benzemah
JF-Expert Member
- Nov 19, 2014
- 1,504
- 3,034
WAZIRI wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Innocent Bashungwa, kuelekea maadhimisho ya miaka 60 ya Jeshi la Kuienga Taifa (JKT) kesho, amesema IKT itaendelea kutekeleza, agizo la Rais Samia Suluhu Hassan la kuibua na kutambua vipaji vya vijana na kuviendeleza.
Bashungwa aliyasema hayo jana jijini Dodoma alipozungumza na waandishi wa habari kuhusu maadhimisho hayo yanayotarajiwa kufanyika kesho, mgeni rasmi akitaraiwa kuwa ni Rais Samia.
Alisema katika maadhimisho hayo, Israel imealikwa kushiriki kutokana na historia ya ushirikiano ulioanza enzi za Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, al-ipokuwa anakwenda Ghana kwa shughuli za kiserikali, aliongozana na baadhi ya marafiki, viongozi wa nchi hivo na aliporejea ndipo JKT ilianzishwa.
Pia alisema, viongozi mbalim-bali wamealikwa kuhudhuria maadhimisho ya miaka 60 ya jeshi hilo tangu lianzishwe Julai 10, 1963 na kuomba watanzania waiitokeze kwa wingi kujionea gwaride litakalofanywa na vijana wa JKT pamoja na shughuli mbalimbali za kijamii
"JKT taendelea kutekeleza agizo la Rais Samia la kuibua na kutambua vipaji vya vijana ikiwamo kuviendeleza ili kuwajengea uwezo katika fani mbalimbali," Waziri Bashungwa alisema
"Pamoja ulinzi wa taifa, jeshi hilo lina jukumu la kulea vijana katika maadili na uzalishaji mali kupitia Shirika la Uzalishaii Mali ( Suma JKT) linalowaandaa kuwa bora. Alisema moja kati ya maagizo ya Rais Samia kwa JKT ni kuibua, kulea na kukuza vipaji vya vijana hususani wanaolelewa ndani ya jeshi hilo ili wajitambue na kuwa imara.
Alisema maadhimisho hayo yali-tanguliwa na shughuli mbalimbali za kijamii ikiwamo uzinduzi wa mnara wa kumbukumbu ya miaka 60, uchangiaji wa damu, kutembelea vituo vya kulea watoto na kutoa zawadi mbalimbali vikiwamo vyakula na kufanya usafi katika Hospitali ya Chamwino na kutoa msaada kwa wagonjwa.
Bashungwa aliyasema hayo jana jijini Dodoma alipozungumza na waandishi wa habari kuhusu maadhimisho hayo yanayotarajiwa kufanyika kesho, mgeni rasmi akitaraiwa kuwa ni Rais Samia.
Alisema katika maadhimisho hayo, Israel imealikwa kushiriki kutokana na historia ya ushirikiano ulioanza enzi za Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, al-ipokuwa anakwenda Ghana kwa shughuli za kiserikali, aliongozana na baadhi ya marafiki, viongozi wa nchi hivo na aliporejea ndipo JKT ilianzishwa.
Pia alisema, viongozi mbalim-bali wamealikwa kuhudhuria maadhimisho ya miaka 60 ya jeshi hilo tangu lianzishwe Julai 10, 1963 na kuomba watanzania waiitokeze kwa wingi kujionea gwaride litakalofanywa na vijana wa JKT pamoja na shughuli mbalimbali za kijamii
"JKT taendelea kutekeleza agizo la Rais Samia la kuibua na kutambua vipaji vya vijana ikiwamo kuviendeleza ili kuwajengea uwezo katika fani mbalimbali," Waziri Bashungwa alisema
"Pamoja ulinzi wa taifa, jeshi hilo lina jukumu la kulea vijana katika maadili na uzalishaji mali kupitia Shirika la Uzalishaii Mali ( Suma JKT) linalowaandaa kuwa bora. Alisema moja kati ya maagizo ya Rais Samia kwa JKT ni kuibua, kulea na kukuza vipaji vya vijana hususani wanaolelewa ndani ya jeshi hilo ili wajitambue na kuwa imara.
Alisema maadhimisho hayo yali-tanguliwa na shughuli mbalimbali za kijamii ikiwamo uzinduzi wa mnara wa kumbukumbu ya miaka 60, uchangiaji wa damu, kutembelea vituo vya kulea watoto na kutoa zawadi mbalimbali vikiwamo vyakula na kufanya usafi katika Hospitali ya Chamwino na kutoa msaada kwa wagonjwa.