Umenioa nije kwako kula na kulala?

Umenioa nije kwako kula na kulala?

Sa ingine twaenda kufanya overtime, au kukutana na wadau kupata tips za kutafuta pesa kihalali, au labda kupata ulabu kutuliza kichwa maana kutafuta wiki nzima si mchezo mama, pole, tuvumiliane, ila mbona weekend twawapa quality wewe na watoto, be tolerant and understanding mama..
 
Ila ukikaa bar kama boya ndio haudhaliliki? Hivi tafsiri yenu ya kudhalilika inatokea sayari gani!!! Sasa huwa mnaoa ili iweje!! Si mkaage hivyo hivyo ili uwe huru zaidi, hata ukiamua kukesha bar haudhaliliki.
Point...Mim huwa nashangaa mwanaume anaoa then hatulii nyumbani...Wangekuwa wanajua raha ya kutooa wasingethubutu kuoa..Huwa wanajua ndoa ni furaha
 
Hivi nyinyi makaka ambao weekend mnafikiria kufanya shopping kujaza fridge na kuweka luku nyumbani baada ya hapo mnapotea kurudi saa nane usiku. Hivi unafikiri kwetu sikuwa ninakula au mzazi wangu wangu alishindwa kununua luku?

Weekend ndiyo muda wa kuongea na wewe. Monday to Friday unawahi kazini acha J'mosi nikupikie breakfast tuongee, ikiwezekana basi kufanya shopping wakati ninasafisha nyumba tule pamoja then unaweza kuwa na masaa mawili matatu na marafiki zako lakini unawahi kurudi nyumbani.

Kama unaenjoy sana company za marafiki mpaka saa nane usiku basi hukuwa tayari kuoa.
Mh, mbona kama sijaelewa
 
Vijana wengi wanaoa wakati wakiwa hawajajiandaa kisaikolojia kuwa wanandoa.

Haiwezekani mwanandoa urudi nyumbani Saa nane....

Ukishaoa unapaswa kubadili aina ya Maisha uliyokuwa unaishi kabla ya ndoa
 
ukishinda nyumbani sana mwisho wake utaanza kusugulishwa masufuria na steel wire uonekane mme bwege
Nilivyomuelewa sio kushinda nyumbani..... Swala ni kurudi nyumbani saa nane Usiku
 
Umeowa ila bado unaishi maisha ya u-bacholor,, kuna aina ya kazi ni full tym unakuwa busy bt smtyms jiibe hata 3hrs ukae na mkeo, apart from mahitaji mengne unayompa muda wako pia anauhitaji,, wanaume tubadilike tulioko kweny ndoa, na mji-tune mnaotarajia kuingia kweny ndoa. Unapotaka kuoa/kuolewa means umeamua kuuza sehemu ya uhuru wako.
Well said Kinehe
 
Siku zote kwenye mahusiano yoyote ya Kimapenzi aama kindoa ni lazima kuwe na makubaliano na mipaka ambayo kila mmoja anatakiwa kuheshimu. Lazima Mpange muda wa kushinda na hata kama kutoka basi mtoke wote. Muweke makubaliano kuwa siku fulani ni lazima tushinde wote nyumbani na tupange na kuzungumza kuhusu Maisha Yetu.

Ni lazima kila mmoja aheshimu hilo na kulikubali hilo. Lakini bila makubaliano kila siku mtaumia ba kuumizana. Pasipo na maelewano basi hapatakuwepo na Mahusiano Thabiti.

Kwangu Mimi simu yangu ni Tatizo kwa kuwa Muda mwingi lazima niwaze kuandika Riwaya. Nawaza kesho niandike nini ama leo nifanyeje. Nina watu ambao hulipia Riwaya zangu kisha kutumiwa. Sasa Tukiwa pamoja ni lazima nikutaarifu hilo. Na nikikutaarifu Basi uwe Tayari Kunielewa. Lakini yote kwa Yote napenda sana kukaa Sehemu ama kushinda ndani na mpenzi Wangu. WANAWAKE MKIPUNGUZA MDOMO KILA KITU KINAWEZEKANA. TATIZO MNAPENDA KUONEKANA MKO JUU
Amen, mkeo/mpenzi wako na akuelewe kwa kweli. Umeongea jambo la msingi, kukubaliana juu ya jambo fulani lifanyikeje, na kila mtu aheshimu makubaliano, ukamaliza na wanawake tuache midomo mirefu......
Mkuu naomba niwe nakutag kwenye uzi wowote unaohusu mahusiano.
 
Amen, mkeo/mpenzi wako na akuelewe kwa kweli. Umeongea jambo la msingi, kukubaliana juu ya jambo fulani lifanyikeje, na kila mtu aheshimu makubaliano, ukamaliza na wanawake tuache midomo mirefu......
Mkuu naomba niwe nakutag kwenye uzi wowote unaohusu mahusiano.
Karibu sana.. Zamani nilikuwa mtu sahihi hapa jukwaani sema mambo mengi ndio maana tunapotea. Nitag tu haina tabu
 
Back
Top Bottom