Uliza ujibiwe kuhusu madini, gesi na mafuta

Gesi ya helium kwa volume iliyoko hata Tanzania inawezekana kujengewa kiwanda na ikauzwa baada ya kuwa processed au inauzwaga hivyo hivyo ikiwa raw??

Vipi kuhusu dhahabu, kwa nini dhahabu kwenye machimbo madogo huwa inafumuka kwa msimu bila kutumia nguvu yoyote kuichimba, na baadaye kupotea kabisa.??
Hili jambo la dhahabu kufumuka na baadaye kupotea ni la kitaalamu au ni mambo ya kishirikina??
 
Ni vitu gani hasa vinasababisha mafuta kujitengeneza huko chini ya ardhi? na ni kwa nini kuna baadhi ya maeneo mafuta yako kwa wingi sana tofauti na pengine? mfano huko uarabuni toka enzi na enzi uchumi wao ni mafuta tu..itatokea hizo reserves ziishe?

Huku kwetu je kiasi kilichogundulika kinaweza kufikia kiwango walicho nacho? Kuna tofauti ya mafuta yanayopatikana baharini na yale yanayopatikana kwenye maziwa? Inawezekana kupata mafuta au gas eneo la nchi kavu?

Mfano pale Ruvu naona kuna shughuli inayoendelea nikaambiwa ni utafiti wa mafuta na gas? kuna viashiria gani vinavyoonesha kuwa hapa kuna mafuta na gas?
 
Kwanini Gas yetu asilia haiwekwi wazi kwamba twaweza ku i refine na tukapata gesi ya jikoni na bidhaa nyingine? Petroleum?
 
Kwanini Gas yetu asilia haiwekwi wazi kwamba twaweza ku i refine na tukapata gesi ya jikoni na bidhaa nyingine? Petroleum?
mkuu kujenga huo mtambo ya kurifine natural gas ikatumika majumbani ni gharama sana. Imagine plant za madimba na songosongo kwa kuprocess gas cost ni almost 2.5Trilion wakati cost ya LNG plant zidisha hiyo cost mara 10
 
Ni vitu gani hasa vinasababisha mafuta kujitengeneza huko chini ya ardhi? na ni kwa nini kuna baadhi ya maeneo mafuta yako kwa wingi sana tofauti na pengine? mfano huko uarabuni toka enzi na enzi uchumi wao ni mafuta tu..itatokea hizo reserves ziishe? huku kwetu je kiasi kilichogundulika kinaweza kufikia kiwango walicho nacho? Kuna tofauti ya mafuta yanayopatikana baharini na yale yanayopatikana kwenye maziwa? Inawezekana kupata mafuta au gas eneo la nchi kavu? mfano pale Ruvu naona kuna shughuli inayoendelea nikaambiwa ni utafiti wa mafuta na gas? kuna viashiria gani vinavyoonesha kuwa hapa kuna mafuta na gas?

Naweza kukujibu kama ifuatavyo

1. Ni vitu gani hasa vinasababisha mafuta kujitengeneza huko chini ya ardhi?

Jibu

Mafuta hutengenezwa kutokana na mkusanyiko wa masalia ya viumbe hai na mimea ambavyo kwa pamoja hufukiwa na mchanga (sediments) kwa kipindi kirefu sana (millions of years) hasa katika maeneo ya mabonde, maziwa, bahari (basin area), mgandamizo na joto linalotokana na kinakirefu cha mchanga kilichofukia masalia ya viumbe na mimea ndicho kinachopelekea kuzalishwa kwa mafuta, gesi na makaa yam mawe (fossil fuels).

2. Na ni kwa nini kuna baadhi ya maeneo mafuta yako kwa wingi sana tofauti na pengine? mfano huko uarabuni toka enzi na enzi uchumi wao ni mafuta tu.

Jibu

Kiwango cha masalia ya viumbe na mimea kinachofukiwa huchagiza kiasi cha mafuta kitachotengenezwa ingawa kiwango kinaweza kikawa sawa lakin kiasi cha oxygeni kikizidi hupelekea decomposition kuwa kubwa na hivyo kuharibu bond ya hydrogen na carbon ambazo ndizo hupelekea mafuta kutengenezwa.

3. ..itatokea hizo reserves ziishe?

Jibu

Hii ni aina ya nishati ambayo hupungua kadiri unavyo izalisha kwaiyo ukianza kuzalisha lazima itafika siku itaisha

4. huku kwetu je kiasi kilichogundulika kinaweza kufikia kiwango walicho nacho?

Jibu

Huku kwetu mafuta bado hayajagunduliwa ingawa serikali kupitia shirika la maendelea Tanzania (TPDC) zinafanya jitihada yakuendelea kutafuta katika maeneo mbalinmbali nchini

Ni Gesi asilia ndio tumefanikiwa kugundua katika maeneo ya mwambao wa pwani na bahari ya hindi ambayo imefikia kiasi cha 57 Trillion Cubic feet (TCF) (data za mwaka 2016 TPDC) hiki kiasi ni sawa na mapipa ya mafuta (equivalent oil amount in barrel) 9,826,499,031, kiasi hiki cha gesi tuliyo nayo ni asilimia 0.86 ya gesi yote ambayo tayali imeshagunduliwa duniani, bado jitihada zakuitafuta zinaendelea.

