Hum B
JF-Expert Member
- Sep 17, 2014
- 1,065
- 1,540
Mkuu Rudi usome ulicho andikaMaumivu ya kuhongwa na nyoka ni makalio mno ni kama nge mara saba
Mkuu Rudi usome ulicho andikaMaumivu ya kuhongwa na nyoka ni makalio mno ni kama nge mara saba
Urambo,tabora!!koboko msikie tu,ni kiburi,mbabe na mshenzi haswa! Kuna jamaa alimpga na jiwe ikawa kosa kupita ile njia!alikua anagonga kila kinachopita hadi raia tukabadili njia,ilibid wamwue kwa gobole la magololi maana alikua tishio! pia niliwa kutana na koboko huko huko urambo ghafula aloo nilisali sala zote maana alisimama na kutoa kunitazama my next act ili ajibu,uzur nilitulia mwisho akasepa zake!almost Tabora yote koboko wapo na hawana noma na mtu ila ukimchokoza umekwenda na maji!
Muongo sana eti nyoka wote, wakati hata usiku huu kuna nyoka utamchezea😂😂Zoote hata kiwe kidogo km mnyoo, kwanza mnyoo nauogopa nao
😂😂😂😂 Laiti ungejua sina namna ya kumpata huyo nyoka, tatizo baridi la kwenu ni kali mwee nawaza July itakuwaje itabidi nikimbie aiseeMuongo sana eti nyoka wote, wakati hata usiku huu kuna nyoka utamchezea😂😂
Kuna pori linaitwa ipemba mpazi kuna nyoka wengi sanaTabora nyoka ni wengi kulko raia sababu ya mapori
Naogopa sana na sijawahi ona kwa macho. Mwaka huu mtoto wangu ilikuwaa usiku tupo nje yeye alisimama kwenye majani ghafla akaja analia amegongwa na nyoka mimi sikumwona ila yeye anasema kamuona wa black ( mweusi). Nilikuwa na jirani yangu akamwangalia akasema huyo sio nyoka atakuwa mdudu tuu wa kawaida mimi sijui kitu.
Tumekaa ndani kama dk 5 hivi mguu ukaanza kuvimba, bahati kuna bodaboda niliagiza msosi akawa analeta akashangaa leo mbona anko mpole sio kawaida yake nikamwambia kuna mdudu kamng'ata anavimba mguu kuja kumwangalia nusu aninase vibao aisee.
Akamfunga mguu kumbeba mbio mpaka kwa huyo mzee anamjua ndio kumpa dawa ya kunywa na nyingine akampaka na kusugulia mguu wote. Akaendelea na dawa hizo siku hadi ilipoisha Yule boda boda alinambia kama nisingekuja kwa dk 10 mbele ulikuwa unamkosa mtoto huyu. Yaani sikulala karibia wiki kwa woga.
Acha kabisa kaka
Mbezi beach moja hii. Hata ukiambiwa Bongo kuna vinyonga utabisha.Bongo tuna Cobra?? Eneo gani?. Ungenambia koboko sawa.
umechanganya kidogo ndugu... yule anayewika ni mwingine kabisa (kiswahili halisi sijui ila kikwetu tunamuita ntuanyika). koboko yeye ni mrefu, mgongoni kama amesukwa na jina lake ni black mamba hata awe wa kijani au rangi nyingine yoyoteCobra sio koboko, ni aina mbili za nyoka tofauti. Cobra nimeshuhudia Mwaka huu mwezi January tulimuua baada ya kuingia kwenye zone yake pasipo kujiua akatuletea utata tukapambana naye.
Cobra anajitanua shingo yake hasa anapokuwa ameudhika.
Koboko (Black/Green mamba) sijawahi kumuona kwa macho yangu ila nimehadithiwa na nimemsikia hasa nyakati za usiku akiwa anawika
Duh watu mna makasiriko ya bure sanaKama unaogopa kaa kimya unachafua uzi kwa udangaji wako
Ni kweli kabisa nilipuuzia kizembe ila ni kutokujua tuu.Ulifanya uzembe mkubwa sana yaani kupuuzia, huyo ni Kobra moja kwa moja
Umekurupuka kama jina lako mkuu. Sijadanganya ni kweli ilitokea january hii. Tena ni Dar mbezi mwisho huko kuna nyoka wengi sana nina bahati tuu sikuwahi kuona kwa macho ila wenyeji wanakutana nao kila siku na wamezoea.Kama unaogopa kaa kimya unachafua uzi kwa udangaji wako
Hahahaa yaani mpaka nimemshangaaDuh watu mna makasiriko ya bure sana
Stress zipo tuchukue hatua,, nyuzi za leo ni ukimwi na nyoka ujikute vyote vimekujeruhi kila anaecheka anakuwa mbayaHahahaa yaani mpaka nimemshangaa
Hahahaa yaani leo nyuzi trending ni hizi, Ukimwi na nyoka hata mimi nazunguka humo humo toka mchanaStress zipo tuchukue hatua,, nyuzi za leo ni ukimwi na nyoka ujikute vyote vimekujeruhi kila anaecheka anakuwa mbaya



.Pole Sana mkuu.Chatu alitaka kunimeza.Lakini kwa vile hii hadithi nimeisimulia mara kadhaa Facebook na wapi,sitaki kuwaboa watu.
Lakini huyu chatu nilikuwa sijui kama ni chatu. Nilidhani ni oversized cobra.
We unasema cobra alikuhurumia. Hayo ndiyo mawazo yangu pia. Nilifanikiwa kumtoroka yule chatu,au alinihurumia?
Siku hiyo chatu alipomitokea ni siku ambayo Kagame alikuja Dar kumuona Kikwete,siku hiyo hiyo.
Watoto wa kishua hao,nyoka wanawaona kwenye channel ya Nat Geo wild.Mbezi beach moja hii. Hata ukiambiwa Bongo kuna vinyonga utabisha.
Sana yaaniJamaa alikufa kikatili Sana.
Imagine mtu unapark gadi pembeni Kisha uende ukajisaidie huko unakutana na mziki wa chatu anakumeza!! Lilikuwa tukio la kusikitisha Sana.