Satoh Hirosh
JF-Expert Member
- Mar 30, 2021
- 5,950
- 23,264
Kuna mtu ukimtania "hapo chini Kuna nyoka" ni Kama unatafuta kumuua kwa presha, hawapendi kabisa kuleteana utani wa nyoka. Wengine wakijua ndani, nyumba wanazoishi Kuna nyoka ataikimbia nyumba na kuitelekeza kabisa hadi asikie nyoka ameshauawa.
Sasa, Kuna akina sisi ambao huwa hatuogopi nyoka. Kuna baadhi ya matukio nayakumbuka na mengine najiona mjinga Sana kwa kucheza na mdudu huyu hatari Sana.
====
Enzi hizo nipo kijana mdogo wa darasa la tano, siku moja ilikuwa msimu wa baridi Kali (kipupwe). Kwetu kipindi Cha baridi Hali inakuwa tete kwa sisi tusiopenda maji, inafikia wakati baridi linakuwa Kali Hadi mchanga ukikanyaga bila viatu unahisi umekanyaga barafu. Kipindi hiki swala la kuoga linageuka kuwa Jambo la ufahari.
Sasa siku moja nikiwa nimejiandaa mapema Sana ili niwahi shule kuchukua namba maana mwalimu wa zamu alikuwa mnoko. Kwa sababu ya baridi kuwa kali, nikagahilisha swala la kuoga, nikapiga mswaki Kisha nikanawa uso na kutinga uniform tayari kwenda shule. Sasa njiani Kuna zile nyasi zilizopata umande. Nikijiangalia miguuni naona miguu Kama imepakwa chokaa, habari ya kupaka mafuta usiku kabla ya kulala upo kijijini unaanzia wapi? Nikasema hii miguu hapana kwa kweli, imezido kuchakaa, nikawa nimehama njia na kuanza kupita kwenye nyasi zenye maji (umande) ili kusafisha miguu. Hapo miguuni nimevaa kandambili alafu kitendo Cha kupita kwenye nyasi zenye maji zikawa Safi hadi nikiwa nainua mguu kandambili inaitika waah!! .Watoto wa siku hizi wa gari za njano na wakiamka wanasalimia good morning Dad and mamy hawaelewi hizi mambo za kunawa maji ya umande.
Sasa wakati nimehama njia natembea kwenye nyasi ili kuosha miguu, huku kidumu na fagio vipo mikononi, Ghafla..!! Cobra akiwa amevimbisha shingo huku amejaza mate yenye sumu alikuwa ameshajihami yupo mbele yangu tayari yupo katika mkao wa kushambulia. Wakati nimetaharuki nawaza nini Cha kufanya yeye ndiyo kwanza akasogea barabarani kweupe kabisa. Ni Kama alisogea mbele kuniblock nisiende shule. Nikaangalia nyuma Kama Kuna mtu anakuja nikawa naona ukungu tu, nilikuwa mzee wa kuwahi Sana. Wale wanafunzi wanaowahi sana shule. Nidhamu nyingi. Hata hivyo kwa sababu sikuwa mwoga wa nyoka nikasema leo mbona tutanyooshana tu. Pembeni yangu kulikuwa na mti mrefu kidogo nikauchukua nikatoa vitawi ikabaki fimbo. Nikaanza kumrushia.
Sasa Cobra kwa kukwepa ndiyo mwaliku wao. Kila nikirusha anakwepa alafu ananifokea balaa huku amejaza lundo la mate yenye sumu shingoni. Lakini Cha ajabu Wala harudishi mashambulizi wala kunitemea mate yake yaliyojaa shingoni yenye sumu Kali.
Kumbe nyoka ana akili Sana.
Wakati najiona Kama napambana nae nimuue kumbe mwenzangu ananiona Kama mtoto tu nisiye na hatia akawa ananikwepa pasi na kunidhuru. Ilikuwa Kama anacheza na Mimi maana hata nguvu ya kurusha ule mti ilikuwa dhaifu Sana kwa sababu ya umri wangu.
Alipoona nimetaharuki huku macho yamenitoka Kama tochi nakaribia kulia alafu sina msaada akaamua kuinama chini na kusepa mdogo mdogo na kuishia zake porini. Alipotokomea ndiyo nikakumbuka Kumbe nilibeba kidumu cha maji na fagio, sijui nimevitupa wapi. Nikavitafuta nikakuta nilivitupa kwenye majani, maji yameshamwagika maana kidumu hakikuwa na mfuniko. Nikasepa zangu shule miguu ikiwa haina nguvu kabisa.