5. Kuna tofauti ya mafuta yanayopatikana baharini na yale yanayopatikana kwenye maziwa?

Jibu

Katika maana ya utengenezwaji wake unafanana kote baharini (offshore) na nchi kavu (onshore) kote hutenezwa kwa namna moja kama ilivyo elezwa katika jibu la swali la kwanza, kinachoweza kutofautisha reserve moja na nyingine ni viambata vilivyomo katika mafuta (chemical composition of crude oil or gas).


6. Inawezekana kupata mafuta au gas eneo la nchi kavu? mfano pale Ruvu naona kuna shughuli inayoendelea nikaambiwa ni utafiti wa mafuta na gas?

Jibu

Uwezekano upo kama nilivo eleza katika jibu la swali la kwanza kwa mafuta au gesi vinatengenezwa katika maeneo ya mabonde (basin)ambapo uwezekano wa masalia ya viumbe hai na mimea kufukiwa na mchanga (sediments), kwa hiyo Ruvu ni moja ya mabonde (basin) ndo maana uliona tafiti zinaendelea.

7. kuna viashiria gani vinavyoonesha kuwa hapa kuna mafuta na gas?

Jibu

Namna raisi yakujua kama eneo fulan kuna gesi au mafuta, unaweza kuona gas/oil seep hii inamaana mafuta au gesi ambayo imepenya miamba nakutokezea juu ya ardhi pasipo kuchibwa kunabaadhi ya maeneo Tanzania kuna izi seeps Kunasehemu inaitwa wingayongo maeneo ya rufiji na sehemu fulani kule mtwara karibu na mnazibay.

Zipo namna nyingine nyingi zakitaalammu zinazotumika kutafuta mafuta au gesi lakin namna pekee ambayo unaweza kujua kama kweli kuna mafuta au gesi nikuchimba kisima nakufanya upembuzi yakinifu.
 
Kwanini Gas yetu asilia haiwekwi wazi kwamba twaweza ku i refine na tukapata gesi ya jikoni na bidhaa nyingine? Petroleum?

Mkuu, kuhusu kurifine (processing of natural gas) tayari imeshafanyika na tayari serikali imefanya jitihada zakuifikisha Dar es salaam kilicho baki nikusambaza mabomba katika mitaa na nyumba za watu tayari kwa matumizi kwa kuwa hakuna namna nyingine raisi yakuweza kuifikisha majumbani bila kusambaza mabomba, rabda tatizo ni funds na ugumu wakupitisha mabomba katika mitaa yetu ambayo haijapangwa vizuri kwa kuwa gesi asili is very sensitive case kwenye maswala ya usalama, Kuhusu bidhaa nyingine ambozo zinatokana na gesi, mojawapo ambayo tunanufaika nayo sasa ni umeme natayari kunamchakato wakuanzisha kiwanda cha mbolea ambacho pia kitatumia gesi kama raw material
 
1: Zamani enzi za mababu zetu walikuwa wanaokota dhahabu juu ya ardhi kwanini isiwe sasa au madini yaliyopo juu ya ardhi yaliisha na kama yaliisha ilikuwaje wakae juu ya ardhi kipindi hicho?

2:Mafuta ni bidhaa muhimu sana kwa dunia ya sasa ni vipi mafuta hutokea?

3: Nasikia Mchanga wa Madini una tabia ya kuzaliana na baadae kuwa madini je kuna ukweli juu ya hili na kama ni kweli kwanini?

4:Kuna aina ngapi za Madini duniani na ni madini gani ni ghali kuliko yote.

5:Je hapa duniani kuna (nchi) ukanda ambao hauna madini yeyote yale ?.

6:Je Kuna Mahusiano gani kati ya madini na Miamba?

7: Gesi na Mafuta hutofautiana nini?

8: Kwanini Nchi nyingi za Uarabuni zina Mafuta sana?

9:Kipi kati ya Gesi, Mafuta na Madini kina gharama kubwa katika uzalishaji?.

10:Ni dalili zipi za awali huonekana katika ardhi yenye Madini,Mafuta na Gesi kabla ya utafiti kufanyika(huwa kuna dalili zipi).

11:Naomba kujua hii gasi ya kupikia ina tofauti gani na hii gasi iliyopo hapa Nchini (Mtwara).

12: Mafuta ya Ndege Gari na vyombo vingine huwa yanatofautiana nini?
 
Gesi ya helium kwa volume iliyoko hata Tanzania inawezekana kujengewa kiwanda na ikauzwa baada ya kuwa processed au inauzwaga hivyo hivyo ikiwa raw??

Vipi kuhusu dhahabu, kwa nini dhahabu kwenye machimbo madogo huwa inafumuka kwa msimu bila kutumia nguvu yoyote kuichimba, na baadaye kupotea kabisa.??
Hili jambo la dhahabu kufumuka na baadaye kupotea ni la kitaalamu au ni mambo ya kishirikina??
Bilionea Asigwa.
1 juu ya helium kujenga plant
mpaka sasa kuna maeneo matatu yanayofanyiwa utafiti wa helium(helium exploration) hapa tanzania ambazo miradi hiyo inaendeshwa na kampuni ya HELIUM ONE na kampuni zake tanzu. miradi hiyo inafanyika ZIWA Rukwa, Ziwa Eyasi na Balangida. kwa utafiti wa awali unaonesha helium gasi ipo nyingi lakini hadi sasa hakuna hata mradi mmoja uliofikia hatua ya uchambuzi yakinifu(feasibility study) na kutoa majibu ya kuwa huo mradi unafaida au hamuna. na hadi sasa hakuna leseni hata moja iliyoombwa kwa ajili ya kuchimba helium(ML au SML) isipokuwa kunaleseni za utafiti tu. mwisho wa utafiti ndiyo itatoa majibu ya kuwa processing plant ijengwe hapa au isafilishwe gafi(raw). kwa hiyo ukifika wakati huo tutapata majibu ya swali lako juu ya helium.

