Seran
JF-Expert Member
- Feb 7, 2025
- 10,620
- 31,829
Binafsi nikiwa na huzuni inaniletea sonona sijui huwa ni kwanini najisikia hivi, kitu kikinikosesha raha kabisa nawaza sana mapigo ya moyo yanaenda kwa kasi kila nikifikiria upya!
Mbaya zaidi inanipelekea nakosa hamu ya kula, hata nikila naonja onja tu,napata homa ya ghafla, sijisikii kuongea na watu,sitaki mtu anipigie simu, sijisikii kwenda kazini na hata nikienda sijisikii kuongea na watu ni tumbo joto tu, nataka kukaa mwenyewe chumbani ata siku mbili hadi 3! Natamani chumba kisiwe na mwanga uwe wa mbali sana! Nakaa tu ndani na siwezi kufanya chochote! Sitamani kuoga, kula sebleni wala kupika japo itanilazimu sometimes😩
Hivi na nyie mnapitia hii hali mkiwa na stress au ni mimi tu?🥺
Mbaya zaidi inanipelekea nakosa hamu ya kula, hata nikila naonja onja tu,napata homa ya ghafla, sijisikii kuongea na watu,sitaki mtu anipigie simu, sijisikii kwenda kazini na hata nikienda sijisikii kuongea na watu ni tumbo joto tu, nataka kukaa mwenyewe chumbani ata siku mbili hadi 3! Natamani chumba kisiwe na mwanga uwe wa mbali sana! Nakaa tu ndani na siwezi kufanya chochote! Sitamani kuoga, kula sebleni wala kupika japo itanilazimu sometimes😩
Hivi na nyie mnapitia hii hali mkiwa na stress au ni mimi tu?🥺