Umeme na Nishati: Tatizo sugu Tanzania

Je hakuna uwezekano wa kuanzisha micro-hydrosystems kwenye maeneo ambayo yana potential?
 
TATIZO la Wizara, Wakurugenzi na wafanyakazi kwa ujumla katika sekta za umma kama umeme ni kwamba ni mabingwa wa kutumia lakini akili ndogo ya kutafuta na kuingiza mapato.

Ilishawahi kupendekezwa jamani TANESCO igawanywe tena katika sehemu tatu. Na sehemu kubwa zimilikiwe na halmashauri ya wilaya au mkoa kama vitaga uchumi vyao kwa ubia na sekta binafsi.

. Kwanza kuwe na uzalishaji umeme. Hapa umeme utaendelea kuzalishwa na TANESCO kwa kutumia vinu, mbinu na njia ilizonazo sasa pia kuongeza vyanzo vininge. Lakini pia watu binafsi, Ushirika, makampuni, wilaya, mikoa nazo zinaweza kuchangia kuzalisha. Tatizo ni kwamba tumedekeza watu, tarafa, wilaya na mikoa kiasi ambacho kazi ya kuanzisha 'social or community venture' katika nchi hii bado mbichi kwelikweli!
. Pili ni kusmbaza umeme. Kazi ambayo ni ya wholesale na retail. Watu binafsi, ushirka na makampuni yawe huru kusambaza umeme kila kona nchini kwa faida na manufaa ya nchi na wananchi.

. Tatu, ni kuunganisha na kufunga umme. Nayo, again, hii ni kazi ya kina John na Juma, Mwajabu na Salome ama mmoja mmoja au katika ushirika au makampuni.

MAPENDEKEZO haya yamezikwa na serikali.

Hata umuweke gavana Mkuu wa zamani wa BOT pale TANESCO bado kazi kubwa ya jamaa hawa itakuwa ni ULAJI na UINGIZAJI utakuwa ule wa kibabe, kiwiziwizi, kinguvunguvu, lakini sio wa kihaki na ubunifu wa kuzalisha na kuuza bidhaa au huduma bora kwa bei nafuuu lakini ubora uleule!
 
Kuhani

Watu huchukua misimamo mbalimbali, kuna wasio na misimamo, wenye misimamo na kuna wale ambao hawajijui kuwa wana msimamo ama hawana. Kuna wenye uthubutu wa kuchukua hatua mbele zaidi na kuzuia madhara wanayohisi yaweza kutokea kutokana na aina ya msimamo walionao, na kuna wale ambao wanasubiri madhara yatokee halafu waseme 'nilijua tu pataharibika' na kuna wale ambao hata madhara yakitokea hawajali. Hawa ni wenzetu na ni lazima kuwa nao, hatuwezi kuwatenga.
 
Kuhani

Watu huchukua misimamo mbalimbali, kuna wasio na misimamo, wenye misimamo na kuna wale ambao hawajijui kuwa wana msimamo ama hawana. Kuna wenye uthubutu wa kuchukua hatua mbele zaidi na kuzuia madhara wanayohisi yaweza kutokea kutokana na aina ya msimamo walionao, na kuna wale ambao wanasubiri madhara yatokee halafu waseme 'nilijua tu pataharibika' na kuna wale ambao hata madhara yakitokea hawajali. Hawa ni wenzetu na ni lazima kuwa nao, hatuwezi kuwatenga.

...sasa Rev. Kishoka yupo ktk kundi gani?? mie nahisi yupo ktk hilo kundi la "nilijua tu pataharibika"

...usitolee sana macho haya mambo, ningekuwa mwandishi ningekupa lecture, lakini kwa bahati mbaya mie ni mtu wa domo zaidi kuliko kalamu....eazy now.
 
wale mafundi vibatari wataupgrade na kuuza zaidi. Wataanza kutengeneza majeri ken ya kumwagilia badala ya kutengeneza vibatari; hii itawaongezea kipato kwani jeri keni moja bei yake ni juu kuliko ya kibatari. Kumbuka unaweza kukaa na kibatari miaka mitano bila kununua kingine (kinawekwa pale kumulika tu-hakipati mikiki). Hata hivyo umeme utawasaidia kufanya kazi kwa urahisi na kutoa products zenye ubora utakaokidhi masoko nje ya nchi.

...umefikiria sana!! hahahaha kama ni vipodozi basi umejidodeka..:D
 
...sasa Rev. Kishoka yupo ktk kundi gani?? mie nahisi yupo ktk hilo kundi la "nilijua tu pataharibika"

...usitolee sana macho haya mambo, ningekuwa mwandishi ningekupa lecture, lakini kwa bahati mbaya mie ni mtu wa domo zaidi kuliko kalamu....eazy now.

Kwani wewe uko kwenye kundi gani?
 
Kwani wewe uko kwenye kundi gani?

kwa sasa mie nipo kwenye kundi la, "wale ambao hata madhara yakitokea hawajali." Vipi unataka nikupe sababu au umeridhika kulijua kundi langu?
 
hivi kukiwa na umeme sasa wale mafundi wa sido wa vibatari (wakina joe the plumber wa kibongo) wakale wapi? acheni nyinyi maneno yenu.........kukosekana kwa umeme ni industry flani na kupatikana kwake kunapunguza ajira!!

hizo ni two cents zangu, in a nutshell.....

