Qumanina zao mkule kiboga huyo jamaa na Juliet umle piaSEHEMU YA 18
Nilikuwa na hasira, wakati huo nilikuwa na uwezo wa kufanya kitu chochote kile. Christopher alijitahidi kuniomba msamaha lakini sikujali, nikampa kamera Juliet kwa ajili ya kurekodi kila kitu kilichokuwa kikiendelea baina yangu na Christopher.
Siwashauri watu kufanya kama nilichokifanya usiku wa siku hiyo, hapa ninajaribu kuwahadithia maisha yangu ya nyuma.
Mchezo niliotaka kuufanya siku hiyo ulikuwa mbaya ambao nitakuwa nikiukumbuka katika maisha yangu yote.
Nilitaka Christopher ajute tu. Nilikuwa na uwezo mkubwa wa kuwaua lakini hilo halikuwa lengo langu.
Kwa hapa ngoja niwaambieni kitu fulani. Mtu fulani anapokufanyia kosa kubwa, kumuua si suluhisho, kama aliuumiza moyo wako, basi wewe ufanye moyo wake kuwa na majonzi milele.
Nilichokitaka kukifanya ni kuziharibu akili zao tu, niwafanye wajute katika maisha yao yote, yaani hata siku Christopher akikaa chini na kuanza kukumbuka basi kichwa chake kiwe kinamuuma, asijisikie furaha maisha yake yote.
Kama ningewaua, ilimaanisha kwamba ingekuwa mwisho wa kila kitu, kama nilivyokuwa nimeumia, kama nilivyokuwa sina raha, yote hayo nilitaka hata nao wayapate, wajisikie kama nilivyokuwa nikijisikia kipindi hicho. “Nisamehe sana Steven...” alisema huku akilia kama mtoto.
Kwa wakati huo moyo wangu ulikuwa umebadilika kabisa, sikuwa Steven yule niliyekuwa na huruma, nilikuwa kama mwanajeshi wa Jeshi la NAZI huku nikiongozwa na kiongozi mwenye roho mbaya, Adolf Hitler.
“Kipenzi, njoo uchukue hii simu, huu ni muda wa show time,” nilimwambia Juliet ambaye akaja na kuchukua simu yangu.
“Hakikisha haunichukui usoni, ukinichukua usoni hata kama kwa bahati mbaya, nakuua. Hakikisha unarekodi kama mpiga picha mkuu, yaani uchukue sura yake vizuri, ninapomfanyia kazi na mambo mengine, umesikia?” nilimuuliza Juliet.
“Nim..es..iki..a,” alisema Juliet huku akitetemeka.
Mfyuuu nini sasaKheeeeee![]()
SEHEMU YA 17
Niligonga kwa sekunde kadhaa, mlango ukafunguliwa, macho yangu yakagongana na macho ya Christopher, alishtuka sana na kutaka kufunga mlango ila nikauzuia na kumsukumia ndani.
Macho yangu yakatua kwa Juliet, alikuwa mtupu kitandani, aliponiona, alishtuka mno, akajifunika shuka. Hata kabla Christopher hajafanya kitu chochote, nikatoa bastola na kumnyooshea.
“Naomba unisamehe Steven..naomba unisamehe rafiki yangu,” aliniambia Christopher huku akipiga magoti.
“Nisamehe mume wangu,” aliniambia Juliet.
Nikabaki kimya, machozi yalikuwa yakinitoka, hasira zikanipanda, nikauma meno kwa hasira. Nikajisikia kuuaua tu wakati huo. Nikachukua simu yangu na kuwapiga picha mfululizo pale kitandani.
“Nitawasamehe? Naanzaje kuwasamehe? Yaani wewe Chriss ni rafiki yangu wa damu, ulikuwa bestman wangu kwenye harusi yangu, halafu nikusamehe! Nikusamehe kutembea na mke wangu?” niliuliza huku nikionekana kuwa na hasira mno.
“Nisamehe mume wangu....naomba unisamehe...” aliniambia mke wangu Juliet huku akitembea kwa magoti kunifuata, aliponikaribia nikampiga teke moja kali la mbavuni, akaangukia pembeni na kuanza kulia kama mtoto mdogo.
“Wewe malaya hebu nyamaza! Nikisikia unalia, nitakachoacha humu ndani ni ubongo wako kumwagika sakafuni,” nilimwambia Juliet kwa hasira, na kwa jinsi nilivyoonekana muda huo, alijua kabisa nilimaanisha kile nilichokisema.