2. juu ya dhahabu kwenye machimbo madogo kuwa inafumuka na kukata

kunamchakato wa dhahabu kuingia kwenye mwamba (gold mineralization) hii hatua huingiza dhahabu kwenye mwamba. sasa njisi ilivyo dhahabu haingii kwenye mwamba kwa usawa sehemu zote za mwamba( gold not distributed uniformly in ore body) kutokana na kitu hiki mwamba wa dhahabu huwa kunasehemu nyingine imejikusanya nyingi kuliko sehemu nyingine( some areas are highly gold concetrated or mineralized than other area.) hii kusababisha wachimbaji wadogo kuifumania na hivyo kujipatia mipesa. hii sehemu ya dhahabu nyingi inaweza kuwa imejitokeza hata juu kabisa ya aridhi lakini wakichimba zaidi inapungua wingi. na pia unaweza kuchimba kina kilefu na ukakutana nayo tena kwa wingi au usikutane nayo tena. kuhusu ushilikina huu ni upungufu wa uelewa wa madini. Bilionea madini yote na siyo dhahabu tu hayana uhusiano wa ushilikina.

Kila dini unaloliona lipo kwa mchakato fulani uliojitokeza aridhini na kunataratibu za kulitafiti hadi ukalipata na kulichimba. Lakini ushilikina ni imani na hivyo husaidia kuwapa nguvu wachimbaji kuwa na imani kuwa wanapochimba watapata. na hii unaweza ukakuta mchimbaji ametembea miaka 10 kwa waganga na kila anapopewa dawa anachimba na akikosa anaenda kwa mganga mwingine. kwa kuwa akipewa dawa anaimani na hiyo dawa na anaenda kufanya kazi ya kuchimba kunasiku atakutana na madini na siku hiyo akikutana nayo ataamini mganga wa mwisho aliyempa dawa ni wa ukweri. Lakini ukweri ni kwamba amepata madini kwa sababu alikuwa anachimba na siyo kwa sababu ya dawa. kwa hiyo hakuna dawa inayoweza kuhamisha madini sehemu moja kwenda sehemu nyingine.

BILIONEA KARIBU KWA SWALI LA NYONGEZA KAMA SIJAKUJIBU KWA USAHIHI.
 
1: Zamani enzi za mababu zetu walikuwa wanaokota dhahabu juu ya ardhi kwanini isiwe sasa au madini yaliyopo juu ya ardhi yaliisha na kama yaliisha ilikuwaje wakae juu ya ardhi kipindi hicho?

2:Mafuta ni bidhaa muhimu sana kwa dunia ya sasa ni vipi mafuta hutokea?

3: Nasikia Mchanga wa Madini una tabia ya kuzaliana na baadae kuwa madini je kuna ukweli juu ya hili na kama ni kweli kwanini?

4:Kuna aina ngapi za Madini duniani na ni madini gani ni ghali kuliko yote.

5:Je hapa duniani kuna (nchi) ukanda ambao hauna madini yeyote yale ?.

6:Je Kuna Mahusiano gani kati ya madini na Miamba?

7: Gesi na Mafuta hutofautiana nini?

8: Kwanini Nchi nyingi za Uarabuni zina Mafuta sana?

9:Kipi kati ya Gesi, Mafuta na Madini kina gharama kubwa katika uzalishaji?.

10:Ni dalili zipi za awali huonekana katika ardhi yenye Madini,Mafuta na Gesi kabla ya utafiti kufanyika(huwa kuna dalili zipi).

11:Naomba kujua hii gasi ya kupikia ina tofauti gani na hii gasi iliyopo hapa Nchini (Mtwara).

12: Mafuta ya Ndege Gari na vyombo vingine huwa yanatofautiana nini?

Naweza kujibu kama ifuatavyo Mr Mreno

2:Mafuta ni bidhaa muhimu sana kwa dunia ya sasa ni vipi mafuta hutokea?

Jibu


Mafuta hutengenezwa kutokana na mkusanyiko wa masalia ya viumbe hai na mimea ambavyo kwa pamoja hufukiwa na mchanga (sediments) kwa kipindi kirefu sana (millions of years) hasa katika maeneo ya mabonde, maziwa, bahari (basin area), mgandamizo na joto linalotokana na kinakirefu cha mchanga kilichofukia masalia ya viumbe na mimea ndicho kinachopelekea kuzalishwa kwa mafuta, gesi na makaa yam mawe (fossil fuels).


7.Gesi na Mafuta hutofautiana nini?

Jibu


Gesi na mafuta vyote hutengenezwa katika namna inayofanana kamailivoelezwa katika swali na 2 kinacholeta utofauti ni joto na mkandamizo unaotumika kutengeza,

Mafuta yenyewe hutengezwa katika joto kati ya (65'C na 150'C) joto hili hupatikana kutika kina 2000m mpaka 5500 meter, Joto likizidi 150'C basi hizo organic compounds ambazo zingekuwa mafuta sasa zitakuwa gesi asilia na likizidi 250'C basi izo organic compounds zitabadilika nakuwa graphite. (kumbuka Joto na mgandamizo huongezeka kadiri kina kinavyo ongezeka.

