Ulishawahi kufikiria kitu halafu ukakikuta kwenye Mitandao ya kijamii?

Da'Vinci

JF-Expert Member
Dec 1, 2016
35,688
106,829
1680111580493.png

Binafsi sio mshabiki wa mpira kabisa ila 2022 mwishoni nilianza kuahabikia timu ya Yanga, nikajikuta die hard fan. Kombe la dunia lilipoanza nikawa naangalia maramoja moja, siku moja nikasearch Google ratiba ya mechi nikaangalia, baada ya muda usiku nikaingia FB nikaona Meme inayohusu mpira kutoka kwenye Fan pages za Asians nikaingia kwenye hiyo page kisha nikatoka.

Baada ya muda kidogo nikarudi Facebook nikakuta page kibao pale kwenye suggestions zinazohusu mpira kutoka nchi za asia. Kwakua Memes zilikua zinafurahisha nikawa naingia kwenye page mojamoja naangalia. The rest is history Facebook yangu ikabadirika muonekano ikawa imejaa masula ya mpira tu.
FB_IMG_16709683044861352.jpg

[Meme yenyewe ni hii]


[NB. Fb sipo connected na mtu yoyote I meaan sina rafiki nipo mimi tu, that's why ilibadirika na kua ina mambo ya mpira tu before ilikua ina masuala ya Movie]

Argentina walivyochukua kombe nikasachi account ya Lionel Messi nikaangalia picha alizopost Kisha nikatoka, niiliporudi tena fb nilikuta Pages kibao zinazomuhusu Messi.
Kwakua nafahamu nini kinatokea sikushangazwa na kuyaona hayo.

Kama utakua ni mtumiaji wa Mitandao ya kijamii hasa Youtube, Facebook, Instagram, WhatsApp, Tiktok nk unaweza kua ishawahi kukutokea hili tukio. Kuna wakati unaweza ukawa unafikiria kitu fulani ila ukiingia tu FB au instagram ukakiona kikiwa katika mfumo wa tangazo (Advertisement/Sponsored) pengine hata ukisachi kitu Google kile kitu ukienda Insta au FB unakuta page zinazozungumzia kitu hicho au kukiuza.

Kwa wenzetu huko ambao muda mwingi wapo connected na Internet hua hata wakiwa wanaongelea kuhusu kitu fulani wakiingia tu mitandani kile kitu wanakikuta kinatangazwa. It's like walikua wanasikilizwa na hii ipo zaidi katika vifaa vya vyenye mfumo endeshi wa Android OS.

Hapo ndipo inapoingia suala la algorithm na Machine Learning. "Algorithm" ni mfumo uliowekwa kwa ajili ya kutatua tatizo au hitaji la mtumiaji wa vifaa vya computer na Internet na kufanya mahesabu kadri ya hitaji la mtumiaji (End User).

Algorithm inakua kama mfumo fulani uliotengenezwa ili kufanya kazi fulani hatua kwa hatua kwemye software au hardware. Katika kile seju ambapo Information Technology ipo basi tambua kwamba Algorithm ipo pia.

Machine Language ni algorithm inayotumika kutengeneza (Generating) Algorithm. Kwa waliosoma mada yangu ya Artificial intelligence nilielezea mambo haya kwa urefu zaidi maana Machine Language ipo ndani ya Artificial Intelligence.

Sasa basi mitandao ya kijamia (Nitazungumzia zaidi FB maana situmii Twitter, Insta, Tiktok nk) hasa Facebook mtu anapojiunga hua ana "Accept Company's Privacy Policy" najua wengi hua hatuzisomagi hizo.

Ukizisoma sera/ policies hizo utagundua kwamba pindi unapokubali basi unakua umeruhusu Facebook kuchukua taarafia zako kama Majina yako, Group na Pages utakazojiunga, Tarehe ya kuzaliwa, Watu unaofahamiana nao, pengine hadi namba zako za simu wanazichukua nk na hili hua hatujui maana kwenye kujiungahua tunabonyeza tu Accept bila kujua ndio maana ukienda kwenye Setting>>>Imported Contact utazikuta namba zako zote ulizowahi kutumia toka ujiunge Fb.

Pia Facebook hua inauwezo wa kujua hadi Apps ulizonazo kwenye simu yako, Location yako, Aina ya simu yako, Kama upo kwenye Wi-Fi Facebook inaweza kujua hata watu walioLog In kwenye hiyo WiFi Network.

So kwa njia hizo na zingine kibao inapelekea Fb kukujua vyema ndio maana unaweza hisi kwamba wanatusoma akili zetu lakini si kweli it's just Data Collection.

