Chatu na dereva wa gari za Dangote.
Miaka kadhaa iliyopita Kuna Docta mmoja alikuwa anatoka Dar anaelekea Masasi mkoani Mtwara kwa mambo yake binafsi. Alipofika ndani ya viunga vya wilaya ya kilwa mkoani Lindi kwa mbali mbele yake akaoana na gari (roli) ya Dangote ambayo ilikuwa inaelekea Mtwara. Baada ya dakika chache jamaa wa Dangote akapunguza mwendo akapaki kando ya barabara Kisha akashuka akasogea kwa ndani kwenye majani. Ilikuwa mida ya jioni Kama saa kumi na moja. Doctor akalipta lile roli na kuendelea na safari yake.
Kesho yake Doctor alipomaliza mishe zake mjini Masasi akawasha gari na kurudi Dar. Cha ajabu alipofika eneo lile la Jana mahali gari la Dangote limepaki alilikuta lipo vile vile. Na gari halikuwekwa triange kuashiria kwamba limehaeibika. Ilikiwa Kama limepaki kwa muda Kisha safari itaendelea.
Jamaa akapunguza mwendo Kisha akawa anaendesha mdogo mdogo mpaka usawa wa lile roli. Akapaki pembeni Kisha akashuka na kuvuka barabara kwenda upande wa pili kuangalia pengine dereva ana shida au amepata ugonjwa wa ghafla alafu watu/madereva wapita njia wasijue maana gari halikuonekana Kama Lina ishara ya kuharibika na halikuwa na mzigo maana lilikuwa linarudi Mtwara.
Alipofika akapiga hodi kwa mlango wa dereva hakukuwa na response yoyote. Akajaribu kufungua mlango ukafunguka bila shida. Akaangalia ndani hakuona mtu. Wasiwasi ukamwingia akahisi Kuna uwezekano wa tatizo,ile haikuwa hali ya kawaida.
Akasogea barabarani kuangalia magari yanayokuja. Kwa bahati Kuna gari ndogo ikawa inapita akaipungia mkono ikasimama. Wakapita madereva Kama watatu nao wakasimama. Jamaa akawasimulia kilichotokea kuanzia jana. Wakaamua kuingia kwa ndani,ndani ya kamsitu kuangalia Kama wataona chochote.
Kilichotokea....
Kumbe yule dereva ile Jana aliposhuka kwenye gari alienda kujisaidia (tafsida). Huko porini ndiyo akakutana na balaa la chatu. Inavyoonyesha chatu aliweka mtego jamaa akauingia,na kwa kukosa msaada akazidiwa nguvu akauawa Kisha akamezwa.
Pale porini walimkuta chatu amelala hoi kwa kushiba na tumbo lake limejichora alama ya mtu akiwa amelala kwa kunyooka.
Taarifa ikawafikia wenye mamlaka,chatu akauawa na marehemu akatolewa nje ya mwili wa chatu. Picha za yule jamaa zilikuwa zinatisha sana maana alimezwa mzima mzima,yeye,viatu hadi nguo. Alikuwa Kama amemwagiwa mayai au mlenda.
Kama humu ndani Kuna madereva au wahusika wa Dangote wanaweza kukumbuka hiki kisa Cha dereva wao aliyemezwa na chatu Miaka kadhaa iliyopita.
Kuna kisa kingine Cha kishujaa Kati ya chatu na Mamba...
Narudi