimwili au hisia. Ucheleweshaji ndio sababu kuu ya vifo vya kina mama na wachanga muda tu baada ya kuzaa na ni pamoja na:
  • Kuchelewa kutambua mapema na kufanya uamuzi wa kupata usaidizi, kutokana na imani potofu na miiko ya kitamaduni. Familia pia zinaweza kuwa na ogopa gharama kufuatia huduma za afya.
  • Kuchelewa kupata huduma ya usafiri hadi kituo cha afya, au kupata mhudumu wa afya wa kwenda naye nyumbani kwa mama.
  • Kuchelewa kupata huduma mwafaka anapofika katika kituo cha afya, kutokana na ukosefu wa wahudumu au vifaa.
Kuwapa motisha mama na familia juu ya kutafuta huduma mapema ndio msingi katika utoaji wa huduma mwafaka baada ya kuzaa. Unapaswa kujaribu kuweka uwezo kwa jamii wa kukabiliana na hali yoyote ya dharura ambayo inaweza kutokea wakati wa kipindi baada ya kuzaa. Hasa, lazima tahadhari itolewe katika kila kijiji kwa kubuni mfumo wa rufaa wa dharura kwa kina mama na wachanga walio kwa hali inayohatarisha maisha.

Muhtasari wa Kipindi cha 5​

Katika Kipindi cha 5, umejifunza kwamba:
  1. Lengo la huduma kwa kina mama baada ya kuzaa ni kwa utambuzi wa mapema wa ishara hatari za jumla kwa njia ya uchunguzi wa mara kwa mara wa hali ya joto, mpigo kwa mshipa wa mama, na shinikizo la damu, uchunguzi wa kimwili kwa mkazo wa uterasi, kutokwa na damu, uharibifu wa sehemu za siri, maambukizi au matatizo ya shinikizo la damu, ikifuatiwa na rufaa ya haraka.
  2. Huduma muhimu unayopaswa kumpatia mama baada ya kuzaa ni pamoja na kumpima ishara muhimu kila anapotembelea kliniki, kumwosha sehemu za siri na kuchunguza iwapo kumepasuka, damu kuganda, kuchomoka kwa seviksi, na kutokwa na damu, kumsaidia kukojoa, kula na kunywa, na kumpa nyongeza ya kirutubishi kidogo(vitamini A, ioni, na folic acid).
  3. Kumshauri mama, mwenzake, na wanafamilia wengine wakati wa kipindi baada ya kuzaa inalenga kuwawezesha kutambua dalili hatari za jumla na kutafuta huduma mwafaka kwa haraka, kuboresha lishe yake ili kusaidia kunyonyesha na kupona, na kumpa usaidizi wa kihisia na wa maisha ya kila siku.
  4. Kutenga kina mama na watoto katika kipindi baada ya kuzaa si bora kwa afya ya kimawazo ya mama na inaweza kumweka mama katika hatari ya kutelekezwa au kuhisi ametengwa na kufadhaika. Dalili hatari zinaweza pia kukosa kutabulika iwapo hakuna aliye naye.

Maswali ya Kujitathmini ya Kipindi cha 5​

Sasa kwa kuwa umekamilisha Kipindi hiki cha somo, unaweza kutathmini mafanikio ya matokeo ya kujifunza kwa kujibu maswali yafuatayo. Andika majibu yako katika Shajara yako ya somo na uyajadili na na mkufunzi wako katika mkutano ujao wa Usaidizi kwa Somo. Unaweza kulinganisha majibu yako na Maelezo juu ya Maswali ya Kujitathmini yaliyo mwishoni wa Moduli hii.

Swali la Kujitathmini 5.1 (linatathmini Malengo ya Somo la 5.1 na 5.2)​

Uliwasili kama umechelewa kuzalisha mtoto ambaye alizaliwa masaa mawili kabla ya wewe kufika huko. Utafanya nini?
Reveal answer