9. Kipi kati ya Gesi, Mafuta na Madini kina gharama kubwa katika uzalishaji?

Jibu

Napenda kuelezea kuhusiana na gaharama za gesi na mafuta pekee.

Kwanza gharama zinaanzia katika utafutaji na badae tutaona katika uzalishaji, ntaelezea katika mukitadha wa kitu kinaitwa oil and natural gas life cycle.

1. Gharama za kupata access (gaining Access)

Hizi ni gharama zitakazo husiana na kupata vibali katika mamlaka mbalimbali lakini pia kupata documents au taarifa za awali (data) kuhusiana na eneo amabalo unapanga kufanya utafiki ( gharama hizi zitategemea sana sheria na aina ya mikataba katika nchi husika lakin wastani ni dola za kimarekani 20 million na hutumia kati ya miaka 0 mpaka 2 kukamilisha taratibu katika kipengele hiki.

2. Gharama ya kufanya utafiti (exploration cost)

Gharama hizi zitahusisha tafti mbalimbali za awali utakazo zifanya kama aerial survey, seismic ( ambazo unaweza kuzifanya kwakutumia meli kama ni baharini au tracks kama ni nchi kavu) lakin pia gharama za kuchimba kisima kama tafiti za awali zitaonesha dalili njema za kuwepo mafuta au gesi na gharama za kufanyia analysis sample mbalimbali ambazo utazitoa kwenye kisima (gharama zake zitategemea eneo unalofanyia utafiti kama ni kinakirefu cha bahari au kifupi au nchi kavu) wastani wa gharama za kuchimba kisima kimoja katika nchi kavu (onshore) ni dola za kimarekani million 1 mpaka million 15 kutokana na urefu na complication za mahari kilipo wakati kuchimba kisima kimoja katika kina kirefu cha bahari (offshore) (1000 meta na kuendelea) ni dollar za marekani kuanzia million 100 nakuendelea ,so hapo utajumlisha na gharama nyingne za tafiti za awali ambazo zitategemeana na watoa huduma. Unaweza tumia miaka 4 au zaidi katika kipindi hiki cha exploration.

3. Gharama za kuchimba visima vingne zaidi kwa ajili yakujiridhisha kiasi kilichopo katika eneo (appraisal phase cost)

Katika hatua hii utalazimika kuingia gharama za kuchimba visima vingine kadhaa kama kisima ulicho chimba awali kimeonesha matumaini ya kuwepo mafuta au gesi, katika hatua hii visima vinaweza kuwa vitatu au zaidi kwa gharama zile zile nilizo zioredhesha katika point no 2, umhimu wa hatua hii nkutaka kujua jumla ya kiasi kilichopo katika eneo lako atachoweza kuzalisha, unaweza tumia miaka 2 au zaidi

4. Gharama za kuandaa miundo mbinu ya uzalishaji

Katika hatua hii sasa utakuwa tayari umejua kama kitaru chako kina mafuta au gesi au vyote kwa pamoja hivyo utatikiwa kuandaa mazingira ya uzalishaji kulingana na aina ya product iliyopo.

Kama ni gesi asilia ndo ipo

Itakulazimu kuandaa mazingira ya uzalishaji kutoka na soko lilipo kwanza itabidi kujenga kisima kiwe nahadhi ya uzalishaji na sio utafiti tena, hapa utaweka mabomba ya kuzalishia kuanzia chini ya kisima mpaka kwene well head na kisha utajenga kiwanda cha kuisaficha gesi kwani huwa inazalishwa ikiwa na viambata mbalimbali ambavyo hupunguza efficiency ya gesi lakin pia husababisha ugumu wa kuisafirisha.. gharama zake zitategemeana na wingi wa gesi unayo zalisha lakin pia aina na kiasi cha viambata ambavyo unataka kuvitoa kwani kuniaviambata vingine ambavyo ni complex kuviondoa kama hydrogen sulfide, but Tanzania hatuna gesi yenye sulfur gharama za kujenga plant hii ya kasafisha inaweza kurange kati ya dola million 100-200 million kwa kiwanda chenye uwezo wakuzalisha wastani wa 80-180MMcft per day , harafu utatandaza mabomba kutoka kiwanda cha kuchakata kilipo mpaka kwa wateja wako kama watakuwa hawapo mbali sana ( kama ndani ya nchi au nchi jirani ) gharama zake ni umbali wa kutoka mtwara mpaka somanga fungu, songosongo mpaka somangafungu harafu somanga fungu dsm imecost kama pesa za Tanzania zadi ya 1 tillion.

Lakin kama wateja wako wapo nchi za mbali lets say Tanzania to china hutoweza kujenga mambomba kwa umbali huo itakulazimu kujenga LNG plant ambapo itakuwezesha kubadilisha gesi yako kutoka kwenye gesi form kwenda katika liquid form hivyo basi mbali nakujenga kiwanda cha kusafisha gesi itakulazimu kujenga pia LNG plant kwa gharama zake zitategemia nakiasi utakacho safirisha kwa mwaka kam itakuwa ni tani million 1 kwa mwaka kiwanda chako kitagarimu takiribani dola za marekani 1.5bilion hii nikwenye plant ya kupabadilishia gesi kwenda kwenye liquid form lakin ikifika sokoni itabidi kujenga plant itakayo badilisha kuirudisha kwenye gesi form kiwanda hiki kitagharimu takribani dola za marekani 1 bilion uwezo wake itakuwa nikubadilisha kiasi cha gesi yenye ujazo wa 1billion cubic feet per day.

