SEHEMU YA 22
“Hapana. Mtoto acha abaki.”
Siku iliyofuata tukachukua ndege mpaka Zanzibar, alionekana kuwa mwenye furaha mno na tulipofika kule, tukakaa kwenye hoteli ya gharama, huko tulifanya yetu na tulikaa kwa muda wa wiki nzima na ndipo tukarudi nyumbani.
Maisha yakaonekana kubadilika, upendo wa kinafiki niliokuwa nao moyoni ulikuwa zaidi ya kile kipindi cha kwanza.
MARCH 2
“Nahitaji mtoto wa pili kipenzi,” aliniambia kwa sauti ya upole.
“Usijali kipenzi, atatafutwa tu,” nilimwambia.
Kazi haikuwa ndogo, usiku mzima tulishinda tukimtafuta mdogo wake na Magreth. Kwa kipindi hicho nilijifanya kuwa mjinga bila kujua kwamba nilikuwa na akili zangu timamu.
Usiogope kuzaa na malaya, unachotakiwa ni kuwa na mtoto wako tu bila kujali ni mwanamke gani uliyezaa naye. Unaweza ukategemea kuwa na mke aliyetulia ili uzae naye mtoto lakini matokeo yake ukaambiwa kwamba mwanamke huyo hana kizazi.
Kwangu mimi, kuzaa na Juliet ilikuwa kawaida sana, alikuwa mke wangu japokuwa nilikubaliana na ukweli kwamba alikuwa kahaba mstaafu.
Siku ziliendelea kukatika, ilipofika Julai ya tarehe 21 ndipo nilipoanza kubadilika.
Kitu cha kwanza nikaanza kuchelewa kurudi nyumbani, kila alipokuwa akiniuliza, jibu langu lilikuwa ni kwa sababu nilikuwa na kazi nyingi mno ofisini.
Kiukweli ni kwamba nikaamua tu kutembea na wanawake wengine.
Nina fedha, nina kampuni so kuhusu wasichana walikuwa wakinipapatikia sana. Kuna siku nyingine sikuwa nikilala nyumbani na kila nilipoulizwa, kama kawaida yangu kisingizio changu kikaanza kuwa kilekile, kazi zilikuwa nyingi.
Juliet aliumia sana, aliniamini kwa asilimia mia moja, alinipenda kwa mapenzi yote, kitendo cha kumwambia kwamba nilikuwa bize tena huku akiwa mjauzito, aliumia kupita kawaida.
Hilo ndilo nililokuwa nikilitaka, nilitamani aendelee kuumia maisha yake yote, sikutaka kumuonea huruma kwa sababu hata mimi nilipokuwa nikiumia, hakunipa nafasi ya kunionea huruma.
“Baby, naomba leo uwahi nyumbani,” aliniambia simuni.
“Nahisi nitawahi, kazi si nyingi ofisini,” nilimwambia.
“Sawa. Mpenzi, nimekumisi mume wangu.”