Algorithm ya mitandao ya kijamii hua inapamgilia machapisho/Posts yaonekane kwako kutokana na mapendeleo yako na sio yale yaliyo mapaya. Kama kitu ni kipya na hakipo kati vile uvipendavyo hutaweza kuviona na kama kitu ni cha zamani ila unakipenda ipo silu utakutana nacho.

Zamani miaka ya 1770s dunia ilipiga hatua kubwa baada ya Industrial Revolution, nchi zilizokua na nguvu ni zile zilizokua na viwanda vingi zaidi hapo ndio Britain ilipozipiga bao nchi zingine za Europe. Baadae miaka ya 1900s dunia ikahamia kwenye Era ya Arms and Ammunition, nchi iliyokua inasiraha nzito nzito ndio iliokopeka zaidi Hapo ndio Germany,USSR, USA zikaibuka.

Sasa tupo Digital World malighafi muhimu kuliko zote kwa sasa kuliko siraha,Chuma au viwanda ni Information. Yaani taarifa muhimu kwa wakati sahihi, Kwakweli makampuni ya Teknolojia kama Google,apple Inc, Disney,Sony, Meta nk wameweza kutuweka kati. Hakuna wasiojua kutuhusu. Pengine wanatufahamu kuliko tunavyojifahamu.
FB_IMG_16779913957518355.jpg

Alamsiki...ningependa kuendelea ila vidole vimechoka😟
~Da'Vinci
 
Nafkr wameset search engine zote hasa za mmarekani zinakuwa connected na mitandao ya kijamii , ina maana ukiingia google kuangalia kitu fulan , taarifa zako za simu na kile unachotafta zinafika kwenye mitandao ya kijamii , ukifungua tuu taarifa inatoka kwamba unatfta kitu fulan , wanadesplay chap , mi nafkr hvyo
 
Nafkr wameset search engine zote hasa za mmarekani zinakuwa connected na mitandao ya kijamii , ina maana ukiingia google kuangalia kitu fulan , taarifa zako za simu na kile unachotafta zinafika kwenye mitandao ya kijamii , ukifungua tuu taarifa inatoka kwamba unatfta kitu fulan , wanadesplay chap , mi nafkr hvyo
Google na makampuni ya mitandao ya kijamii kijamii wanashirikiana kulink taarafia wenyewe wanaita Web Data Collection. Kuna Machine Learning zinafanya kazi hiyo
 
Nouma sana , leo hii ukisearch bidhaa Alibaba , ukija google , youtube , instagram , fb zinakuja ads za bidhaa kama zote

Kwa upande wa Google huko wao wana project yao wanaita Hummingbird, hii ni alogarithm ambayo inafanya kazi ya kumwezesha mtumiaji wa huduma za google (Hasa YouTube na Google as Search engine) kupata huduma hizo kwa urahisi na kwa haraka...wanasema Google inakujua kuliko mama yako mzazi, Ni kweli.

Unapotafuta kitu Google chochote Hummingbird inarekodi kila kitu baadae ukitaka kuitumia tena inakuletea vitu kama vile ulivyotafuta mwanzo. Ndio maana ukitafuta kitu fulani YouTube ukaangalia ukamaliza labda ukatoka huko baadae ukirudi tena youtube utakuta video mbalimbali zinazoshabihiana na zile ulizoangalia mwanzo.

Yes kwakua Google wanakua washajua ni vitu gani unapendelea ili usisumbuke kuandika wanakuletea hapo kwenye homepage as suggestion posts
 
Kwa upande wa Google huko wao wana project yao wanaita Hummingbird, hii ni alogarithm ambayo inafanya kazi ya kumwezesha mtumiaji wa huduma za google (Hasa YouTube na Google as Search engine) kupata huduma hizo kwa urahisi na kwa haraka...wanasema Google inakujua kuliko mama yako mzazi, Ni kweli.

Unapotafuta kitu Google chochote Hummingbird inarekodi kila kitu baadae ukitaka kuitumia tena inakuletea vitu kama vile ulivyotafuta mwanzo. Ndio maana ukitafuta kitu fulani YouTube ukaangalia ukamaliza labda ukatoka huko baadae ukirudi tena youtube utakuta video mbalimbali zinazoshabihiana na zile ulizoangalia mwanzo.

Yes kwakua Google wanakua washajua ni vitu gani unapendelea ili usisumbuke kuandika wanakuletea hapo kwenye homepage as suggestion posts
Na ukiclear history search
 
Google - They have Hummingbird
Facebook - Algorithm
Instagram - I thought Algorithm

What about JF?
Kuna muda naaingia humu hili kusoma nyuzi fikirishi zenye contents.
Lakini unakutana na nyuzi "mume wangu anifikishi kileleni" au kama hizi mada za One gender relationship "LGBTIQA" (Lesbian, Gay, Bisexual, Trans/transgender)🤗🤗 unajiuliza what a fu.......k is thiz? unafanya kuignore unapita kushoto.