Kuhusu gharama za uzalishaji wa mafuta

Hapa itakulazimu kwanza kuchimba kisima cha uzalishaji au kubadilisha kisima kilicho chibwa kwaajili ya utafiti kiwe cha uzalishaji hivyo utaweka mabomba maalum kwa ajili kutoka chini mpaka juu kwenye well head baada ya hapo utaweka mabomba kutoka kwenye well head mpaka kwenye refinery plant ambayo utaijenga kulingana na wing I wa mafuta unayo zalisha, mfano Uganda wanataka kujenga refinery plant yenye uwezo wakuzalisha mapipa 60000 kwa siku kwa bei ya 2.5 billion dollar unawezakupata picha ya gharama zake lakin wakati huo huo kunakiasi cha mafuta kama 200000 ivi watapitisha Tanzania mpaka bandari ya Tanga kupitia kwenye bomba litakalo jengwa kwa gharama za shilingi 4 billion usa dollar so unaweza kuona how this iverstment cost a lot

So issue nkwamba ni ngumu kujua nkipi kinagharama kubwa kuliko kingne kutokana na mazingir za hiyo product ilipo, composition zake na soko lako
 
Naweza kujibu kama ifuatavyo Mr Mreno

2:Mafuta ni bidhaa muhimu sana kwa dunia ya sasa ni vipi mafuta hutokea?

Jibu

Mafuta hutengenezwa kutokana na mkusanyiko wa masalia ya viumbe hai na mimea ambavyo kwa pamoja hufukiwa na mchanga (sediments) kwa kipindi kirefu sana (millions of years) hasa katika maeneo ya mabonde, maziwa, bahari (basin area), mgandamizo na joto linalotokana na kinakirefu cha mchanga kilichofukia masalia ya viumbe na mimea ndicho kinachopelekea kuzalishwa kwa mafuta, gesi na makaa yam mawe (fossil fuels).


7.Gesi na Mafuta hutofautiana nini?

Jibu

Gesi na mafuta vyote hutengenezwa katika namna inayofanana kamailivoelezwa katika swali na 2 kinacholeta utofauti ni joto na mkandamizo unaotumika kutengeza,

Mafuta yenyewe hutengezwa katika joto kati ya (65'C na 150'C) joto hili hupatikana kutika kina 2000m mpaka 5500 meter, Joto likizidi 150'C basi hizo organic compounds ambazo zingekuwa mafuta sasa zitakuwa gesi asilia na likizidi 250'C basi izo organic compounds zitabadilika nakuwa graphite. (kumbuka Joto na mgandamizo huongezeka kadiri kina kinavyo ongezeka.


9. Kipi kati ya Gesi, Mafuta na Madini kina gharama kubwa katika uzalishaji?

Jibu

Napenda kuelezea kuhusiana na gaharama za gesi na mafuta pekee.

Kwanza gharama zinaanzia katika utafutaji na badae tutaona katika uzalishaji, ntaelezea katika mukitadha wa kitu kinaitwa oil and natural gas life cycle.

1. Gharama za kupata access (gaining Access)

Hizi ni gharama zitakazo husiana na kupata vibali katika mamlaka mbalimbali lakini pia kupata documents au taarifa za awali (data) kuhusiana na eneo amabalo unapanga kufanya utafiki ( gharama hizi zitategemea sana sheria na aina ya mikataba katika nchi husika lakin wastani ni dola za kimarekani 20 million na hutumia kati ya miaka 0 mpaka 2 kukamilisha taratibu katika kipengele hiki.


2. Gharama ya kufanya utafiti (exploration cost)

Gharama hizi zitahusisha tafti mbalimbali za awali utakazo zifanya kama aerial survey, seismic ( ambazo unaweza kuzifanya kwakutumia meli kama ni baharini au tracks kama ni nchi kavu) lakin pia gharama za kuchimba kisima kama tafiti za awali zitaonesha dalili njema za kuwepo mafuta au gesi na gharama za kufanyia analysis sample mbalimbali ambazo utazitoa kwenye kisima (gharama zake zitategemea eneo unalofanyia utafiti kama ni kinakirefu cha bahari au kifupi au nchi kavu) wastani wa gharama za kuchimba kisima kimoja katika nchi kavu (onshore) ni dola za kimarekani million 1 mpaka million 15 kutokana na urefu na complication za mahari kilipo wakati kuchimba kisima kimoja katika kina kirefu cha bahari (offshore) (1000 meta na kuendelea) ni dollar za marekani kuanzia million 100 nakuendelea ,so hapo utajumlisha na gharama nyingne za tafiti za awali ambazo zitategemeana na watoa huduma. Unaweza tumia miaka 4 au zaidi katika kipindi hiki cha exploration.


3. Gharama za kuchimba visima vingne zaidi kwa ajili yakujiridhisha kiasi kilichopo katika eneo (appraisal phase cost)

Katika hatua hii utalazimika kuingia gharama za kuchimba visima vingine kadhaa kama kisima ulicho chimba awali kimeonesha matumaini ya kuwepo mafuta au gesi, katika hatua hii visima vinaweza kuwa vitatu au zaidi kwa gharama zile zile nilizo zioredhesha katika point no 2, umhimu wa hatua hii nkutaka kujua jumla ya kiasi kilichopo katika eneo lako atachoweza kuzalisha, unaweza tumia miaka 2 au zaidi

4. Gharama za kuandaa miundo mbinu ya uzalishaji

Katika hatua hii sasa utakuwa tayari umejua kama kitaru chako kina mafuta au gesi au vyote kwa pamoja hivyo utatikiwa kuandaa mazingira ya uzalishaji kulingana na aina ya product iliyopo.


