Ulinisaliti Juliet

Ulinisaliti Juliet

SEHEMU YA 25

Niliporudi nyumbani usiku, kondomu zile sikuzikuta na wakati nguo zilikuwa zimefuliwa. Nilipomwangalia, macho yake yalikuwa mekundu hali iliyoonyesha kwamba alikuwa amelia sana.

“Kuna nini mke wangu?” nilimuuliza.
“Hakuna kitu mpenzi. Pumzika tu.”
“Hapana, siwezi kupumzika na wakati upo kwenye hai hii.”
“Naomba upumzike.”
Sawa.”

Wakati yeye akiwa na uchungu wa moyo, kwangu ilikuwa ni furaha tele. Ilipofika saa sita na nusu usiku, simu yangu ikaanza kuita, alikuwa amelala ila kwa sababu nilipanga kuipokea simu hiyo, hivyo sikutaka kulala japokuwa nami nilijifanya kulala.

Alipoisikia simu yangu inaita, akashtuka, nikaipokea na kuanza kuongea. Ilisikika sauti ya mwanamke upande wa pili, alikuwa ni Getrude, msichana aliyekuwa mfanyakazi wangu. Aliongea kwa kulalamika kwamba alikuwa amenimisi na alitaka kuniona, nilichokifanya ni kuinuka na kwenda kuoga.

Wakati nipo huko, meseji ikaingia simuni mwangu, nilisikia mlio huo na nilimpanga kwamba baada ya kuongea naye ilikuwa ni lazima atume meseji ambayo iliandikwa hivi ‘Baby, naomba uje, mwili unaniwasha, nahisi kuna vijidudu vinanitembelea mwilini.

Njoo uupoze moyo wangu kama jana na juzi ulivyonikuna vilivyo. Achana na huyo mjauzito, hawezi kukuridhisha, njoo kwangu nikupe mahaba motomoto mpaka uchanganyikiwe na kuona kwamba watoto wa kitanga tunayajua mapenzi. Kama unanipenda zaidi ya mke wako, njoo, ila kama mke wako ni zaidi yangu, usije’.
Nilipomaliza kuoga, nikarudi chumbani.

Alikuwa akilia sana kwani aliusoma huo ujumbe, nikajifanya kutokujali na wala sikumuuliza kulikuwa na nini, nikavaa na kuondoka zangu huku nikimuacha akilia kama mtoto.
Nilichokuwa nikitaka ni kumuumiza tu.
*
*
*
*
Je, nini kitaendelea?
Tukutane Ijumaa.
khaaaa nawe umezidi sasa,usingempa mimba kwanza umalize kisasi chako
 
SEHEMU YA 25

Niliporudi nyumbani usiku, kondomu zile sikuzikuta na wakati nguo zilikuwa zimefuliwa. Nilipomwangalia, macho yake yalikuwa mekundu hali iliyoonyesha kwamba alikuwa amelia sana.

“Kuna nini mke wangu?” nilimuuliza.
“Hakuna kitu mpenzi. Pumzika tu.”
“Hapana, siwezi kupumzika na wakati upo kwenye hai hii.”
“Naomba upumzike.”
Sawa.”

Wakati yeye akiwa na uchungu wa moyo, kwangu ilikuwa ni furaha tele. Ilipofika saa sita na nusu usiku, simu yangu ikaanza kuita, alikuwa amelala ila kwa sababu nilipanga kuipokea simu hiyo, hivyo sikutaka kulala japokuwa nami nilijifanya kulala.

Alipoisikia simu yangu inaita, akashtuka, nikaipokea na kuanza kuongea. Ilisikika sauti ya mwanamke upande wa pili, alikuwa ni Getrude, msichana aliyekuwa mfanyakazi wangu. Aliongea kwa kulalamika kwamba alikuwa amenimisi na alitaka kuniona, nilichokifanya ni kuinuka na kwenda kuoga.

Wakati nipo huko, meseji ikaingia simuni mwangu, nilisikia mlio huo na nilimpanga kwamba baada ya kuongea naye ilikuwa ni lazima atume meseji ambayo iliandikwa hivi ‘Baby, naomba uje, mwili unaniwasha, nahisi kuna vijidudu vinanitembelea mwilini.

Njoo uupoze moyo wangu kama jana na juzi ulivyonikuna vilivyo. Achana na huyo mjauzito, hawezi kukuridhisha, njoo kwangu nikupe mahaba motomoto mpaka uchanganyikiwe na kuona kwamba watoto wa kitanga tunayajua mapenzi. Kama unanipenda zaidi ya mke wako, njoo, ila kama mke wako ni zaidi yangu, usije’.
Nilipomaliza kuoga, nikarudi chumbani.

