Umeshawahi kuletewa nyodo na mhudumu wa kike?

Wadau kwa hii sijui aliyekuwa na dharau ni yupi.. Nikiwa mkoa wa Arusha nafanya biashara mwaka 2015/2016 nilikuwa na hizi mashine za betting za kampuni Premier na huwa mauzo yao yanatumwa kwa m-pesa kwanda namba yao ya kampuni. Siku moja nikatuma mida ya saa nne nikaendelea na kazi zangu. Sasa hii kampuni ilikuwa kama hujatuma mauzo yao mashine inafungwa. Basi mida ya saa kumi jioni nashangaa mashine imefungwa. Kucheki salio la m-pesa pesa imetoka ukiwapigia Premier wanasema sijatuma na kweli sms haijarudi ila hela imekatwa.
Basi nikawapigia Voda wanasema kweli nimetuma hela na wanaiona ipo hewani nivumulie baada ya masaa 72 (kama sijakosea) itafeli itarudi kwangu. Nikaamua kutafuta hela nyingine nikalipa kwa namba nyingine ili biashara iendelee.
Kesho yake mida ya asubuh nikapita vodashop moja ipo karibu na clock Tower Arusha. Nikaeleza tatizo langu kwa wahudumu wakaona hawaliwezi wakanipeleka kwa meneja wao pale jina limenitoka. Akanipokea vizuri na akaona tatizo langu na akasema hela anaiona ila anaomba nije kesho yake. Kesho yake nikaenda asubuhi hayupo naambiwa nije saa nane, sikuweza kurudi nikakaa siku mbili tena nikarudi nikamkuta akadai alikuwa nauguliwa na mtoto so hakuweza kutatua shida yangu ila nije kesho atakuwa amekamilisha.
Ikumbukwe Wakati naenda vodashop pia nilikuwa napiga simu customer care majibu yao ni mepesi tuu hela ipo hewani itarudi kwako. Lini itarudi hawana jibu na kili nikiwapigia nilikuwa nawarecord. Na pia nikishamaliza kuongea nao walikuwa wanatuma sms inatosema tatizo lako limepewa id ****** utajulishwa likikamilika. Na mimi nikawa natunza kama ushahidi.
Nimerudi kwa meneja wa hapo vodashop sound ni zile zile nikachoka. Basi niakona niende vodashop nyingine ya pale karibu na metro pole hapo hapo Arusha. Huyu alisema lipo nje ya uwezo wake niende vodashop kubwa ba kubwa ndio iyo hapo clock tower.
Nikaona hii hela ishapotea sina cha kufanya. Basi nilikuwa na mshakaji wangu ndio ametoka chuo kusomea sheria nikamwelezea akaniambia waandikie demand letter wape siku saba kama hela haijurudi kafungue kesi mahakamani.
Nikaona huu ushauri ni wa kuzidi kupoteza muda nawezaje kupambana na kampuni kubwa kama vodacom? Baadae nikasema potelea pote ngoja na mimi nikajionee nini kitatokea huko mbeleni kweli nikaandika demand letter nikapeleka pale branch ya clock tower naambiwa hakuna wa kupokea labda nipeleke pale karibu na metro pole. Nakapeleka akasema hilo lipo nje ya uwezo wake nipeleke pale pale nikarudi nikaambiwa nilete kesho yake nitamkuta meneja. Kesho yake nikapeleka kweli nikamkuta na ananikumbuka vzr tuu. Akasema siku mbili tuu jambo langu litakuwa tayari.
Nilikaa jumla ya siku 33 sijawahi kuona hela ikirudi wala kupigiwa simu na voda kuhusu hela yangu. Basi kama kawaida rafkiyangu akaniongoza kwenda kufungua kesi mahakamani. Hapa kuna utaalam mwingi kidogo kuhusu hizi kesi za namna hii. Basi nikafuta ushauri wake nikafungua kesi nikapewa na samansi (Summons) niipeleke voda.
