Umeme wa 'wireless' kuiangamiza TANESCO!

Umeme wa 'wireless' kuiangamiza TANESCO!

"imposible"haiwezekani kwa umeme!

Mkuu hata kwa sayansi ya darasa la saba tu unaweza kugundua kuwa haiwezekani umeme kuwa wireless.

Haiwezekani kusafirisha nguvu ya umeme hewani kama radi, maana sio salama.

Ni ngumu sana umeme kuwa wireless, Electric charge lazima zisafiri kwenye kitu ambacho kinapitisha hizo charge, Hewa hutumika kama kikinzani (resistance) tena ni resistance kubwa sana, unapokuwa na gap dogo tu la kama 0.1mm linatosha sana kukata umeme hasa huu umeme mdogo, kwa hiyo unapokuwa na gap la kama 5km kutoka kituo kimoja hadi kingine ukinzani wake ni balaa na kama kuna nguvu ya umeme itapenya hapo maana yake viumbe hai vilivyopo katikati ya hivyo vituo vitakufa vyote maana haviwezi kuhimili hiyo nguvu.

Haiwezekani.

practically impossible,,, acha kugoogle na kupaste mambo ya "yahoo answers" bichwa lako.

noooo haiwezekannnn


Kasomeni mtu mmoja anaitwas Tesla, Miaka ya 20 alitoa wazo la Global wireless electricity,akapeleka hilo wazo lake kwa mdhamini wake,Rockafella family,wakamuuliza where do we put meters,akawaambia there is no need of meters,it is wireless,wakamuondolea ufadhili na mradi ukafa maana hao kina Roka wao ni hela tu,jambo lolote linaloonekana kutowafaidisha hawalitaki.

Kwa hiyo usibishe jambo usilolijua,ni dalili za ujinga.
 
Kasomeni mtu mmoja anaitwas Tesla, Miaka ya 20 alitoa wazo la Global wireless electricity,akapeleka hilo wazo lake kwa mdhamini wake,Rockafella family,wakamuuliza where do we put meters,akawaambia there is no need of meters,it is wireless,wakamuondolea ufadhili na mradi ukafa maana hao kina Roka wao ni hela tu,jambo lolote linaloonekana kutowafaidisha hawalitaki.

Kwa hiyo usibishe jambo usilolijua,ni dalili za ujinga.

Mkuu usitumie nguvu nyingi sana kuwaita watu wajinga, Huyo Tesla unayemsema kafanya hiyo project toka 1899 hadi leo haijawa Implemented kwa hiyo unataka kusema tatizo bado ni hela tu? zaidi ya miaka 100 imepita.

Unafikiri ni kwa nini Transmission kwenye Telecommunication kwa kutumia Satellite pamoja na Microwave siku hizi inakuwa replaced na Fibre Cable?
 
ndani ya miaka 5 mpaka 10 tutakuwa na umeme wa wireless, kuna vifaa tayari vitaingia sokoni mwaka huu na mwaka kesho ambavyo vinatumia umeme wa wireless ndani ya nyumba. Mfano kama charger ya simu hautahitaji cable bali unachomeka charger yako kwenye umeme then ndani ya nyumba yako unaweza kucharge simu regardless upo wapi kwani haiitaji wire.

Kwa large scale hasa umeme wa msongo mkubwa tayari wameshaproove inawezekana wanachofanyia kazi sasa ni safety kwa watu. Hatuna muda mrefu hatutakuwa na high tension cables allover our heads maana transmission itakuwa wireless.

Cha muhimu ni namna gani ya kuondokana na monopoly ya TANESCO kwa maana ya kupata vyanzo, mifumo, taasisi na usambazaji mbadala kwani tunapotafuta suluhisho la nishati hapa TZ mindsets ziko centralized kwa TANESCO tu.
 
Inawezekana kabisa maana hata mawimbi ya simu ni umeme.
 
"imposible"haiwezekani kwa umeme!
That's what I am thinking if it's possible. Wireless kwa umeme, Hapana aisee. Mawimbi/ waves zenye umeme mdogo sana ndio waweza kusafirishwa kwa njia ya wireless na sii huu wa more than 250 voltage. Haya ngoja tuone maana Kama hii technology ipo basi hizo nchi za ulimwengu wa kwanza wangekuwa wameshaanza kutumia kitambo kabla ya sisi huku.
Je kuna nchi ambayo wameshaapply hii technology?
 