Jibu ni Innovation.

Maneno yako yamenikumbusha yule kibosile aliyeamuru na kupiga marufuku matumizi ya simu za Internet (kupiga simu ng'ambo) kwa sababu TTCL ilikuwa haifanyi mauzo tena!
 
Kuhani,

On a serious note though, hivi umeona kuwa natumia mgongo wa Nyani kutukana Watanzania na kuona sina kende kutukana kwa mdomo wangu mwenyewe?

Si wewe uliyeshangilia nilipomsiliba FMES kwenye hoja moja mpaka ukatoa tuzo ya Mtu mwenye Makende ya Chuma?

Umepitia Screw Muungwana? Je CCM adui wa Maendeleo nako huko nimekosa mfupa?

Sasa kwenye hili la Nishati na kutumia maneno ya Nyani "Ndivyo Tulivyo" nimekosea nini kueleza ukweli kuwa Serikali yetu na watendaji wake ni wavivu wa kufikiri, kupanga mambo na kuingia gharama?

Wewe ni mchumi, tupe basi zako nasaha kuwa tufanyeje zaidi ya kupembua utata wa tungo zangu au wasifu wangu.

Kusema sisi Miafrika ni Ndivyo Tulivyo sio tusi. Ni ukweli na watu wanajua kuwa ndio ukweli..and just like the old adage goes...truth hurts.

Wengi wenu hapa mna majina ya ki Anglo Saxon, mna practise imani tulizoletewa na wazungu, na mengine mengi. Hivi mnataka kunambia bila wazungu kuja kututawala na hatimaye kuwasomesha akina Nyerere leo mngekuwa wapi? Elimu tunayopata sasa ni ya kizungu. Hivi kabla ya kuja wakoloni Tanzania kulikuwa taasisi gani ya elimu ya juu au ya kati?

Huyo Obama mnaemshangilia ushindi wake bila wazungu kumpigia kura asingekuwa raisi mteule leo hii. Au mmesahau hilo? Na wazungu wamempigia kura ku prove pointi ya kuwa wengi wao sio wabaguzi.

Listen people, it takes creativity, courage, and ingenuity to progress. How are going to harness our supposedly abundant natural resorces if we lack ingenuity? Even coming up with sound policies requires ingenuity.

Kwa nini Afrika Kusini imeendelea kuliko nchi ingine ya Kiafrika?
 
tatizo la miradi mingi tanzania ni kuweka maslahi binafsi mbele kuliko National interest au tuseme kitu ambacho kitakuwa na faida kiuchumi. Ndio maana utaona leo hii Viongozi wetu wanafurahia umeme wa Vibaba, badala ya kuwa na Grand Project kama atleast kama Kidatu, to cut the story short, mradi wanaotakiwa kuwekeza ni huo wa Stigler, mingine ni hiyo ya upepo, na jua, sasa labda hamna kamisheni ya kutosha ndio maana wanakimbilia miradi ya dharura
 
tatizo la miradi mingi tanzania ni kuweka maslahi binafsi mbele kuliko National interest au tuseme kitu ambacho kitakuwa na faida kiuchumi. Ndio maana utaona leo hii Viongozi wetu wanafurahia umeme wa Vibaba, badala ya kuwa na Grand Project kama atleast kama Kidatu, to cut the story short, mradi wanaotakiwa kuwekeza ni huo wa Stigler, mingine ni hiyo ya upepo, na jua, sasa labda hamna kamisheni ya kutosha ndio maana wanakimbilia miradi ya dharura

It is true, gharama za kuendesha kidatu, mtera, kihansi, nyumba ya mungu hale, na diesel generators huko katika wilaya mbalimbali zaweza kuwa sawa na kuhudumia mradi mmoja mkubwa. Rasilimali za kutuwezesha kupata umeme zipo zimekaliwa. Hatuko cost effective wala hatuna malengo ya muda mrefu.
 
tatizo la miradi mingi tanzania ni kuweka maslahi binafsi mbele kuliko National interest au tuseme kitu ambacho kitakuwa na faida kiuchumi. Ndio maana utaona leo hii Viongozi wetu wanafurahia umeme wa Vibaba, badala ya kuwa na Grand Project kama atleast kama Kidatu, to cut the story short, mradi wanaotakiwa kuwekeza ni huo wa Stigler, mingine ni hiyo ya upepo, na jua, sasa labda hamna kamisheni ya kutosha ndio maana wanakimbilia miradi ya dharura

Kwa hiyo wakifanya hivyo tatizo la umeme kwisha habari yake...?
 
Kusema sisi Miafrika ni Ndivyo Tulivyo sio tusi. Ni ukweli na watu wanajua kuwa ndio ukweli..and just like the old adage goes...truth hurts.............