Christopher hakuzungumza kitu, alikuwa kimya huku akiwa amepiga magoti.
Alinijua ninapokuwa na hasira nakuwaje, ninaweza kufanya jambo lolote lile bila kujali chochote. Kwa jinsi nilivyomuona, alijua kabisa muda wowote ule ningebonyeza kitufe cha bastola na kuwamaliza wote wawili.
“Christopher ni lazima uigize filamu ya ngono na mimi, Juliet utakuwa mpiga picha wetu, tukimaliza, picha nazipeleka magazetini na mitandaoni,” niliwaambia na kufunga mlango, ufunguo nikauweka mfukoni, nikatoa simu yangu na kuwasha kamera.
“Mkikataa, nawaua wote,” niliwaambia huku nikionekana kuwa na hasira.
Huo ndiyo uamuzi ambao niliamua kuuchukua, Christopher aliona raha kutembea na mke wangu, na mimi nilihitaji kumuonyeshea ni madhara gani yanatokea unapokamatwa na huyo mke wa mtu.

Dawa ya moto ni motoSHEMU YA 12
“Ninakupenda sana Steven,” aliniambia kipindi alichokuja ofisini mwangu.
“Samahani Upendo niite bosi,” nilimwambia huku sauti yangu ikitoka kwa kumaanisha sana.
Upendo alinisumbua sana lakini nilikuwa na msiamamo mkali, sikutarajia kumsaliti mke wangu maishani mwangu, na kama ingetokea hivyo isingekuwa kwa mfanyakazi wangu, ambaye anaishi kwa fedha zangu, anabadilisha nguo na kununulia magari kwa fedha zangu.
“Siweza kudate nawe,” nilimwambia Upendo.
Hakukoma, aliendelea kunifuatiia zaidi na zaidi lakini msimamo wangu ulikuwa uleule, sikutaka kudate naye.
Siku hiyo nilipoingia ofisini huku nikiwa na majonzi, kwa kuniangalia tu, aligundua kwamba nyumbani kwangu kilikuwa kimenuka, hivyo aliitaka nafasi hiyo kwa kisingizio cha kunipa furaha.
Nilipokaa kitini, akapiga hodi na kuingia, bado sikuonekana kuwa na furaha kabisa. Akapiga hatua na kusogea kule nilipokuwa, akanishika begani.
“Kuna nini bosi?” aliniuliza.
“Hakuna kitu.”
“Hapana. Haiwezekani. Huwa haupo hivyo. Wifi kakukorofisha nini?” aliniuliza huku akionekana kunionea huruma.
“Kawaida tu Upendo. Naombe ukaendelee na kazi.”
“Bosi, nitaendelea vipi na kazi na wakati upo katika hali hii? Siwezi, nakosa amani moyoni kukuona hauna furaha,” aliniambia kwa sauti yake nyembamba.
“Kaendeleea na kazi Upendo,” nilimwambia, kidogo nikatoa sauti yenye ukali.
Akaonekana kuogopa, akaanza kuondoka ofisini mwangu. Kumkataa Upendo ulihitajika moyo wa chuma, alikuwa msichana anayevutia sana, kwa nyuma alikua amejazia halafu siku hiyo sketi yake aliyokuwa ameivaa iliishia magotini huku kukiwa na mpasuo mdogo wa kizushi, nilipouona upaja wake, matemate yakanitoka na kujilaumu kwa kumuumiza mtoto huyu.
Kuna mambo mengi nilijifunza kwamba inawezekana mtu hataki kuchepuka ila kutokana na maisha yanayomzuka nyumbani, anajikuta akiwa amechepuka.
Toka nimuoe Juliet, sikutarajia kama kuna siku ningekuja kuchepuka nje lakini kwa kile kilichokuwa kikiendelea cha kunisaliti, niliona kwamba huo ndiyo ulikuwa muda pekee wa uchepuka.
“Lakini nina mtoto, nitaweza vipi kuchepuka? Kweli nimuumize Juliet? Haiwekani,” nilijiambia.
Wewe mke wa mtu anauma, ingawa sijaoa ila yanatokea, hata demu wangu kunisalit naptwa na wazimu sembuse mkeYaani stev kala amber rutty??
Hata kama ni hasira ila mambo mengine daah!!![]()
kumbeee,ukimuona niite nimpe vichambo vyakebaba kitunguu wake mtu kumbe story kasitisha namuona mmu huko anashusha mathread