Tulimumu
JF-Expert Member
- Mar 11, 2013
- 14,395
- 13,266
Sayansi inakua mkuu, zamani kidogo tulizoea simu ya waya hatukuamini kama mtu anaweza kuwa na kadude kadogo akaongea popote na wakati wowote dunia nzima. Tulikuwa tunasikia zile za upepo za viwanja vya ndege. Sasa hivi kuna ndege zinakwenda bila rubani na wameshagundua gari linalokwenda bila dereva. Angalia matangazo ya TV. Mtu yuko maelfu ya kilomita toka ulipo lakini unamuona na kinachotendeka wakati huo huo. Mkutano unaweza kufanyika Arusha lakini wahudhuriaji wakawa wengine Marekani, Uingereza au Ufaransa na wakawa wote wanajadiliana kama vile wapo ukumbi mmoja -video conference. Umeme wa sola nao ni sawa na kusema ni wireless power. Itafika wakati tutaona usambazaji wa umeme bila nyaya kama sio kizazi chetu basi kijachoUMEME KUWA WIRELESS HAIWEZEKANI KAMWE NI SAWA NA KUSEMA IVUMBULIWE WELDING MACHINE KWA AJILi YA KUUNGIA MBAO