Umeshawahi kukutana na balaa la nyoka?

Umeshawahi kukutana na balaa la nyoka?

Hiyo story ya cobra, nikwamba asubuhi kabla ya jua kuchomoza reptilia (damu baridi)nyoka, mijusi, kenge, mamba... wote wanakuwa hawana nguvu, hata kuwinda hawawezi. Lazima wakae juani kupasha mwili joto ndio wanakuwa active, ndio maana hakukushambulia.
 
Ilikuwa Aidha atuue sisi au tumuue yeye. Alikuwa mkubwa sana mweusi anatanua mashavu yake halafu anatema mate kwa njia ya kukurushia~wanasema yakikupata machoni unapofuka, ilikuwa hatari mno
Kwahiyo nje na kutema mate cobra hana silaha nyingine nikimaanisha labda kung'ata etc? Na je mate yake yakikupata sehemu nyingine ya mwili sio machoni nn kinatokea?
 
Kwahiyo nje na kutema mate cobra hana silaha nyingine nikimaanisha labda kung'ata etc? Na je mate yake yakikupata sehemu nyingine ya mwili sio machoni nn kinatokea?
Kobra ana ng'ata na kudunga sumu. Silaha yake ya kutemea / kurushia mate ni anapokuwa kwa mbali anaanza nayo hiyo kisha akikufikia anakutandika meno na kukudunga sumu kwa njia hiyo na ni kwa Kasi ya ajabu.

Mate yake yakikupata sehemu tofauti na machoni yanasababisha muwasho mkali na kwa baadhi ya watu eneo hilo huvimba hata wakati mwingine hutoa vidonda vinavyosababishwa na kujikuna sana.
 
Ilikuwa Aidha atuue sisi au tumuue yeye. Alikuwa mkubwa sana mweusi anatanua mashavu yake halafu anatema mate kwa njia ya kukurushia~wanasema yakikupata machoni unapofuka, ilikuwa hatari mno
1. Hupofuki moja kwa moja, utavimba then baada ua siku 3 unapona
2. Kobra sio mrahisi king'ata bali kukitemea mate
3. Huwa hsogopi endapo umesimama kwenye shimo lake atakunyookea ulipo hadi umpishe aingie au umuue
 
Kobra ana ng'ata na kudunga sumu. Silaha yake ya kutemea / kurushia mate ni anapokuwa kwa mbali anaanza nayo hiyo kisha akikufikia anakutandika meno na kukudunga sumu kwa njia hiyo na ni kwa Kasi ya ajabu.

Mate yake yakikupata sehemu tofauti na machoni yanasababisha muwasho mkali na kwa baadhi ya watu eneo hilo huvimba hata wakati mwingine hutoa vidonda vinavyosababishwa na kujikuna sana.
Lakini kobra hawezi kukufuata akung'ate kama hujamzuia kuingia kwenye shimo lake.
Sio nyoka mchokozi wala mkorofi.
Atakung'ata:
1. Ukimkanyaga
2. Ukimzuia kuingia shimoni kwake....huwa hawezi kuingia shimo jipya
 
Duh,

Maswali mengine Ni ya ajabu Sana,itakuwa wewe ni mtoto wa Dar hujawahi kutoka nje ya Dar kutembelea mikoani. Unashangaa cobra Tz?
Kwan mikoa ya kusini suala la cobra sio habar ya kushangaza maana wamepakana na msumbiji, kule wanapatikana cobra maarufu duniani wanaitwa MOZAMBIQUE SPITTING COBRA, Ni hatar na nusu
 
Back
Top Bottom