Umeshawahi kukutana na balaa la nyoka?

Umeshawahi kukutana na balaa la nyoka?

Kwan mikoa ya kusini suala la cobra sio habar ya kushangaza maana wamepakana na msumbiji, kule wanapatikana cobra maarufu duniani wanaitwa MOZAMBIQUE SPITTING COBRA, Ni hatar na nusu
Aisee wale Mozambique spiting cobra ni wanene, wepesi na wanatema mate mengi sana
 
Hapana mkuu,

Cobra ni nyoka mwingine na koboko ni mwingine pia. Na Kati ya hao wawili hatari zaidi ni koboko,ni nyoka mwenye kisirani na anapenda sifa za kijinga.

Unaweza kwenda kuchunga ng'ombe yet akaamua kukutia hasara akawagonga ng'ombe wote ili wafe tu akutie umasikini. Cobra anavimba Sana kwenye mashavu akiwa na hasira na anatema mate yenye sumu,nakumbuka cobra ameshawahi kumtia upofu ng'ombe wa shule kwa kumtemea mate yenye sumu Kali.
Koboko ni yule ambaye huwa anagonga Utosi Satoh?
 
Hapo kwenye kumrushia fimbo ndipo ulipofeli ila sa umesema ulikuwa darasa la 5 mi nlikuwa na mfuata namchapa hadi namuua.

Ngoja kinupe kisa kimoja......
siku moja tumetoka kanisani mida ya saa saba mchana, tumekaa nje kusikilizia msosi nje kulikuwa na karundo kadogo ka matofali ya kuchoma sina hili wala lile nimekaa jirani kabisa na hayo matofali kuja kuhamaki nyoka mreefu wa rangi ya kijivu kilichokolea akamkosakosa kuku yupo kwenye yake matofali nikachukua fimbo ngumu nikaanza kuoangua tofali moja baada ya jingine nikamuona nlichofanya sikumpiga nikamminya kichwa na ile fimbo kisha nikamshika shingoni jirani kabisa na kichwa kumuinua nalingana nae urefu, maza kuona alipiga ukunga hadi majirani wakajaa anyways kukamata nyoka nlifunzwa na wachina maana nlikulia kambi ya jeshi ambapo wachina waliishi jirani kama wakufunzi wa ndegevita. Nlikuwa form3
Duh,

Japo siogopi nyoka,ila kumshika sipendi kabisa. Huo ujasiri sijawahi kuwa nao asee!! Akinigusa mwilini vile anavyoteleza nakuwa nasisimka Sana.
 
Hapana mkuu,

Cobra ni nyoka mwingine na koboko ni mwingine pia. Na Kati ya hao wawili hatari zaidi ni koboko,ni nyoka mwenye kisirani na anapenda sifa za kijinga.

Unaweza kwenda kuchunga ng'ombe yet akaamua kukutia hasara akawagonga ng'ombe wote ili wafe tu akutie umasikini. Cobra anavimba Sana kwenye mashavu akiwa na hasira na anatema mate yenye sumu,nakumbuka cobra ameshawahi kumtia upofu ng'ombe wa shule kwa kumtemea mate yenye sumu Kali.
Koboko ukimzingua dakika 0 unamkuta katikati ya miguu yako keshafanya yake. Anaweza kukugonga mara tatu mfululizo. Yule kisirani siyo kabisa.
 
Koboko ukimzingua dakika 0 unamkuta katikati ya miguu yako keshafanya yake. Anaweza kukugonga mara tatu mfululizo. Yule kisirani siyo kabisa.
Unavyoelezea utafikiri unamfahamu ana kwa ana😂😂
 
Duh,

Japo siogopi nyoka,ila kumshika sipendi kabisa. Huo ujasiri sijawahi kuwa nao asee!! Akinihusa mwilini bile anavyoteleza nakuwa nasisimka Sana.
Jamaa wa kwanza kunifunza kushika nyoka alikuwa anatokea Mtwara huko nyoka ni kama mchwa so ni kitu cha kawaida. Tukiwa form one tunafyeka majani shuleni akaonekana nyoka wanafunzi wakaanza kelele yule jamaa alimbana na kwanja shingoni akamshika. 🙂🙂
 
Hapo kwenye kisa cha kwanza cobra.
Kuna aina nyingi za cobra. Cobra anaerusha mate ni aina moja tu anaitwa Mozambique spitting cobra (Moza)
Angekua ni Moza angekua amekurushia mate muda mrefu sana na asingekukosa.

Kuhusu chatu yeye hana sumu ila ni hatari sana.
Hivi chatu huwa anawekaje mtego wake akiwa ana winda?
 
Unavyoelezea utafikiri unamfahamu ana kwa ana😂😂
Tukiwa shule aliwahi kumvaa jamaa mmoja mkononi akamgonga chap mara mbili aisee yule nyoka jasiri sana. Yan alitoka kwenye tawi la mti akamvaa jamaa mkononi akajivirinvisha hapo hapo mkononi akaanza kugonga jamaa huku anashangaa.
 
Urambo,tabora!!koboko msikie tu,ni kiburi,mbabe na mshenzi haswa! Kuna jamaa alimpga na jiwe ikawa kosa kupita ile njia!alikua anagonga kila kinachopita hadi raia tukabadili njia,ilibid wamwue kwa gobole la magololi maana alikua tishio! pia niliwa kutana na koboko huko huko urambo ghafula aloo nilisali sala zote maana alisimama na kutoa kunitazama my next act ili ajibu,uzur nilitulia mwisho akasepa zake!almost Tabora yote koboko wapo na hawana noma na mtu ila ukimchokoza umekwenda na maji!
 
Urambo,tabora!!koboko msikie tu,ni kiburi,mbabe na mshenzi haswa! Kuna jamaa alimpga na jiwe ikawa kosa kupita ile njia!alikua anagonga kila kinachopita hadi raia tukabadili njia,ilibid wamwue kwa gobole la magololi maana alikua tishio! pia niliwa kutana na koboko huko huko urambo ghafula aloo nilisali sala zote maana alisimama na kutoa kunitazama my next act ili ajibu,uzur nilitulia mwisho akasepa zake!almost Tabora yote koboko wapo na hawana noma na mtu ila ukimchokoza umekwenda na maji!
Kumbe ukitulia anasepa?
 
Back
Top Bottom