Kuna siku December 2021 sikumbuki tarehe nlienda kwenye ofisi ya moja wa clients wetu wakubwa, issue ya support na troubleshooting. Nkapokelewa vizuri na kupelekwa server room yao, nkafanya yangu wakawa fresh. Wakati naagana na technical manager wa pale, akanipeleka na ofisi ya wahasibu wao nichukue na cheque ya malipo ya mwezi uliopita.
Mimi huwa sihusiki na cheque coz sio mhasibu lakini coz nilikua pale wakaona niichukue tu niende nayo.
Kwenye hyo ofisi ya wahasibu nkakuta watu watatu. Mwamba mmoja anaonekana mtu poa sana, mmama mmoja wa makamo na binti mmoja pisi ina muonekano wa kichaga au kisukuma, mweupe, ana shape moja matata sana. Nkajisemea moyoni nkiipata hii pisi naweka kambi hapa, ishu ni naanzaje.
Nkaishia kuchukua cheque na kusepa. Baada ya wiki hivi nkarudi tena pale. Baada ya kutoka server room nkajipeleka ofisi ya wahasibu, nkamkuta yule mmama na yule binti, nkawapigisha story pale hazina kichwa wala miguu. Wakati naaga nkawaambia ni vzuri niwe na namba zeo kama wana shida waweze kuntafuta directly wakanipa wote nkasepa.
Baada ya kama siku tatu nkaipigia ile pis nkajitambulisha na vistory kidogo ikaisha. Baada ya hapo nkawa naona status zake (Mimi hu2a siwekagi status, ever). Mara moja moja nacomment tunachat kidogo yanaisha. Ile mwaka mpya unakaribia kuna siku nkamtext whatsapp tukawa tunachat kizushi, nkamuomba outing. Mimi huwa nikimuelewa mwanamke sizungushi, namfanya ajue nimemuelewa ajue yeye ataamua vipi.
Na kweli kanipiga chini, kasema hawezi ana mtu wake na bla bla kibao. Nkajifanya muelewa af nikamute life likaendelea. Baada ya hapo chats zikaishia tu kucomment status. Uzuri anajijua akivaa gauni fupi fupi au skirt anatokelezea balaa so status zake nyingi anakua kavaa hivyo. Mara mojamoja nacomment ujinga tu wa kumsifia kuwa mwamba anafaidi kumkaza anaishia kucheka tu kwa viimoji na kusema nna tabia mbaya na mimi nakausha. Nkaomdoa possibility ya kumla coz kuisotea sikutaka. Maisha yakaendelea
Jumamosi ya juzi 19 Feb nilikua na mechi ya kikapu na veterans wenzangu (wana tuliodunda sana kikapu miaka hiyo ya umiseta na chuo. Now kwa sababu ya majukumu, umri, bia na uzinzi tunaishia kudunda mara moja au 2 kwa mwezi). Maeneo ya posta kiwanja flani hivi, mida ya saa 10 wakati naenda uwanjan nkawa nachat nae akaniambia anaumwa kichwa na mafua halafu home yuko peke yake (Alishaniambiaga anaishi tabata na dada yake). Nkampa pole nkamuambia nkitoka kwenye mechi ntakuja kukuona na matunda, kauliza saa ngapi nkamuambia saa 1 mechi inaisha halafu tunafanya close down, kwenye saa 1 na nusu ndo nakua nasepa, akasema sawa.
Veterans kama veterans tukafungwa hiyo mechi, vijana wako moto sana plus pumzi na mazoezi, tulikua hatutoboi. Wakati tunafanya close down nkaona ananipigia nkaimute. Tulivomaliza nkampigia nkamuambia ndo natoka, kasema poa na kanielekeza kituo cha kushuka.
Veteran nkashuka buguruni nkanunua matunda kibao nkadaka bolt nkaenda pale aliponielekeza chap. Nkampigia kaniambia nisubiri.
Alivofika pale kituoni kaja kavaa kigauni cha kushindia home, ni balaa. Kinaishia juu ya magoti hivi af kilainiii, design flan kama ilikua kijora af kaenda kukishona kiendane na mwili wake.
Nkampa matunda yake hao mdogo mdogo hadi anakoishi, ni vyumba viwili, sebule, choo na kajiko. Kaingia jikoni na matunda katoa baadhi mengine kaweka kwenye friji, akakata matango na machungwa tukawa tunakula huku tunapiga story kizushi. Ndo akaniambia dada yake kaenda kwenye harusi ya staff mwenzao atarudi night kali. Tulipomaliza kachukua zile sahani kaenda kwenye kile kijiko akawa anazisuuza kwenye sink, nkamfata na kumkumbatia kwa nyuma nambusu shingoni huku mikono inafanya utalii huku namsifia, akawa anasema niache mm naumwa huku anasogeza shingo lakini mikono haitoi. Nkaendeleza mashambulizi mpaka akalainika na kugeuka mwenyewe anipe mate.
Huwa nachaguaga sana wanawake wa kuzama chumvini, lakini hapa nlizama bila kujiuliza. Nimepiga viwili vyangu nkasepa. Nlipanga nkaangalie game ya man city na tot lakn ndo nkawa nshaichelewa ingawa tot walijua sana kunifurahisha, yule kipara alikua ashaigeuza ligi ya wingereza kuwa yake.
Kesho yake jumapili mchana kaja home kwangu rasmi kwa ajili ya show sasa, nmeambiwa tu niandae wine nzuri.
Life linasonga, nasubiri jmosi aje nizame chumvini tena. Kuhusu yeye na bwana wake watajisort wenyewe.