Umeshawahi kukutana na balaa la nyoka?

Umeshawahi kukutana na balaa la nyoka?

Hapo kwenye kisa cha kwanza cobra.
Kuna aina nyingi za cobra. Cobra anaerusha mate ni aina moja tu anaitwa Mozambique spitting cobra (Moza)
Angekua ni Moza angekua amekurushia mate muda mrefu sana na asingekukosa.

Kuhusu chatu yeye hana sumu ila ni hatari sana.
 
kuna siku nimeenda kijijini sasa katika harakati nikapata demu mmoja hivi tukawa tuko sehemu tuna kulana tumemaliza tukawa tuna sindikizana taratibu bila shida sasa tukafika mahali tukaagana wakati mimi naondoka na njia moja hv ya nyasi ndogo naona ghafla nyoka wawili wanatokea upande wa kushoto. wakati manzi ananiangalia nikiwa naondoka akashangaa nakimbia shambani bila mipangilio naenda mbele naona mwingine aisee nilipotelea bondeni bila kupenda akili imekuja kurudi niko kilometa mbili nahema natetemeka maana yule nyoka alikuwa wa kijivu na amesimamisha kichwa aisee manzi alikuwa nanishanga.

nafika home nimesahau kama nilitoka kupiga show na nimeingia ndani nahisi kila kona kuna nyoka acha kabisaaa
 
Mi hata story zinahusu manyoka sizipendi kwa kweli. Hapa nimeanza kuangalia angalia mazingira niliokaa isije kuwa kuna nyoka ananivizia!
Leo utamkuta ghetto
Screenshot_20230518_174358_Instagram%20Lite.jpg
 
Ulivyosema ulikuwa unatumia fimbo kupiga nyoka umenikumbusha tukio moja la miaka ya nyuma.

Wakati niko shambani nalima kuna nyoka akakatiza mbele yangu, nikasema huyu simuachi.

Nikachukua fimbo ndefu nikawa namchapa nayo ila alikuwa yuko fasta kukwepa. Ghafla nilikuta nilivyorusha kumchapa akairukia ile fimbo akawa anatembea juu yake kuja kwangu.

Aisee nilipagawa niliachia ile fimbo nikafanya mara 3 ya kile anachokifanyaga Usain Bolt
Ukiwa unakimbia matukio hatarishi Kama la nyoka,miguu inakuwa haigusi chini. Kiufupi unakuwa unapaa.
 
Hiyo story ya cobra, nikwamba asubuhi kabla ya jua kuchomoza reptilia (damu baridi)nyoka, mijusi, kenge, mamba... wote wanakuwa hawana nguvu, hata kuwinda hawawezi. Lazima wakae juani kupasha mwili joto ndio wanakuwa active, ndio maana hakukushambulia.
Aisee,

Me nilidhani alinionea huruma maana nilishaanza kulia na kutaharuki.
 
Kwan mikoa ya kusini suala la cobra sio habar ya kushangaza maana wamepakana na msumbiji, kule wanapatikana cobra maarufu duniani wanaitwa MOZAMBIQUE SPITTING COBRA, Ni hatar na nusu
Na haya matukio yote niliyosimulia kasoro la Dangote yametokea kusini kwa mzee Membe RIP.
 
Back
Top Bottom