JF wanafikiria nn?
Hili kuendena na kasi ya maendeleo ya sayansi na teknolojia.
For Example: I'm big fan Of Vinci, pindi napo login in in my account ni vyema kuwe na sehemu inayonilitea mada pendwa zinazo-correlate na mimi na mtu ninae like na kusoma sana threads topic zake instead of going straight into a specific forum.

✍️Itasaidia sana kwenye kuokoa muda na mtu kupata content materials anazopenda kuzisoma kwa muda sahihi na wakati sahihi.
✍️Act as a Filter or Chujio, kwa kuchuja na kumletea mtu kile ambacho angependa kukisoma na kujifunza hapa mjini JF.

👏👏 Marvelous One🔥 Mr. Random Useless Guy

Adios Compatriot
✌️

By "No One Who Is Someone"​
 
Google - They have Hummingbird
Facebook - Algorithm
Instagram - I thought Algorithm​
Nikuweke sawa kidogo, mitandao yote ya kijamii wanatumia Algorithm sema ndio wanakua wameipa majina tofauti tofauti. Mfano Facebook Wanatumia Algorithm iliyopo katika mfumo wa Machine Learning, Google wao Algorithm yao wameiita Hummingbird

What about JF?
Kuna muda naaingia humu hili kusoma nyuzi fikirishi zenye contents.
Lakini unakutana na nyuzi "mume wangu anifikishi kileleni" au kama hizi mada za One gender relationship🤗🤗 unajiuliza what a fu.......k is thiz? unafanya kuignore unapita kushoto.​
Kwa JF ni ngumu kidogo maana wao ni Forum. Forum unaweza kuinunua ukaCustomize vile upendavyo. Lakini kitu kama Facebook hiyo ni lazima uanzie from scratch kutengeneza so kwa JF inaweza kua vigumu kidogo kwa sababu wao hawana means au platform zao binafsi bali wanalipia tu (?)

JF wanafikiria nn? Hili kuendena na kasi ya maendeleo ya sayansi na teknolojia.
For Example: I'm big fan Of Vinci, pindi napo login in in my account ni vyema kuwe na sehemu inayonilitea mada pendwa zinazo-correlate na mimi na mtu ninae like na kusoma sana threads topic zake instead of going straight into a specific forum.

Itasaidia sana kwenye kuokoa muda na mtu kupata content materials anazopenda kuzisoma kwa muda sahihi na wakati sahihi.​
Nahisi hii inawezekana ukiFollow watu kuna sehemu ukienda mbele ya New Posts utakuta michango ya uliowafollow tu

👏👏 Marvelous One🔥 Mr. Random Useless Guy

Adios Compatriot
✌️

By "No One Who Is Someone"​
Thanks for compliments Sir.
It's me Just a random person ☺️
 
Na ukiclear history search​
Kwenye Computer Processors kuna kitu kinaitwa Caches, hii ni sehemu ambapo ukifinya kitu fulani kwenye computer b Iasi kile kitu kinahifadhiwa huko ndani ili ukitaka kukitumia tena basi kinafanyiwa kazi kwa haraka zaidi. Pia kuna kitu kingine kinaitwa HTTP Cookie hizi zinafahamika pia kama Web cookie, browser cookie, internet cookie. Hizi ni data ndogondogo ambazo huchukuliwa kwenye web, internet, browser n.k na kuhifadhiwa kwenye Computer wakati mtumiaji yuko anaperuzi. Kazi yake ni kurekodi mambo yote ambayo mtumiaji (user) anayafanya kwenye internet mfano. Zinarekodi Password, page ipi umetembelea, Majina, nk. Hayo yote yanakusaidia wewe mtumiaji wa internet utakapotaka kuperuzi mitandaoni basi iwe rahisi kutumia.

Kwenye Computer ili kuziepuka cookies baada ya kutumaliza kuperuza mitandaoni inatakiwa uende upande wa setting kisha chagua Clear Cookies ili kuondoa kumbukumbu zote zote za kuperuzi siku hiyo. Kwa upande wa Google kubaki na taarifa zako. Huwa tunashauri kutumia Search Engine ya Duck Duck Go, Hii web ni nzuri zaidi maana hua ina clear taarifa zako zote baada ya kumaliza kuitumia..ina mengi mazuri ya kiusalama hasa kwenye taarifa za utumiaji wa kila siku (Browsing History).

