Umekumbwa na nini ex -wangu

Umekumbwa na nini ex -wangu

Sawa ila hapo kwenye kuacha baiskeli na kujitupa na kugaragara imeleta ukakasi kuhusiana na afya na usalama wa abiria aliepanda hiyo bicycle baada ya kuachwa ghafla na dereva

Kama ingekupendeza ni vyema ungeanzisha uzi mpya unaoelezea hali ya abiria baada ya hili tukio lenu😁😁
hahaaa ww unataka storii iendelee
 
Wiki hii nilipata safari ya kikazi mkoani kwetu Iringa -mafinga.
Baada ya kuisha kwa ukaguzi na kuandikia ripoti ya kazi zangu nikaamua kujisogeza nyumbani
sababu sijaenda kuwasalimu miaka kadhaa sasa tangu nipate ajira.

basi ndugu zangu nilifurahi sana kufika home, nikasalimu wazazi ndugu, jamaa na marafiki. ilipofika mida ya mchana nikawa nimetoka kwenda uwanjani kutafuta network(mtandao).

Kila napopiga hatua kuelekea mbele nikawa namuona mdada ambaye sura yake sio ngeni machoni pangu anaendesha baiskeli akiwa kambeba mama mtu mzima ambaye anakuja usawa wangu .

doh! vile amekaribia kumbe ni ex wangu ,yule aliye utesa moyo wangu . aliye nisulubu nikaona dunia chungu mpaka nikashindwa kufanya mtihani wa kidato cha nne kwa mwaka huo.

Nikaita jina lake mara mbili akasimama, nikamsalimu uhali gani ? ulikumbwa na nini? ajabu sana ex wangu katika maongezi ya dakika tano bado alishindwa kunifahamu mi ninani? mpaka pale nilipo mwambia mimi ni fulani umenisahau.!!

Ex wangu alishindwa kujizuia akaanza kulia. Hali iliyo nifanya namimi nianze kujikaza kiume kutoa chozi sababu ex wangu kapoteza nuru ,tabasamu na muonekano, jamani Huyu mwanamke nilimpenda sana.

Nilipo muuliza ulikua wapi kipindi chote , katikati ya mapenzi yetu uliondoka bila hata kuniaga nilikukosea nini Akaniambia Mama alimpeleka Dar kwa wajomba zake kusoma!!

ebu funguka hapa chini ex wako yuko wapi, umewahi tenga muda kujua anajihusisha na nini kwasasa?
Ma ex wangu wote wako vizuri kuliko nilivyo waacha namahukuru Mungu.. wote nawaombea mafanikio kama Mimi[emoji1374]
 
Ex Sio mke kwann usumbukie maisha yake kila mtu na maisha yake.
Alikukataa ukafeli pepa Mungu alikua na makusudi yake.
Wapo watu huja kwenye maisha yetu ili kutuharibia kwa wakati huo lakini kwa faida ya mbeleni
 
Wiki hii nilipata safari ya kikazi mkoani kwetu Iringa -mafinga.
Baada ya kuisha kwa ukaguzi na kuandikia ripoti ya kazi zangu nikaamua kujisogeza nyumbani
sababu sijaenda kuwasalimu miaka kadhaa sasa tangu nipate ajira.

basi ndugu zangu nilifurahi sana kufika home, nikasalimu wazazi ndugu, jamaa na marafiki. ilipofika mida ya mchana nikawa nimetoka kwenda uwanjani kutafuta network(mtandao).

Kila napopiga hatua kuelekea mbele nikawa namuona mdada ambaye sura yake sio ngeni machoni pangu anaendesha baiskeli akiwa kambeba mama mtu mzima ambaye anakuja usawa wangu .

doh! vile amekaribia kumbe ni ex wangu ,yule aliye utesa moyo wangu . aliye nisulubu nikaona dunia chungu mpaka nikashindwa kufanya mtihani wa kidato cha nne kwa mwaka huo.

Nikaita jina lake mara mbili akasimama, nikamsalimu uhali gani ? ulikumbwa na nini? ajabu sana ex wangu katika maongezi ya dakika tano bado alishindwa kunifahamu mi ninani? mpaka pale nilipo mwambia mimi ni fulani umenisahau.!!

Ex wangu alishindwa kujizuia akaanza kulia. Hali iliyo nifanya namimi nianze kujikaza kiume kutoa chozi sababu ex wangu kapoteza nuru ,tabasamu na muonekano, jamani Huyu mwanamke nilimpenda sana.

Nilipo muuliza ulikua wapi kipindi chote , katikati ya mapenzi yetu uliondoka bila hata kuniaga nilikukosea nini Akaniambia Mama alimpeleka Dar kwa wajomba zake kusoma!!

ebu funguka hapa chini ex wako yuko wapi, umewahi tenga muda kujua anajihusisha na nini kwasasa?
umeonesha weakness.mwanamke anapolia mwanaume hupaswi kuunga tela nawe eti
unaanza kulia.inatakiwa uwe jasiri wewe ndo umbembeleze.
 
Ex wangu aliolewa na rafiki yangu baada ya Mimi kwenda kusoma mjini, sasa hivi ni mama wa watoto saba na ana wajukuu wa wawili, Mimi ndo kwanza nina watoto wawili wanasoma nilipo kwenda kusalimia ndugu zangu nilonana naye na akaniambia mzee Ngonyani haya maisha ni fumbo, isingekuwa huyo mshenzi yaani mumewe tungekuwa wote mjini. Nilimjibu kila kitu Mungu ndiye anayepanga. ila amechakaaaa harafu Kawa mzee kuliko mimi. Hata hivyo nilimwacha na chochote
 
Sio kila x lazima achakae muulizeni steve Nyerere na Welu alipomuacha akajua atafubaa mtoto akazidi kung'ara kuona vile steve acha roho imuume ikafikia hatua akijua unataka umpe dili Welu anakuja hata na magoti usiku wa manane na majungu kibaoo eti usimpe kazi yule atakuharibia blah blah blahh😂😂
 
Beb aliniambia juzi kati alikutana na X wake huko Iringa, kumbe ndio wewe...🤔
 
nimekuta ex wangu kachakaa sio mchezo
Sijawahi sikia mtu anasema amekutana na ex wake amenawiri , amaeng'aa au ametoboa ...yaani maEx wote wanakuwaga wameparanganyika eti...ndio kanuni ya kumuongelea Ex labda ... Labda nione humu Leo ex akisifiwa.
 
Back
Top Bottom