Umeshawahi kukutana na balaa la nyoka?

Umeshawahi kukutana na balaa la nyoka?

Ana rangi gani? Kuna mtu kaandika kuwa ndiye black mamba.
Black mamba ni kutokana na mdomo kuwa mweusi, yeye wa kijani mpauko na kaki flani yenye ukijani kwa mbali
Screenshot_20230519-144337_Chrome.jpg
 
Kobra ana ng'ata na kudunga sumu. Silaha yake ya kutemea / kurushia mate ni anapokuwa kwa mbali anaanza nayo hiyo kisha akikufikia anakutandika meno na kukudunga sumu kwa njia hiyo na ni kwa Kasi ya ajabu.

Mate yake yakikupata sehemu tofauti na machoni yanasababisha muwasho mkali na kwa baadhi ya watu eneo hilo huvimba hata wakati mwingine hutoa vidonda vinavyosababishwa na kujikuna sana.
Na akipiga mara tisa mfulurizo ndipo, huishia nguvu, Wale wanao kamata nyoka wengine hutumia kioo, cobra akiona picha yake kwenye kioo, huanza kikgonga akizani nyoka mwingine, ila akisha fikisha mara tisa huishiwa nguvu, ndipo wakamata hutumia nafasi hiyo kumkata na kumtoa meno.
 
Na akipiga mara tisa mfulurizo ndipo, huishia nguvu, Wale wanao kamata nyoka wengine hutumia kioo, cobra akiona picha yake kwenye kioo, huanza kikgonga akizani nyoka mwingine, ila akisha fikisha mara tisa huishiwa nguvu, ndipo wakamata hutumia nafasi hiyo kumkata na kumtoa meno.
Sijawahi kujua hili
 
Kobra ana ng'ata na kudunga sumu. Silaha yake ya kutemea / kurushia mate ni anapokuwa kwa mbali anaanza nayo hiyo kisha akikufikia anakutandika meno na kukudunga sumu kwa njia hiyo na ni kwa Kasi ya ajabu.

Mate yake yakikupata sehemu tofauti na machoni yanasababisha muwasho mkali na kwa baadhi ya watu eneo hilo huvimba hata wakati mwingine hutoa vidonda vinavyosababishwa na kujikuna sana.
Narudia tena mkuu...
Kama hujamkanyaga au hujamzuia kuingia shimoni kwake cobra kamwe hawezi kukufuata akudunge.
Nimeishi maeneo yenye cobra na nimewahi kuua cobra wakubwa tu nikiwa peke yangu.
Ukimpiga nshingo aliyoinyanyua na kuitanua huwa anajizinga kwenye fimbo na habari yake inaishia hapo
 
Ulivyoandika Swila umenikumbusha mbali sana Gereza, Ushora
Na swila ni jamii ya cobra, ila huyu ukiktana nae kwenye 18 za huwa anafukuza ili mradi tu akugonge, na kama akikugonga huduma ya kwanza kama iko mbali andika usia.

Huyu nyoka alisha wahi nipandia juu ya mti aje kunigonga, kilichoniokoa ujana tu nilidandia tawi la mti mwingine wa karibu kama nyani wafanyavyo, nikadanda chini nikakimbia.
 
Kuna mtu ukimtania "hapo chini Kuna nyoka" ni Kama unatafuta kumuua kwa presha,hawapendi kabisa kuleteana utani wa nyoka. Wengine wakijua ndani, nyumba wanazoishi Kuna nyoka ataikimbia nyumba na kuitelekeza kabisa hadi asikie nyoka ameshauawa.

Sasa,Kuna akina sisi ambao huwa hatuogopi nyoka. Kuna baadhi ya matukio nayakumbuka na mengine najiona mjinga Sana kwa kucheza na mdudu huyu hatari Sana.


==============================================
Enzi hizo nipo kijana mdogo wa darasa la tano,siku moja,ilikuwa msimu wa baridi Kali (kipupwe). Kwetu kipindi Cha baridi Hali inakuwa tete kwa sisi tusiopenda maji,inafikia wakati baridi linakuwa Kali Hadi mchaanga ukikanyaga bila viatu unahisi umekanyaga barafu. Kipindi hiki swala la kuoga linageuka kuwa Jambo la ufahari.