Ndio maana juu mwanzo wa post hii nimeweka Logo ya Duckduckgo
 
Kwenye Computer Processors kuna kitu kinaitwa Caches, hii ni sehemu ambapo ukifinya kitu fulani kwenye computer b Iasi kile kitu kinahifadhiwa huko ndani ili ukitaka kukitumia tena basi kinafanyiwa kazi kwa haraka zaidi. Pia kuna kitu kingine kinaitwa HTTP Cookie hizi zinafahamika pia kama Web cookie, browser cookie, internet cookie. Hizi ni data ndogondogo ambazo huchukuliwa kwenye web, internet, browser n.k na kuhifadhiwa kwenye Computer wakati mtumiaji yuko anaperuzi. Kazi yake ni kurekodi mambo yote ambayo mtumiaji (user) anayafanya kwenye internet mfano. Zinarekodi Password, page ipi umetembelea, Majina, nk. Hayo yote yanakusaidia wewe mtumiaji wa internet utakapotaka kuperuzi mitandaoni basi iwe rahisi kutumia.

Kwenye Computer ili kuziepuka cookies baada ya kutumaliza kuperuza mitandaoni inatakiwa uende upande wa setting kisha chagua Clear Cookies ili kuondoa kumbukumbu zote zote za kuperuzi siku hiyo. Kwa upande wa Google kubaki na taarifa zako. Huwa tunashauri kutumia Search Engine ya Duck Duck Go, Hii web ni nzuri zaidi maana hua ina clear taarifa zako zote baada ya kumaliza kuitumia..ina mengi mazuri ya kiusalama hasa kwenye taarifa za utumiaji wa kila siku (Browsing History).

Ndio maana juu mwanzo wa post hii nimeweka Logo ya Duckduckgo
Nimekupata mkuu , hii Duckduckgo hata kwenye smart inafanya kaz au computer tuu
 
Nimekupata mkuu , hii Duckduckgo hata kwenye smart inafanya kaz au computer tuu
Duckduckgo ni search Engine kama ilivyo Google, Bing,Yahooo, Nk nk.
Ili uitumie kwa urahisi ni bora ukatumia Browser ambayo haimilikiwi na Google kama Chrome. Chrome inamilikiwa na Google so by default imeweka Google kama search Engine yake. Hivyo basi jaribu Kuitumia kwenye browser kama Opera, Phoenix,Mozira, Microsoft Edge, nk. Lakini kwakua Google kadorminate sana soko la Search Engine nadhani hata hizo browser wameziset Google iwe Default search Engine.

So nenda kwenye Setting kisha itoe Google weka Duckduckgo as Search Engine
Screenshot_20230329-225350~2.png
Screenshot_20230329-225249~2.png
 
Ndio maana huwa nashangaa sana kwann kwenye Google news nakutana sana na mastory au habari za mashoga na ushoga kumbe ni kwasababu huwa nawaponda sana huku JF na kuwaongelea na watu so simu inarekodi inaniletea habari zao. Mbwa hawa.
 
Ndio maana huwa nashangaa sana kwann kwenye Google news nakutana sana na mastory au habari za mashoga na ushoga kumbe ni kwasababu huwa nawaponda sana huku JF na kuwaongelea na watu so simu inarekodi inaniletea habari zao. Mbwa hawa.
Nenda Setting kisha kwenye Permission ziwia notification. Hutaziona tena
 
Google - They have Hummingbird
Facebook - Algorithm
Instagram - I thought Algorithm

What about JF?
Kuna muda naaingia humu hili kusoma nyuzi fikirishi zenye contents.
Lakini unakutana na nyuzi "mume wangu anifikishi kileleni" au kama hizi mada za One gender relationship "LGBTIQA" (Lesbian, Gay, Bisexual, Trans/transgender)🤗🤗 unajiuliza what a fu.......k is thiz? unafanya kuignore unapita kushoto.

JF wanafikiria nn?
Hili kuendena na kasi ya maendeleo ya sayansi na teknolojia.
For Example: I'm big fan Of Vinci, pindi napo login in in my account ni vyema kuwe na sehemu inayonilitea mada pendwa zinazo-correlate na mimi na mtu ninae like na kusoma sana threads topic zake instead of going straight into a specific forum.

✍️Itasaidia sana kwenye kuokoa muda na mtu kupata content materials anazopenda kuzisoma kwa muda sahihi na wakati sahihi.
✍️Act as a Filter or Chujio, kwa kuchuja na kumletea mtu kile ambacho angependa kukisoma na kujifunza hapa mjini JF.

👏👏 Marvelous One🔥 Mr. Random Useless Guy

Adios Compatriot
✌️

By "No One Who Is Someone"​
Umeongea boonge la point, JF walichukue hili na kulifanyia kazi.
 
Back
Top Bottom