Swali la Kujitathmini 5.2 (linatathmini Malengo ya Somo la 5.1, 5.3 na 5.4)​

Lishe bora na usaidizi kwa mama baada ya kuzaa ni masuala muhimu ya huduma bora baada ya kuzaa. Kamilisha Jedwali 5.1 ilikuonyesha, kila tatizo katika safu ya kwanza:
  • Unayotumaini mama au familia yake watafanya.
  • Utakalofanya ili kuhakikisha kwamba mama ana kila anachohitaji.
Jedwali 5.1 Huduma na usaidizi kwa kina mama wapya.
Tatizo au uwezekano walo iwapo halitashugulikiwaHatua mama au familia yake inaweza kuchukua ili kumsaidiaMatibabu au hatua zingine unaweza kuchukua
Tezi (inayosababishwa na upungufu wa madini ya iodini)
Kutokula au kunywa katika masaa machache ya kwanza
Ukosefu wa nguvu(kudumisha nguvu wakati wa kunyonyesha)
Upungufu wa vitamini A
Anaemia
Utengwaji wa mama na mtoto
Kutokuwa na hamu na mtoto
Usaidizi kwa mama

◄ 5. Utaratibu wa Kumhudumia Mama baada ya Kuzaa
Unless otherwise stated, copyright © 2023 The Open University, all rights reserved.
 

Answer​

Jedwali 5.1 Utunzaji na usaidizi kwa kina mama wapya (iliyokamilishwa).
Tatizo au uwezekano wa tatizoHatua mama au familia yake wanaweza kuchukua ili kumsaidiaMatibabu au hatua zingine unazoweza kuchukua
Tezi (inayosababishwa na upungufu wa madini ya iodini)Matumizi ya chumvi iliyowekwa iodini kwa kupikiaDozi ya mafuta iliyo wekwa iodini baada ya kuzaa, kama tezi inapatikana kwa urahisi.
Kutokula au kunywa katika masaa machache ya kwanzaMama anapaswa kujaribu na kukumbuka kwamba ni lazima anywe na ale kwa ajili ya afya yake na ya mtoto.Chunguza kama kuan utokaji wa damu, homa, au ishara zingine za ugonjwa ambazo zinaweza kuwa ndio kiini cha tatizo; mshawishi mama kuzungumza kuhusu vile anajihisi.
Ukosefu wa nguvu(kudumisha nguvu wakati wa kunyonyesha)Kula mara moja au mbili zaidi kwa siku vyakula vyenye protini vingi (nyama, maziwa, mafuta, karanga, na kadhalika) kama inawezekana.Chunguza kama kuna miiko kuhusu vyakula, zungumza na familia juu ya kuhakikisha mama anakula chakula cha kutosha na kuepukana na kazi ngumu.
Upungufu wa vitamini AOngezea ulaji wa vitamini A nyingi, mboga na matunda, kwa mfano, karoti, maembe, kabichi, mchicha; pia ule ini, mafuta ya ini ya samaki, maziwa, mayai, na siagi.Mpatie kapsuli moja ya vitamini A iliyo na IU 200,000 baada ya kuzaa au ndani ya wiki sita za kuzaa; elezea umuhimu wa vyakula vyenye vitamini A.
AnaemiaOngezea ulaji wa mboga na matunda yenye ioni na folate.Mpatie tembe za kutosha (miligramu 60 ioni na mikrogramu 400 folate) ameze moja kila siku kwa miezi mitatu
Utengwaji wa mama na mtoto.Wanafamilia kukaa na mama na mchanga kutoa ili kuwapa usaidizi, licha ya kanuni za kiutamaduni.Eleza ni kwa nini mama anahitaji mtu kukaa karibu naye, hasa katika siku saba ya kwanza, wakati kuna hatari kubwa; huduma ya haraka inahitajika iwapo chochote kibaya kitatokezea.
Kutokuwa na hamu na mtotoFamilia imtunze na imsaidie zaidi na kuwe na mtu wa kuhudumia mchanga kama kuna haja.Chunguza kuwepo kwa ugonjwa, kuvuja damu au maambukizi. Zungumza naye. Chunguza kama anasikia sauti, au ‘kuona vitu’. Kama ni hivyo mwelekeze kwa daktari wa akili kwa usaidizi.
Usaidizi kwa mamaMwenzake, nyanya na/au mama mkwe wachukue baadhi ya kazi za nyumbani za kawaida.Hakikisha kwamba mwenzake na familia wanajua dalili hatari na umuhimu wa kutochelewa kumpeleka mama kwenye kituo cha afya.
Mwisho wa jibu
 
Back
Top Bottom