Ila sikukoma, niliendelea na tabia yangu ya hovyo na kukutana na balaa la nyoka? Ilikuwaje?
Sasa, Kuna akina sisi ambao huwa hatuogopi nyoka. Kuna baadhi ya matukio nayakumbuka na mengine najiona mjinga Sana kwa kucheza na mdudu huyu hatari Sana.
====
Enzi hizo nipo kijana mdogo wa darasa la tano, siku moja ilikuwa msimu wa baridi Kali (kipupwe). Kwetu kipindi Cha baridi Hali inakuwa tete kwa sisi tusiopenda maji, inafikia wakati baridi linakuwa Kali Hadi mchanga ukikanyaga bila viatu unahisi umekanyaga barafu. Kipindi hiki swala la kuoga linageuka kuwa Jambo la ufahari.
Sasa siku moja nikiwa nimejiandaa mapema Sana ili niwahi shule kuchukua namba maana mwalimu wa zamu alikuwa mnoko. Kwa sababu ya baridi kuwa kali, nikagahilisha swala la kuoga, nikapiga mswaki Kisha nikanawa uso na kutinga uniform tayari kwenda shule. Sasa njiani Kuna zile nyasi zilizopata umande. Nikijiangalia miguuni naona miguu Kama imepakwa chokaa, habari ya kupaka mafuta usiku kabla ya kulala upo kijijini unaanzia wapi? Nikasema hii miguu hapana kwa kweli, imezido kuchakaa, nikawa nimehama njia na kuanza kupita kwenye nyasi zenye maji (umande) ili kusafisha miguu. Hapo miguuni nimevaa kandambili alafu kitendo Cha kupita kwenye nyasi zenye maji zikawa Safi hadi nikiwa nainua mguu kandambili inaitika waah!! .Watoto wa siku hizi wa gari za njano na wakiamka wanasalimia good morning Dad and mamy hawaelewi hizi mambo za kunawa maji ya umande.
Sasa wakati nimehama njia natembea kwenye nyasi ili kuosha miguu, huku kidumu na fagio vipo mikononi, Ghafla..!! Cobra akiwa amevimbisha shingo huku amejaza mate yenye sumu alikuwa ameshajihami yupo mbele yangu tayari yupo katika mkao wa kushambulia. Wakati nimetaharuki nawaza nini Cha kufanya yeye ndiyo kwanza akasogea barabarani kweupe kabisa. Ni Kama alisogea mbele kuniblock nisiende shule. Nikaangalia nyuma Kama Kuna mtu anakuja nikawa naona ukungu tu, nilikuwa mzee wa kuwahi Sana. Wale wanafunzi wanaowahi sana shule. Nidhamu nyingi. Hata hivyo kwa sababu sikuwa mwoga wa nyoka nikasema leo mbona tutanyooshana tu. Pembeni yangu kulikuwa na mti mrefu kidogo nikauchukua nikatoa vitawi ikabaki fimbo. Nikaanza kumrushia.
Sasa Cobra kwa kukwepa ndiyo mwaliku wao. Kila nikirusha anakwepa alafu ananifokea balaa huku amejaza lundo la mate yenye sumu shingoni. Lakini Cha ajabu Wala harudishi mashambulizi wala kunitemea mate yake yaliyojaa shingoni yenye sumu Kali.
Kumbe nyoka ana akili Sana.
Wakati najiona Kama napambana nae nimuue kumbe mwenzangu ananiona Kama mtoto tu nisiye na hatia akawa ananikwepa pasi na kunidhuru. Ilikuwa Kama anacheza na Mimi maana hata nguvu ya kurusha ule mti ilikuwa dhaifu Sana kwa sababu ya umri wangu.
Alipoona nimetaharuki huku macho yamenitoka Kama tochi nakaribia kulia alafu sina msaada akaamua kuinama chini na kusepa mdogo mdogo na kuishia zake porini. Alipotokomea ndiyo nikakumbuka Kumbe nilibeba kidumu cha maji na fagio, sijui nimevitupa wapi. Nikavitafuta nikakuta nilivitupa kwenye majani, maji yameshamwagika maana kidumu hakikuwa na mfuniko. Nikasepa zangu shule miguu ikiwa haina nguvu kabisa.
Ila sikukoma, niliendelea na tabia yangu ya hovyo na kukutana na balaa la nyoka? Ilikuwaje?