Hapa ndio nilianza kuona nguvu ya Mahakama. Basi meneja wa kwanza kakimbia hataki kupokea, meneja wa pili nae nduki hataki hata kuskia hicho kitu. Basi tukashauriana niipeleke ofisi ya kanda ya vodacom ipo pale summit center karibu na kilombero. Kufika pale nilikutana na secretary wa meneja wa kanda wakuu ukiskia dharau ndio nilikutana nazo ana kwa ana. Akaniuliza unaapointment na meneja nakumbuka hadi jina la meneja alikuwa anaitwa Hendrish. Nikamjibu hapana nimeleta Summons inatakiwa nikabidhi na isainiwe. Akanijibu peleka makao makuu Dar yapo pale mlimani City hapa hatupokei na kwani hujui mtandao unaweza kukwama mda wowote na maneno kibao ya shombo.
Nilikuwa na uyo mshkaji wangu akajibu kwa upole tuu dada kwani tumeleta kesi kwako au tumesema tunataka kuonana na meneja wa kanda? Akajibu kwa dharau yupo busy na kama huna appointment naye huwezi kuonana nae.
Mshakaji akamjibu hizi dharau zako hazina mda mrefu sana, sisi tutaweka hii summons hapo posta wala sio hela nyingi ifike isifike matajua wenyewe sisi tutaenda na ushaidi wa resit ya ems mahakami kwa hiyo wala hujatukomoa.
Kumbe wakati tunazozana pale meneja alikuwa anaskia akamwambia secretary waambie waje ndio kuingia kwa meneja na kueleza a-z ya tukio zima. Basi meneja wa kanda alikuwa mstaarabu sana kwa kweli 👏👏👏. Basi akapokea summons akasaini kaomba nirudi kesho yake tuzungumze na secretary akaambiwa asija akanizuia tena siku yoyote nitakayofika ofisini kuonana na meneja wa kipindi icho Mr Hendry.
Baada ya kutoka hapo ofisini nikaenda kwenye biashara yangu kuendelea na shughuli zangu baada ya masaa mawili nikaona sms ya mpesa muamala umerudi iyonilikuwa kama siku ya 36 hivi.
Nilipoenda kesho yake kwa meneja akaomba iyo kesi niifute maana kama ningekuja mapema kwake yasingefika huku. Mshakji wangu akasema kama wanataka wafute walipe fidia ya hasara tuliyopata shilingi milioni mbili. Hapa nilibaki hoi maana mshakaji nasema hadi hela tulizotumia kula hotelini mjini wanatakiwa kulipa maana tilikula tukiwa tunafatilia kesi.
Hendry akasema hiyo hela hawezi kuilipa basi watakuja kwenye kesi. Siku moja kabla ya kesi nikaanza kupokea simu nyingi sana za wanasheria wa vodacom wakitaka tunegotiate msimamo ukabaki milioni mbili wakasema wanatia laki mbili nikakataa. Wakanitishia sana tuu ila nilikuwa nimelishwa maneno na mshakji kuwa waambie mahakama itaamua na itakachoamua mahakama nitakubaliana nacho hata kama ni elfu moja.
Basi kweli majibu yangu yalikuwa na nguvu usiku wake kesho kesi wakanipigia tena wakaanza kunibembeleza nichukue hata milioni moja tuondoe kesi mahakamani. Nikawaambia mwisho kabisa milioni moja na laki mbili kama hawataki kesho tukutane mahakamani.
Kesho yake kweli akaja hadi mahakamani wakataka tuondoe kesi wamekubali kulipa icho kiasi. Basi hakimu anamuiliza mmekutana na kiboko yenu ee akamjibu hakimu hio hela kidogo sana kwa kampuni kama vodacom. Ee bana ee hakimu akawa mbogo ghafla akasema haya njoo hapa andika madai ya milioni 8 achana na hizo kidogo. Jamaa aliomba sana kwa ile dharau aliyoonyesha pale kwa hakimu. Badae wakamaliza kinamna. Basi na mimi nikajaza form flani hivi kule voda inayoonyesha kesi imeisha na nimeridhika na makubaliano tuliyoyafikia.
Nikakaa kama mwezi nikapokea hela yangu nikampa mshakaji nusu na mimi nikala nusu.
*****×**************×*********
Mtanisamehe kama sijaandika vizuri.
safi sana uliwakomesha mbwa wale
 