Mimi naamini inawezekana hapa duniani kisichowezekana ni kifo tu,nadharia yangu ni kuwa huo umeme unaweza ukafanywa kwa kuwa coded kwenye smartcard na kukawepo na kitu kingine utakachinunua na kukiweka hapo home ambacho ktatoa umeme kwa kutumia smartcad JUST THINKING ALOUD AND OUT OF THE BOX
 
Kama mawasilano ya simu yangeendelea kutumia miwaya ya kwenye nguzo basi ni dhahiri kwamba TTCL ingeendelea kuwa-baka waTZ hadi leo hii, ila tu kilichowaokoa ni teknolojia ya wireless communication iliyoleta upinzani kwa kibudu TTCL.

Sasa basi, hivi karibuni wana-sayansi wanatarajia kuzindua umeme wa wireless ambapo huhuitaji wire kusafirisha umeme toka kituo cha kufua umeme hadi nyumbani kwako, kuanzishwa kwa hii kitu kutasababisha TANESCO iji-bake yenyewe hadi kufa!

Ni kweli na inawezekana.

Someni hapa --> Wireless Electricity Is Here (Seriously) | Fast Company | Business + Innovation
 
Cha muhimu ni namna gani ya kuondokana na monopoly ya TANESCO kwa maana ya kupata vyanzo, mifumo, taasisi na usambazaji mbadala kwani tunapotafuta suluhisho la nishati hapa TZ mindsets ziko centralized kwa TANESCO tu.

Mkuu sidhani kama upo sahihi sana...hii kasumba kua Tanesco ina monopoly kiivo sio kweli...sidhani kama kuna new utility company mpya imekuja kuomba leseni Ewura ikanyimwa...sidhani

On top of it all,Atumas walipewa madhan Mtwara na Rukwa wamefeli totally...sio kweli kuna monopoly hiyo kiivo...

Biashara ya electricity ni hasara tupu,hasa kwenye distribution na hata transmission...ndio maana watu binafsi wamejikita kufanya generation wamuuzie Tanesco ndio kwenye walao faida...yeye tanesco auze rejareja kwa wananchi ambayo ni headache kupita maelezo
 
leo wamegundua wireless charger,jiulize miaka 70 ijayo hiyo tech itakuwa imeimprove aje.
 
Mkuu unadhani Tanesco wamelala?Wanajua trend inaenda wapi way long before other normal Tanzanians see it...wana branch inayoshughulikia renewable energy as a whole na sio vipengele pengele...na naskia ina grow as fast

Corruption TANESCO sucks. Consumers country wide hawana imani na TANESCO. Across border Kenya power are performing wonders. Like concrete power poles hadi vijijini nimeshuhudia , 30 percent power cost reduction by december 2014!
 
hivi umeme jua unaodakwa na solar panels sio wirelss??:shock:


Umeme hapo ni ngumu aiseee.

Haiwezekani kusafirisha nguvu ya umeme hewani kama radi, maana sio salama.

Kila kitu kinaweza kuwa moderated na kuwa safe (waulize mods wanajua hili)

Mkuu ungesoma vizuri post yangu wala hata usingeniquote, nimesema sijawahi kuziona hizo charger sijasema kwamba hazipo, unaposema kitu hujawahi kukiona haina maana ya kwamba hakipo.
 
huo ugunduzi unawezekana,Kama mcharo anavyokula nyama kila siku kwa kukopa kwenye simu.
 
Mbona watu wanabisha kwa nguvu sana? Walau mtu aseme kwa sasa haipo ila sio HAIWEZEKANI. Kama umepitia physics huwezi kusema haiwezekani. Mbona wireless zote ni kama haziwezekani lakini zipo? Jiulize useme Hello halafu sauti ipite hewani mtu akusikie marekani! watu wacheze mpira brazil halafu picha zipite hewani uwaone hapa bongo! Come on ni sayansi tu ile picha/sauti/umeme unabadilishwa kutoka mfumo mmoja kwenda mwingine basi! Energy can neither be created nor destroyed but...
 
Back
Top Bottom