Lakini Nyani, hawa hawa watanzania wanaonekana kwenye nchi yao hawawezi kufanya kazi au kuengeneza anything productive wakienda kwenye nchi za watu wanasifika kwa ufanyaji kazi na wenyeji wao wanawatumia kuleta maendeleo. Ukichukulia Botswana, Namibia, Rwanda watanzania wengi tu wamezisaidia hizi nchi kusonga mbele.

Mifano mingine ni waliopo/waliokuwepo kwenye mashirika ya kimataifa, kama kina merehemu Balali, wakati wakiwa huko walikuwa ni wafanyakazi wazuri na wenye sifa kibao mpaka kuombwa kuja nyumbani. Mimi nadhani tatizo kubwa la tanzania ni 'system' yetu ya utawala inayojumuisha mambo mengi kama utungaji wa sera na malengo, utekelezaji wake, evaluation & monitoring, uwajibikali wa serikali na kiongozi mmoja mmoja etc...Kwa ujumla sijui nchi kama nchi tunajua tunataka nini na tufikaje huko tunakotaka kwenda.
 
Lakini Nyani, hawa hawa watanzania wanaonekana kwenye nchi yao hawawezi kufanya kazi au kuengeneza anything productive wakienda kwenye nchi za watu wanasifika kwa ufanyaji kazi na wenyeji wao wanawatumia kuleta maendeleo. Ukichukulia Botswana, Namibia, Rwanda watanzania wengi tu wamezisaidia hizi nchi kusonga mbele.

Mifano mingine ni waliopo/waliokuwepo kwenye mashirika ya kimataifa, kama kina merehemu Balali, wakati wakiwa huko walikuwa ni wafanyakazi wazuri na wenye sifa kibao mpaka kuombwa kuja nyumbani. Mimi nadhani tatizo kubwa la tanzania ni 'system' yetu ya utawala inayojumuisha mambo mengi kama utungaji wa sera na malengo, utekelezaji wake, evaluation & monitoring, uwajibikali wa serikali na kiongozi mmoja mmoja etc...Kwa ujumla sijui nchi kama nchi tunajua tunataka nini na tufikaje huko tunakotaka kwenda.

Huko kwenye nchi za watu kila kitu kiko tayari na kilitengenezwa ama kuundwa na wenye nchi yao. Sisi tukienda huko tunavikuta tu. Sasa kama unasema "system" yetu ni mbovu na tunajua kuwa ni mbovu kwa nini sasa tusitengeneze inayofaa kama tunaweza?

Hao kina Balali wanafanya kazi huko majuu kwa kusimamiwa na wazungu na wanafanyia kazi makampuni na mashirika yaliyoanzishwa na wazungu. Kwa hiyo hoja yako iko nullified...
 
Huko kwenye nchi za watu kila kitu kiko tayari na kilitengenezwa ama kuundwa na wenye nchi yao. Sisi tukienda huko tunavikuta tu. Sasa kama unasema "system" yetu ni mbovu na tunajua kuwa ni mbovu kwa nini sasa tusitengeneze inayofaa kama tunaweza?

Hao kina Balali wanafanya kazi huko majuu kwa kusimamiwa na wazungu na wanafanyia kazi makampuni na mashirika yaliyoanzishwa na wazungu. Kwa hiyo hoja yako iko nullified...

Ndio maana nimetolea mfano nchi kama Rwanda(recent example), Botswana, Namibia .....ambazo ni za waafrika wenzetu lakini walikaa chini wakaamua wapi wanataka kwenda na watafikaje. Mkishajiuliza maswali hayo mtajua kuwa kama ni kuwa na viwanda & uwekezaji wa nguvu tunahitaji umeme wa uhakika na wa bei rahisi kama moja ya goal, issue itakuwa tutaupataje? then utaweka strategy. Baadya ya hapo utaangalia sehemu zote muhimu na mwisho kutokana na uwezo utaamua kuanza lipi na lipi lifuate.
 
Ndio maana nimetolea mfano nchi kama Rwanda(recent example), Botswana, Namibia .....ambazo ni za waafrika wenzetu lakini walikaa chini wakaamua wapi wanataka kwenda na watafikaje. Mkishajiuliza maswali hayo mtajua kuwa kama ni kuwa na viwanda & uwekezaji wa nguvu tunahitaji umeme wa uhakika na wa bei rahisi kama moja ya goal, issue itakuwa tutaupataje? then utaweka strategy. Baadya ya hapo utaangalia sehemu zote muhimu na mwisho kutokana na uwezo utaamua kuanza lipi na lipi lifuate.

Hao nao hawana tofauti kubwa na sisi. Wote ni ulimwengu wa tatu tu
 
Kwa hiyo wakifanya hivyo tatizo la umeme kwisha habari yake...?

Yes NN, of course sio kuwekeza tu, huo ni mwanzo, kinacho fuata baada ya hapo ni maintenance policy, ya hiyo miradi, bila kuacha mbali review ya mara kwa mara uki-focus sema ten years tutakuwa wapi, ili kama kunakuwa na tatizo unaanza kuchukua hatua zifaazo mapema, lakini kama mawazo yangu yana mapungufu, unaweza kuongezea, maana waswahili wanasema akili ni nywele? na kila mtu anazake.
 
Back
Top Bottom