Kama ni gesi asilia ndo ipo

Itakulazimu kuandaa mazingira ya uzalishaji kutoka na soko lilipo kwanza itabidi kujenga kisima kiwe nahadhi ya uzalishaji na sio utafiti tena, hapa utaweka mabomba ya kuzalishia kuanzia chini ya kisima mpaka kwene well head na kisha utajenga kiwanda cha kuisaficha gesi kwani huwa inazalishwa ikiwa na viambata mbalimbali ambavyo hupunguza efficiency ya gesi lakin pia husababisha ugumu wa kuisafirisha.. gharama zake zitategemeana na wingi wa gesi unayo zalisha lakin pia aina na kiasi cha viambata ambavyo unataka kuvitoa kwani kuniaviambata vingine ambavyo ni complex kuviondoa kama hydrogen sulfide, but Tanzania hatuna gesi yenye sulfur gharama za kujenga plant hii ya kasafisha inaweza kurange kati ya dola million 100-200 million kwa kiwanda chenye uwezo wakuzalisha wastani wa 80-180MMcft per day , harafu utatandaza mabomba kutoka kiwanda cha kuchakata kilipo mpaka kwa wateja wako kama watakuwa hawapo mbali sana ( kama ndani ya nchi au nchi jirani ) gharama zake ni umbali wa kutoka mtwara mpaka somanga fungu, songosongo mpaka somangafungu harafu somanga fungu dsm imecost kama pesa za Tanzania zadi ya 1 tillion.


Lakin kama wateja wako wapo nchi za mbali lets say Tanzania to china hutoweza kujenga mambomba kwa umbali huo itakulazimu kujenga LNG plant ambapo itakuwezesha kubadilisha gesi yako kutoka kwenye gesi form kwenda katika liquid form hivyo basi mbali nakujenga kiwanda cha kusafisha gesi itakulazimu kujenga pia LNG plant kwa gharama zake zitategemia nakiasi utakacho safirisha kwa mwaka kam itakuwa ni tani million 1 kwa mwaka kiwanda chako kitagarimu takiribani dola za marekani 1.5bilion hii nikwenye plant ya kupabadilishia gesi kwenda kwenye liquid form lakin ikifika sokoni itabidi kujenga plant itakayo badilisha kuirudisha kwenye gesi form kiwanda hiki kitagharimu takribani dola za marekani 1 bilion uwezo wake itakuwa nikubadilisha kiasi cha gesi yenye ujazo wa 1billion cubic feet per day.


Kuhusu gharama za uzalishaji wa mafuta


Hapa itakulazimu kwanza kuchimba kisima cha uzalishaji au kubadilisha kisima kilicho chibwa kwaajili ya utafiti kiwe cha uzalishaji hivyo utaweka mabomba maalum kwa ajili kutoka chini mpaka juu kwenye well head baada ya hapo utaweka mabomba kutoka kwenye well head mpaka kwenye refinery plant ambayo utaijenga kulingana na wing I wa mafuta unayo zalisha, mfano Uganda wanataka kujenga refinery plant yenye uwezo wakuzalisha mapipa 60000 kwa siku kwa bei ya 2.5 billion dollar unawezakupata picha ya gharama zake lakin wakati huo huo kunakiasi cha mafuta kama 200000 ivi watapitisha Tanzania mpaka bandari ya Tanga kupitia kwenye bomba litakalo jengwa kwa gharama za shilingi 4 billion usa dollar so unaweza kuona how this iverstment cost a lot


So issue nkwamba ni ngumu kujua nkipi kinagharama kubwa kuliko kingne kutokana na mazingir za hiyo product ilipo, composition zake na soko lako

Sawa nimejifunza pia nashukuru sana kwa majibu mazuri
 
Kuna teacher mmoja alinifundisha wakati nikiwa skuli flani akiniambia medulla yangu INA madini sasa nataka kujua madini hayo ni aina gani na nitayatoaje?
Bwana lazaro
madini ni vitu vya thamani. teacher anapokuambia una madini anamaanisha unahakili . "hakili ni mali"
 
Kwanini Gas yetu asilia haiwekwi wazi kwamba twaweza ku i refine na tukapata gesi ya jikoni na bidhaa nyingine? Petroleum?
Bwana nzalendo jibu lako linajibiwa vizuri sana na NATURAL GAS UTILIZATION MASTER PLAN 2016-2045. Hii ni plan ya serikali ya Tanzania itakavyotumia gas. unaweza kuisoma hasa ukurasa wa 15 hadi 31. . ila pia kumbuka gas haifanyiwi utafiti na TPDC. Bali ni makampuni binafisi hupewa vitalu na kufanya utafiti na kulingana na sheria serikali inamiliki 20% na hivyo mipango ya uanzaji wa udhalishaji gas na mafuta inategemea mipango ya mabwana wakubwa wanaomiliki hisa kubwa pia pesa za kuendeleza miladi.
 