Na wewe palikuwa na haja gani ya kusema ulipita na crown? Okee ilikuwa ni C. Athlete, Royal Saloon au Majesta?

giphy.gif
 
Nyie mnaolalamika kutupiwa bahasha kwenye dustbin sielewi wenzangu hizo guts wanazipata wapi?

Mimi uwa nasahau kupandisha, tena kama MD, AD hawapo ndio kabisa nasahau. Siku nikija kumbuka kwamba droo fulani ina barua za watu zishapita siku za kutosha tu.
Watu Kama nyie acha nikuite mbinafsi unaroho mbaya sana inakuaje unasahau majukumu yako tambua hapo ulipo sio kwa sababu yako upo kwa ajili ya watu na ipo siku utaondoka hapo
 
Watu Kama nyie acha nikuite mbinafsi unaroho mbaya sana inakuaje unasahau majukumu yako tambua hapo ulipo sio kwa sababu yako upo kwa ajili ya watu na ipo siku utaondoka hapo
Hujaelewa.

Pia waweza ita utakavyo. Ni juu yako.

MF. Umeleta bahasha yako napokea inapotakiwa kufika wenyewe hawapo. Inanibidi niweke kwa droo, mambo mengi mtu unajikuta umesahau utakuja ona wakati mwingine. ..

Usahaulifu upo, najua unajua.

Kitu kingine msichokijua, Inapopelekwa kwa HR, MD, AD ye HAISOMIIIII anakwambia tu file sehemu husika. Imeisha hiyooo. Kukiwa na uhitaji wa watu flani ndio file inafunguliwa na barua zasomwa kutafuta nani kakidhi vigezo.

Ushauri. Mnapopeleka bahasha omba kumuona mwenyewe muhusika., me kams wahusika wapo uwa napanda kuwaambia kuna mgeni wako. Siku nyingine ye tu anakwambia sina appointment na mtu, sihitaji mgeni yeyote. Kwahiyo wakija inabidi tu uwaambia muhusika hayupo.
 
Salaam wakuu! Kama kichwa cha uzi kinavyojieleza, katika mihangaiko yako ya maisha ya kila siku, umewahi kwenda sehemu kupata huduma fulani na ukaletewa nyodo na mhudumu husika, kwa sababu tu aidha mmiliki ni mpenzi wake, au vyovyote?

Karibuni!
Mi nilimtukana nikasepa
 
Muhudumu mmoja toroka uje kimara aliniletea nyodo, nilifika zangu pale mida kama ya saa kumi jioni, nikaenda kukaa hatua kama tatu na alipokuwa amesimama, nilikuwa nimechafuka balaa huku nimevaa ndala na kaptula. nilipita pale nipate bia za baradiii ndo niende home nikijua kwa nilivyochoka na ni juma pili nikifika home lazima nilale.

Binti hakuja kunihudumia, nikamuita hakuja na ananiangalia macho makavu, akapita muhudumu mwingine nikamwita akanihuhudumia, nikapiga windhoek zangu tano nikawa nimetosheka, wakati huo aliyenihudumia na yule kilaza mpya wakawa counter nikaenda pale pale, yule muhudumu akaniambia nadaiwa 15,000 nikatoa wekundu wawili nikampa nakumuambia chenji utakunywa maji, yaani yule kilaza aliyenifanyia nyodo alishtuka mpaka macho yakatanuka hakuamini kuona makusudi niliyomfanyia.

