Ulinisaliti Juliet

Ulinisaliti Juliet

SEHEMU YA 16

Nikateremka na kuelekea ndani.
“Dada habari yako!” nilimsalimia dada aliyekuwa mapokezi.
“Nzuri. Karibu kaka,” alinikaribisha huku akitabasamu.

“Asante. Ninahitaji chumba.”
“Kipo, gharama yake ni shilingi laki mbili kwa siku.”

“Hakuna tatizo.”
“Sawa. Naomba unipe dakika moja tu.”
“Sawa.”

Dada yule akaondoka, sikujua alipoelekea, nilichokifanya nikamuita dada aliyekuwa pembeni kwa ajili ya kumpa ofa moja tu. Aliponisogelea nikaanza kuongea naye.
“Mambo mrembo.”

“Poa. Karibu. Unahitaji kuhudumiwa?”
“Hapana. Ila nataka unisaidie kitu kimoja.”
“Kitu gani?”

“Kuna rafiki yangu anaitwa Christopher amechukua chumba humu. Unaweza kuniambia ni chumba namba ngapi?”
“Hapana. Haiwezekani.”

“Dada, naomba unisaidie bhana niwahi,” nilimwambia, nikatoa noti za shilingi elfu kumi-kumi, zilikuwa saba na kuziweka mezani, ila kisiri.
“Kweli unataka kuniacha kaka yako hivihivi?

Hebu acha hizo bhanaaaa,” nilimwambia huku nikitoa tabasamu.
Akaziangalia noti zile, kwake likaonekana kuwa si tatizo, yaani kuniambia chumba alichokuwa huyo mtu tu, kwake ikaonekana kitu chepesi lakini si kuacha fedha zile.

Akaangalia kwenye kompyuta fastafasta kwani alitaka kuniangalizia kabla yule mwenzake hakuja, kwani angekuja ilimaanisha zile fedha zisingekuwa zake.
“Namba thelathini na tano, ghorofa ya nne.”

“Nashukuru sana,” nilimwambia. Hakutaka kukaa mahali hapo, akaondoka fastafasta.
Baada ya dakika kadhaa, yule mhusika akarudi.

“Naomba chumba namba thelathini na saba,” nilimwambia.
“Unazipenda namba hiyo?”

“Yeah! Nilipokuwa nchini Ufaransa, namba thelathini na saba ni namba ya bahati sana, namba ya hatari ni 13, naomba chumba hicho,” nilimwambia huku nikitabasamu.

“Sawa. Usijali,” aliniambia na kunipa chumba hicho. Nikapanda lifti na kuondoka.

Nilipofika katika ghorofa hiyo, nikaanza kupiga hatua kuelekea kule kulipokuwa na chumba changu.

Nilipopita mbele ya chumba namba 35, mapigo yangu ya moyo yakadunda kwa kasi huku nikijisemea kwamba kwa wakati huo mke wangu alikuwa mtupu huku akifanya mapenzi na Christopher.

Nilipalekwa mpaka kwenye chumba changu na yule dada kuondoka, haraka sana nikaelekea katika mlango wa chumba kile alichokuwemo Christopher na mke wangu na kuanza kugonga.
 
SEHEMU YA 17

Niligonga kwa sekunde kadhaa, mlango ukafunguliwa, macho yangu yakagongana na macho ya Christopher, alishtuka sana na kutaka kufunga mlango ila nikauzuia na kumsukumia ndani.

Macho yangu yakatua kwa Juliet, alikuwa mtupu kitandani, aliponiona, alishtuka mno, akajifunika shuka. Hata kabla Christopher hajafanya kitu chochote, nikatoa bastola na kumnyooshea.

“Naomba unisamehe Steven..naomba unisamehe rafiki yangu,” aliniambia Christopher huku akipiga magoti.
“Nisamehe mume wangu,” aliniambia Juliet.

Nikabaki kimya, machozi yalikuwa yakinitoka, hasira zikanipanda, nikauma meno kwa hasira. Nikajisikia kuuaua tu wakati huo. Nikachukua simu yangu na kuwapiga picha mfululizo pale kitandani.

“Nitawasamehe? Naanzaje kuwasamehe? Yaani wewe Chriss ni rafiki yangu wa damu, ulikuwa bestman wangu kwenye harusi yangu, halafu nikusamehe! Nikusamehe kutembea na mke wangu?” niliuliza huku nikionekana kuwa na hasira mno.

“Nisamehe mume wangu....naomba unisamehe...” aliniambia mke wangu Juliet huku akitembea kwa magoti kunifuata, aliponikaribia nikampiga teke moja kali la mbavuni, akaangukia pembeni na kuanza kulia kama mtoto mdogo.

“Wewe malaya hebu nyamaza! Nikisikia unalia, nitakachoacha humu ndani ni ubongo wako kumwagika sakafuni,” nilimwambia Juliet kwa hasira, na kwa jinsi nilivyoonekana muda huo, alijua kabisa nilimaanisha kile nilichokisema.
Christopher hakuzungumza kitu, alikuwa kimya huku akiwa amepiga magoti.

Alinijua ninapokuwa na hasira nakuwaje, ninaweza kufanya jambo lolote lile bila kujali chochote. Kwa jinsi nilivyomuona, alijua kabisa muda wowote ule ningebonyeza kitufe cha bastola na kuwamaliza wote wawili.

“Christopher ni lazima uigize filamu ya ngono na mimi, Juliet utakuwa mpiga picha wetu, tukimaliza, picha nazipeleka magazetini na mitandaoni,” niliwaambia na kufunga mlango, ufunguo nikauweka mfukoni, nikatoa simu yangu na kuwasha kamera.
“Mkikataa, nawaua wote,” niliwaambia huku nikionekana kuwa na hasira.

Huo ndiyo uamuzi ambao niliamua kuuchukua, Christopher aliona raha kutembea na mke wangu, na mimi nilihitaji kumuonyeshea ni madhara gani yanatokea unapokamatwa na huyo mke wa mtu.
 
Back
Top Bottom