Attachments

  • oil and gas masterplan.pdf
    1.4 MB · Views: 790
Kuna tofauti gan kati ya mafuta na maji
Bwana ginius. nitakujibu kwa kigezo cha kikemia ambacho ndiyo kinafanya zitofautiane hata kimatumizi.
mafuta ni muunganiko wa carbon na hydrogen(C-H) ambayo tunaziita kwa jina la pamoja hydrocarbons. Lakini maji ni Hydrogen na oxygen (H20). SWALI LA NYOGEZA TAFADHALI!
 
1: Zamani enzi za mababu zetu walikuwa wanaokota dhahabu juu ya ardhi kwanini isiwe sasa au madini yaliyopo juu ya ardhi yaliisha na kama yaliisha ilikuwaje wakae juu ya ardhi kipindi hicho?

2:Mafuta ni bidhaa muhimu sana kwa dunia ya sasa ni vipi mafuta hutokea?

3: Nasikia Mchanga wa Madini una tabia ya kuzaliana na baadae kuwa madini je kuna ukweli juu ya hili na kama ni kweli kwanini?
4:Kuna aina ngapi za Madini duniani na ni madini gani ni ghali kuliko yote

5:Je hapa duniani 5:Je hapa duniani kuna (nchi) ukanda ambao hauna madini yeyote yale ?.

6:Je Kuna Mahusiano gani kati ya madini na Miamba?

7: Gesi na Mafuta hutofautiana nini?

8: Kwanini Nchi nyingi za Uarabuni zina Mafuta sana?

9:Kipi kati ya Gesi, Mafuta na Madini kina gharama kubwa katika uzalishaji?.

10:Ni dalili zipi za awali huonekana katika ardhi yenye Madini,Mafuta na Gesi kabla ya utafiti kufanyika(huwa kuna dalili zipi).

11:Naomba kujua hii gasi ya kupikia ina tofauti gani na hii gasi iliyopo hapa Nchini (Mtwara).

12: Mafuta ya Ndege Gari na vyombo vingine huwa yanatofautiana nini?

Mbwana Raphael

nitakujibu katia awamu mbili. sasa nakujibu swali la 1,3,4,5,6.

1: Zamani enzi za mababu zetu walikuwa wanaokota dhahabu juu ya ardhi kwanini isiwe sasa au madini yaliyopo juu ya ardhi yaliisha na kama yaliisha ilikuwaje wakae juu ya ardhi kipindi hicho?

jibu.

Kwanza dhahabu ipo ndani ya miamba na wakati mwingine miamba huwa imejitokeza juu ya aridhi na kisha miamba hiyo imeoza na kusababisha dhahabu iwe imetapakaa aridhini. kutokana na hilo mababu zetu wameokota sana dhahabu na hadi sasa watu wanaendelea kuokota sehemu mbalimbali hapa tanzania. lakini ukweri ni kwamba dhahabu za kuokota ambazo kwa kitalamu tunaita(placer deposit ) zimepungua sana na hivyo kinachohitajika ni kufanya utafiti wa miamba na kuchimba. lakini pia kila unapoona kuadhahabu za kuokota au ziliwahi kuokotwa inamaanisha kunamwamba wa dhahabu karibu umeoza kwa kitaalamu(rock weathering) na kusababisha dhahabu hiyo itapakae hapo. hivyo pia dhahabu zilizotapakaa zinatoa kiashilia kuwa kunamwamba kalibu hapo na ukifanya utafiti unaweza kuupata.

3: Nasikia Mchanga wa Madini una tabia ya kuzaliana na baadae kuwa madini je kuna ukweli juu ya hili na kama ni kweli kwanini?

jibu

siyo kweri. napenda kukujulisha kuwa dhahabu imetapakaa kwa kiwango cha 0.004gram/ton katika dunia. hii inamaana ukikusanya mawe tani 1000 unapata gram 4 za dhahabu. sasa kunamichakato ndani ya dunia ambazo husababisha dhahabu zijilude sehemu dongo ambapo tunaita sehemu hiyo mwamba wa dhahabu.(their several process that cause mobiliazation of gold eg hydrothermal activity, metamorphism,and volcanism). michakato hii ndiyo huweza kukusanya dhahabu kutoka kiwango kidogo na kuiweka sehemu moja ikawa kiwango kingi) mfano wastani wa mwamba wa dhahabu ya GGM NI4gram/ton, tulawaka 12gram/ton. ukienda kwa wachimbaji wadowadogo utasikia lugha za kiloba kimoja kinatoa kiasi gani?. yaweza 2gran/kiloba, 4gram/kiloba. lakini viloba vya mawe ya dhahabu vikitunzwa haiwezi dhahabu kuongezeka.. sasa mchanga wa madini wauwezi kuzaliana ni sawa na kutunza mchele stoo. hauwezi kuongezeka wala kupungua. nimekujibu kwa kutumia aina ya madini ya dhahabu lakini naamanisha madini yote hayawezi kudhaliana kwa kutuzwa.

