Habari wanajamvi,
Mimi ni msomaji mzuri na member wa muda kidogo hapa jamii forum na nimekuwa nikifuatilia matukio , habari na makala mbalimbali humu, bila kusahau nyuzi zinazoanzishwa.
Miongoni mwa nyuzi ambayo napenda kuifuatilia kila siku ni hii hii ya kula tunda kimasihara. Inafahamika wazi kuwa wanaume ndio wanaopenda au kwa hulka wanaamimiwa kuwa hawawezi kubaki au kuwa na mwanamke mmoja. Sina uhakika sana na hoja hiyo lakini pia siwezi kupingana na hoja hiyo bila kuwa na ushahidi madhubiti.
Wakati naufuatilia hoja ya mwanamke kuliwa kimasihara hasa mke wa mtu napata ukakasi na kujiuliza maswali pasi majibu
1 Je manawake nao hawawezi kutulia na mume mmoja?
2. Kama mwanamke ana mume wake ambaye wakati mwingine anamsemea kuwa anampenda Sana,kwa nini sasa mwanamke huyo anachepuka?
3. Je kumpa mwanamke kila kitu anachokitaka itamzuia mwanamke huyo asichepuke?
4. Mwanake uliyeolewa kuliwa kimasihara maana yake kuwa huridhishwi na mume wako au niamini kuwa mwanamke naye anapenda kujaribu?
Najua kuliwa mke ni jambo ambalo mwanaume huwezi kulizuia ila mwanamke mwenyewe anaweza akiamua.Lakini pia kuliwa kumauma.
Sent using
Jamii Forums mobile app