Sasa siku moja nikiwa nimejiandaa mapema Sana ili niwahi shule kuchukua namba maana mwalimu wa zamu alikuwa mnoko,Kwa sababu ya baridi kuwa kali,nikagahilisha swala la kuoga,nikapiga mswaki Kisha nikanawa uso na kutinga uniform tayari kwenda shule. Sasa njiani Kuna zile nyasi zilizopata umande. Nikijiangalia miguuni naona miguu Kama imepakwa chokaa,habari ya kupaka maguta usiku kabla ya kulala upo kijijini unaanzia wapi? Nikasema hii miguu hapana kwa kweli,imezido kuchakaa, nikawa nimehama njia na kuanza kupita kwenye nyasi zenye maji (umande) ili kusafisha miguu. Hapo miguuni nimevaa kandambili alafu kitendo Cha kupita kwenye nyasi zenye maji zikawa Safi hadi nikiwa nainua mguu kandambili inaitika waah!! .Watoto wa siku hizi wa gari za njano na wakiamka wanasalimia good morning Dad and mamy hawaelewi hizi mambo za kunawa maji ya umande.

Sasa wakati nimehama njia natembea kwenye nyasi ili kuosha miguu,huku kidumu na fagio vipo mikononi..Ghafla..!! Cobra akiwa amevimbisha shingo huku amejaza mate yenye sumu alikuwa ameshajihami yupo mbele yangu tayari yupo katika mkao wa kushambulia. Wakati nimetaharuki nawaza nini Cha kufanya yeye ndiyo kwanza akasogea barabarani kweupe kabisa. Ni Kama alisogea mbele kuniblock nisiende shule. Nikaangalia nyuma Kama Kuna mtu anakuja nikawa naona ukungu tu,nilikuwa mzee wa kuwahi Sana,Wale wanafunzi wanaowahi sana shule..Nidhamu nyingi!!! Hata hivyo kwa sababu sikuwa mwoga wa nyoka nikasema leo mbona tutanyooshana tu!! Pembeni yangu kulikuwa na mti mrefu kidogo nikauchukua nikatoa vitawi ikabaki fimbo. Nikaanza kumrushia.

Sasa Cobra kwa kukwepa ndiyo mwaliku wao,Kila nikirusha anakwepa alafu ananifokea balaa huku amejaza lundo la mate yenye sumu shingoni. Lakini Cha ajabu Wala harudishi mashambulizi wala kunitemea mate yake yaliyojaa shingoni yenye sumu Kali.

Kumbe nyoka ana akili Sana.

Wakati najiona Kama napambana nae nimuue,Kumbe mwenzangu ananiona Kama mtoto tu nisiye na hatia akawa ananikwepa pasi na kunidhuru. Ilikuwa Kama anacheza na Mimi maana hata nguvu ya kurusha ule mti ilikuwa dhaifu Sana kwa sababu ya umri wangu.

Alipoona nimetaharuki huku macho yamenitoka Kama tochi nakaribia kulia alafu sina msaada akaamua kuinama chini na kusepa mdogo mdogo na kuishia zake porini. Alipotokomea ndiyo nikakumbuka Kumbe nilibeba kidumu cha maji na fagio,sijui nimevitupa wapi. Nikavitafuta nikakuta nilivitupa kwenye majani,maji yameshamwagika maana kidumu hakikuwa na mfuniko. Nikasepa zangu shule miguu ikiwa haina nguvu kabisa.

Ila sikukoma,niliendelea na tabia yangu ya hovyo ya n kukutana na balaa la nyoka? Ilikuwaje?
Hapo kwenye kumrushia fimbo ndipo ulipofeli ila sababu umesema ulikuwa darasa la 5, mi nlikuwa na mfuata namchapa hadi namuua.

Ngoja kinupe kisa kimoja......
siku moja tumetoka kanisani mida ya saa saba mchana, tumekaa nje kusikilizia msosi nje kulikuwa na karundo kadogo ka matofali ya kuchoma sina hili wala lile nimekaa jirani kabisa na hayo matofali kuja kuhamaki nyoka mreefu wa rangi ya kijivu kilichokolea akamkosakosa kuku yupo kwenye yale matofali nikachukua fimbo ngumu nikaanza kupangua tofali moja baada ya jingine nikamuona nlichofanya sikumpiga nikamminya kichwani na ile fimbo kisha nikamshika shingoni jirani kabisa na kichwa kumuinua nalingana nae urefu, maza kuona alipiga ukunga hadi majirani wakajaa 🤣🤣🤣

Anyways kukamata nyoka nlifunzwa na wachina maana nlikulia kambi ya jeshi ambapo wachina waliishi kama wakufunzi wa ndegevita. Kipindi hicho nlikuwa kidato cha tatu.
 