4:Kuna aina ngapi za Madini duniani na ni madini gani ni ghali kuliko yote.

jibu

kunaaina dhaidi ya 2200 ya madini(mineral) duniani. nitakufafanulia kwa udani kidogo kwa namuna mbili ya kitaaluma na kibiashara.
naanza na ya kitaalamu
madini yamegawanyika katika makudi 8 (mineral classification)
1) native elements mfano gold, platinum, diamondi ect
2) sulfides and sulfosalt mfano cinnabar madini yanayochenjuliwa ili kupata mercury,galena etc
3) oxides and hydroxides mfano spinel, corundum, uranium, hematite, chromate,magnetite etc
4) halides mfano halite (chumvu), Fluorite ect
5) carbonates, nitrates, borates mfano calcite, magnesite, malachite na azurite etc
6) Sulfate, chromates, molybdates na tangestate mfano gypsum,barite, etc
7) Phosphates , arsenates, vanadates mfano phosphates, Apatite etc
8) silicates mfano feldisper, garnet,tanzanite, quartz, clay ect

kwa kigezo cha kibiashara
1) metalic minerals mfano gold(dhahabu), copper(shaba), nickel cte
2) industrial mineral mfano graphite, feldsper, calcite, etc
3) Gemstone mineral mfano Tanzanite, Diamond(alimasi), ruby, Lulu etc.
4) Energy mineral mfano Uranium, makaa ya mawe etc

madini ya bei ya juu sana ni madini yanayotoka katika kundi la gemstone
ambayo hasa yanaongozwa na Diamodi na kufuatiwa na ruby. mfano diamodi kutoka mgodi wa williamson mwadui mwaka 2015 yenye ukubwa wa 23.16carat(4.632gram) iliuzwa usd $10.6million. na hivi karibuni 2017 diamond 59.6 carat(11.92gram) iliuzwa usd$71.2million. kunamengine kama spinel, green garnet etc. lakini pia katika madini ya metallic yanaongozwa na dhahabu ambayo kwa leo inauzwa TSH89000-91000) kwa gram. NA BEI ZA MADINI YA BEI YA CHINI KABISA YANATOKA KWENYE KUNDI LA INDUSRTIAL MINERAL. MFANO KIWANDA KILICHOZIDULIWA HIVI JUZI HAPO MKURANGA KINANUNUA TANI MOJA YA FELDSPAR KWA TSH 80000. INAMAANA UKACHIMBE NA UPEREKE KIWANDANI WEWE MWENYE.


5:Je hapa duniani kuna (nchi) ukanda ambao hauna madini yeyote yale ?. na

jibu

madi yako kila sehemu. ila tofauti ni kwamba madini haya yanaweza kupatikanika tanzania na aina nyingine yakapatikanika ghana na vile vile aina moja ya madini yanaweza kupatikanika nch mbalimbali ila kwa wingi tofauti.etc. mfano mzuri madini yamesambaa sawa sawa na unavyoona katika maswala ya kilimo. mfano zao la pamba ni kanda ya ziwa lakini zao la korosho ni ukanda wa pwani. mahindi tunapata rukwa na ruvuma kwa wingi na kahawa tunapata bukoba na kilimanjaro. ndivyo ilivyo katika madini. hivyo hakuna nchi isiyokuwa na madini bali unaweza sema nchi inaweza kuwa na madini ya aina frani tu na isiwe na mengine. kwa dhaidi ninakutumia picha ili uangalie njisi madini yalivyosambaa duniani kila picha itaonesha madini aina maja na njinsi yalivyosambaa duniani. inamaana kila aina ya madini yanahitaji mazingira mfani ili yajitengeneze. na hivyo mazingira hayo yakiwepo nayo nayatokea.

6:Je Kuna Mahusiano gani kati ya madini na Miamba?

jibu

s
wali hili pia litasaidia sana uelewa na jibu la No5 .
maana ya neno mwamba(rock) ni muunganiko wa madini(mineral) mbalimbali ndiyo yanafanya yatengeneze mwamba ila pia kuna miamba iliyotengeezwa na dini la aina moja. yaani rock is a combination or composition of different type of mineral but in some cases rock are monomineral.
hii maana yake popote pale uokotapo mwamba au jiwe ujue ni dini hili. hii maana yake dunia(earth) ni mwamba na mchanga ote pamoja udongo wote unaouona ni madini kwani umetokana na kuoza kwa mwamba na mwamba ni muunganiko wa madini. mfano mchanga ni madini tena mchanga tuaojengea nyumba au unaouona ufukweni(beach) ni madini yaitwayo quartz na haya hutumika kutengeneza vioo na asilimia 80 ya vioo au niweke vizuri glass (c hupa za soda, bia etc)ni mchanga kama huo. sasa basi miamba imejipanga aridhini kwa utaratibu flani na diyo maana hata madini yanatokea kwa utaratibu flani kulingana na miamba ilivyokaa. cha msingi hapa utambue kuwa siyo kila dini linahitajika kwa matumizi ya shuguli za binadamu. pia siyo kila dini linathamani sana. nitakuwekea ramani ya tanzania kukuoneya miamba njisi ilivyojipanga. kila baka kwenye ramani ya tanzania ya kijeolojia inaamanisa aina flani ya miamba na kwa uchache kutakuwa na madini hasa utaona madini ya dhahabu, chuma na makaa ya mawe




ASANTE SANA KWA MASWALI WA URENO KARIBU KWA SWALI LA NYONGEZA KAMA KUNASEHEMU SIJAJIBU KWA USAHIHI AU NIMEKUACHA NA DUKUDUKU.










 

Attachments

  • deposite 6.jpg
    deposite 6.jpg
    9.1 KB · Views: 239
  • deposite2.jpg
    deposite2.jpg
    9.4 KB · Views: 179
  • deposite4.png
    deposite4.png
    9.2 KB · Views: 176
  • deposite5.png
    deposite5.png
    12.6 KB · Views: 201
  • deposits-3.jpg
    deposits-3.jpg
    65.9 KB · Views: 184
  • deposi 1.jpg
    deposi 1.jpg
    9.6 KB · Views: 202
Back
Top Bottom