JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,308
- 5,460
Ametoa wito kwa Watanzania kuendelea kujitokeza kupata Chanjo ya UVIKO-19, hasa watu walio katika hatari zaidi ya kupata ugonjwa huo kama vile wenye magonjwa sugu (Shinikizo la damu, kisukari, magonjwa, saratani, UKIMWI n.k) na wazee.
Amebainisha kuwa Serikali kupitia Wizara ya Afya imelenga kufikia asilimia 70 ya watu waliochanja ikiwa ni sehemu ya mkakati wa Dunia wa kupambana dhidi ya ugonjwa wa UVIKO-19.
Ameyasema hayo wakati akiwa na Waziri wa TAMISEMI na Mwakilishi kutoka Wizara ya fedha katika Mkutano na Katibu Mkuu Msaidizi na Mratibu Mkuu wa Kimataifa wa mapambano dhidi ya UVIKO-19 kutoka Umoja wa Mataifa Dkt. Ted Chaiban aliyeambatana na wajumbe kutoka WHO na UNICEF.
Ameongeza kuwa mpaka kufikia Aprili 5, 2022 tayari watu milioni 8.5 wameshapatiwa Chanjo ya kupambana dhidi ya ugonjwa wa UVIKO-19 na kuweka wazi kuwa, bado kuna kazi kubwa ya kufanya ili kuweza kuchanja watu waliobaki ili kuweza kuishi na ugonjwa huo kama magonjwa mengine.
Source: Voice of Bongo