Narudia tena mkuu...
Kama hujamkanyaga au hujamzuia kuingia shimoni kwake cobra kamwe hawezi kukufuata akudunge.
Nimeishi maeneo yenye cobra na nimewahi kuua cobra wakubwa tu nikiwa peke yangu.
Ukimpiga nshingo aliyoinyanyua na kuitanua huwa anajizinga kwenye fimbo na habari yake inaishia hapo
Ni kweli mimi ilinikuta nikiwa moshi 2005 majira ya mchana nimezunguka mbele ya nyumba kuchota maji kwenye pipa lilikuwa linakinga maji ya mvua basi nikiwa nimeinama nachota maji naangalia pembeni yangu namuona cobra mkubwa sana wa kijivu katunisha shingo yake ananiangalia jamani nilipiga kelele kubwa mpaka cobra mwenyewe akachanganyikiwa na kukimbia kupanda kibarazani anatafuta pa kujificha akazama ndani kupitia chini ya mlango tukaziba na dekio ikabaki nafasi kidogo akaenda kutafutwa mkamata nyota akazama humo ndani alimtafuta na hakufanikiwa kumuona huyo cobra.
 
Ni kweli mimi ilinikuta nikiwa moshi 2005 majira ya mchana nimezunguka mbele ya nyumba kuchota maji kwenye pipa lilikuwa linakinga maji ya mvua basi nikiwa nimeinama nachota maji naangalia pembeni yangu namuona cobra mkubwa sana wa kijivu katunisha shingo yake ananiangalia jamani nilipiga kelele kubwa mpaka cobra mwenyewe akachanganyikiwa na kukimbia kupanda kibarazani anatafuta pa kujificha akazama ndani kupitia chini ya mlango tukaziba na dekio ikabaki nafasi kidogo akaenda kutafutwa mkamata nyota akazama humo ndani alimtafuta na hakufanikiwa kumuona huyo cobra.
Mwisho ilikuwaje?
 
Mwisho ilikuwaje?
Mwisho ndo hivyo cobra hakuoneka tukahisi labda alitumia nafasi iliyobaki kutoka nje maana tulivyoziba tuliondoka kwenda kumtafuta mkamataji . Lakini angekuwa wa kuning’ata basi ingekuwa hivyo maana nilisimama karibu yake kabisa na nilivyomuona nikaanza kupiga kelele sikusogea hata hatua moja zaidi cobra ndo alianza kukimbia nilikuwa darasa la sita,imagine angekuwa nyoka aina nyingine basi ningebaki historia tuu.
 
Mwisho ndo hivyo cobra hakuoneka tukahisi labda alitumia nafasi iliyobaki kutoka nje maana tulivyoziba tuliondoka kwenda kumtafuta mkamataji . Lakini angekuwa wa kuning’ata basi ingekuwa hivyo maana nilisimama karibu yake kabisa na nilivyomuona nikaanza kupiga kelele sikusogea hata hatua moja zaidi cobra ndo alianza kukimbia nilikuwa darasa la sita,imagine angekuwa nyoka aina nyingine basi ningebaki historia tuu.
Cobra usipomkanyaga hakung'ati hili nina uhakika nalo 100%
 
Na swila ni jamii ya cobra, ila huyu ukiktana nae kwenye 18 za huwa anafukuza ili mradi tu akugonge, na kama akikugonga huduma ya kwanza kama iko mbali andika usia.

Huyu nyoka alisha wahi nipandia juu ya mti aje kunigonga, kilichoniokoa ujana tu nilidandia tawi la mti mwingine wa karibu kama nyani wafanyavyo, nikadanda chini nikakimbia.
Yeah ni kisanga sana, mpaka nimecheka nikikumbuka mambo yake enzi hizo kwenye mashamba ya Gereza Ushora daaah! 😝😝

Unawafahamu Kanga na kware?
 
Back
Top Bottom