baada ya siku kadhaa, nikaenda kez pub, jumapili kucheki mechi mchana kama saa nane, nikakaa zangu counter, kufika mida ya saa kumi mechi ikaisha wadau wakapungua, mara kaja muhudumu mkali sana ananisalimia huku anajichekesha, maaambo!!!! mi nikamjibu short tu huku nashangaa huyu vipi mbona ananishobokea, kakomaa "inamaana umenisahau" mimi no, samahani sikumbuki tumeonanana wapi.

ikibidi anaieleze namna tulivyokutana toroka uje, na yaliyojiri, lakini hakusema juu ya keep change ya 5,000. nikamkumbuka, sasa kwa namna alivyokuwa mkali ikabidi nimchangamkie fasta na kumkaribisha hoo mimi hapa ndo sebureni kwangu, karibu sana na nini na nini, ghafla tu nikasikia yule dada wa counter anasema "hey hey hey nyie mnapitiliza sasa" huku amesimama still mikono kiuononi na , anatuangalia kwa jicho la hasira sana,ikabidi niache hizo story haraka sana na yule binti akajua amevuka red line akaondoka fasta.
 
Na wewe palikuwa na haja gani ya kusema ulipita na crown? Okee ilikuwa ni C. Athlete, Royal Saloon au Majesta?
ATHLETE...nikiwa na hela inatosha ntanunua Mustang ya 2011...maisha ndio haya haya...na nlisema crown sababu kulikuwa na vx za serikali so aliona kama me nipo kwenye gari chafu chafu mbuzi yule....mkuu ni kosa kusema crown ?

Na wewe palikuwa na haja gani ya kusema ulipita na crown? Okee ilikuwa ni C. Athlete, Royal Saloon au Majesta?
 
tatizo la madada wengi kwenye customer care na utoaji wa huduma huko maofisini ni namna walivyozipata hizo kazi... kwa binadamu aliyefuata taratibu za ajira na kupata ajira kwa haki hawezi kudharau mtu yeyote....
sahihi kabisa mkuu. wengi wenye nyodo wanajiona kama wana-godfather wao
 
tatizo la madada wengi kwenye customer care na utoaji wa huduma huko maofisini ni namna walivyozipata hizo kazi... kwa binadamu aliyefuata taratibu za ajira na kupata ajira kwa haki hawezi kudharau mtu yeyote....

Kuna ukweli sana kwny hili.
 
Sehemu nyingi watu sana dharau na nyodo, kipindi nasoma pale Thaqafa secondary school -mwanza wale walioko utawala ukiwauliza kitu wanajibu kwa nyodoo kudadeki utadhani hawaendi chooni.
Mwenge Catholic university wale ma sister pale utawala ndio wale wale tu
Ukienda benki vile vile, tuombe Mungu atupe unyenyekevu
MWECAU umewasingizia tu.
 
Dah mimi leo nimeenda banda la Mpesa natuma hela, namsalimia huyo dada haitikii afu kakaa ananiangalia kidharau, nikaanza kupaza sauti nimekusalimia unamaanisha hujasikia ama? Eti kinabinua mdomo, karibu, nikamuuliza nataka kutuma pesa kiasi fulani eti ndiyo kamenuna kabisa hadi ikabidi nihudumiwe na kaka mwingine waliekua wote hapo ofisini.

Mwingine mkoani huko tena mbaba, nilikua naulizia mifuko fulani hivi ya kuvunia mpunga, huwa inatofautiana size, nikamuuliza ipo akajibu ipo na bei akasema, eti namuambia naomba niione size yake hee akanijibu vibaya 'nimekwambia mifuko ipo huniamini ama? Duh namimi nikapata hasira nikamwambia basi acha tu si wewe peke yako unayeiuza bana. Nikaenda next duka akiwa ananiona huyo akanionesha ilivo hiyo mifuko na akaikunjua kabisa nikaridhika nikanunua tena mingi tu. Nikaona ananicheki nikajisemea nimekukomesha.
 
Back
Top Bottom