funzadume
JF-Expert Member
- Jan 28, 2010
- 13,560
- 21,041
Unaharibu uzi wetu we boyaNiliwahi kusafiri kuelekea mwanza
Kwa mbele ya Siti niliyokaa walikaa mdada na mkaka.
Nilikuwa nimetulia Sina Mambo mengi zaidi ya kuangalia mandhari dirishani, hata jirani niliyekaa nae sikumbuki alikuwa na jinsia gani! Ule mwaka Ulikuwa 2014.
Hawa jamaa yaani dada na kaka pale mbele yangu stori zilikuwa nyingi Sana, na Kama ilivyodesturi ya mabraza kujishobokesha saana kwa wadada, nilianza kuona huyu brazamani anavyojibidisha kumcare yule binti, kwa huduma ndogondogo mule njiani
Giza likaanza kuingia, nikaanza kuona brazamani mdogomdogo anaanza ukorofi wa mapenzi
Akaanza kuweka mkono kwenye bega la binti, Mara anachezea nywele za binti, Ila binti akiona Hali inazidi nae anazuia mashambulizi kwa kuzuia Ule mkono wa yule bishoo! Mara kwa Mara alikuwa anamwambia "sitaki bwana!"
Mie nimetulia tu naangalia hii picha kwa makini
Duuh, braza akavuka mipaka akapeleka mkono wake kwenye kifua Cha yule dada,aisee, binti akausukuma Ule mkono wa bro kwa hasira na akaondoka kwenye Ile Siti
Naona bro alifadhaika kidogo na katika kupunguza Soo akageuka kutuangalia huku akisema"yaani wanawake wajinga Sana, Sasa anakasirika Nini?
Tangu hapo wagomvi Hawa hawakuongea Tena, na tulipofika Mwanza nikaona kila mmoja ameshika hamsini zake
Hao ndio wanaume
Kukaa na wadada bila kuwatamani haiwezekani
Halafu wanatuambia eti UNEXPECTED SEX!
Mabraza mutuandikie na Yale MATAMANIO YENU YALIYOFELI na kuwapa AIBU tucheke pia