Alikuwa akilia sana kwani aliusoma huo ujumbe, nikajifanya kutokujali na wala sikumuuliza kulikuwa na nini, nikavaa na kuondoka zangu huku nikimuacha akilia kama mtoto.
Nilichokuwa nikitaka ni kumuumiza tu.
*
*
*
*
Je, nini kitaendelea?
Tukutane Ijumaa.
Hapa mtu lazima avimbe mpaka apasuke....maana sio haba.
 
SEHEMU YA 26

Najua unakumbuka kwamba mke wangu aliniumiza sana, nililia usiku na mchana na wakati mwingine kumkufuru Mungu kutokana na yale aliyokuwa amenifanyia, yote yale, nilijivisha moyo wa ujasiri na kuufanya moyo wangu kuwa kama wa bati na wakati ulikuwa ni wa nyama, niliumia nilipoumizwa, nilisononeka pale niliposononeshwa.

Nililia usiku na mchana na kazi ofisini hazikufanyika, kuzikuta kondomu katika gari la mke wako tena huku nyingine zikiwa zimetumika iliniumiza sana.

Majonzi, huzuni ilikuwa ni sehemu ya maisha yangu, huyuhuyu mke wangu, Juliet, mwisho wa siku nilimfumania ndani ya chumba cha hoteli, alikuwa uchi wa mnyama kitandani huku mwanaume mwingine akiwa na taulo tu!

Haukujua maumivu niliyoyapata, haukujua niliumia vipi. Kama ningekuwa na moyo mwepesi nadhani ningeweza kuua kwa sababu nilikuwa na bunduki mkononi mwangu, lakini katika vitu vyote hivyo, hata kuwagusa sikuwagusa.

Hivi unaweza kuniambia ni ujasiri wa kiasi gani niliokuwa nao? Hivi unaweza kuona ni kwa jinsi gani nilimheshimu mwizi wangu na mke wangu?

Hapa ninapoamua kumuumiza, naomba ieleweke tu kwamba ni lazima nimuumize, atake asitake, ni lazima nimuumize.

Usiku wa siku hiyo niliondoka nyumbani, najua moyo wake ulichanganyikiwa kwa sababu alijua fika kwamba niliondoka nyumbani na kwenda kwa mwanamke mwingine kufanya ngono usiku huo, wala sikutaka kujali, sikwenda kwa mwanamke mwingine ila nilikwenda hotelini kulala tena mbaya zaidi mpaka simu yangu nilikuwa nimeizima.

Usiku nilitulia kitandani, kichwa changu kilikuwa kikimfikiria mke wangu, Juliet, najua kwamba aliteseka kwa ajili yangu, aliumia sana lakini kwa wakati huo hakuwa na jinsi, ilikuwa ni lazima aumie kama nilivyoumia.

Asubuhi ilipofika, nikaamka. Kwa sababu haikuwa siku ya kazi kwa kuwa ilikuwa Jumamosi, nikasepa zangu na kuelekea Manzese, huko nilikuwa na kazi moja tu, kununua nguo ya ndani ya mwanamke.
 
SEHEMU YA 27

Nilipofika, nikaelekea katika moja ya duka hapo Manzese na kununua nguo moja nzuri na kumpigia simu Getrude na kumwambia kile alichotakiwa kukifanya, akakubaliana nami.

Nilipoingia garini mwangu, nikavua nguo zangu na kisha kuivaa ile nguo ya ndani ya mwanamke na kuelekea nyumbani.

Japokuwa nilikuwa nikifanya hivyo lakini kiukweli moyo wangu ulikuwa ukiniuma sana, nilimpenda Juliet, sikutaka aumie ila sikuwa na jinsi, nilitaka kumuonyeshea ni kwa jinsi gani nami niliumia.

Nilipofika nyumbani, alikuwa amekaa sebuleni, niliyaangalia macho yake, yalionyesha kabisa kwamba usiku mzima hakuwa amelala. Nilimuonea huruma lakini nikataka kujifanya kuwa na sura ya kikauzu, nikamsalimia, nikakaa kochini na kutulia.

“Unaendelea?” nilimuuliza.
“Naendelea vizuri, karibu mume wangu,” aliniambia huku akinionyeshea tabasamu, kwa kuliangalia tu, halikuwa tabasamu la furaha, lilikuwa na maumivu tele.
“Nashukuru.”

Nikasimama na kuanza kuelekea chumbani huku nikiwa nimeiacha simu yangu mezani makusudi.
“Nikuandalie chai?” aliniuliza.
“Hapana, nimekwishakunywa huko nilipotoka. Asante.”

Hakuna kitu kinachomuuma mwanamke kama kuona mume wake hali chakula alichokipika yeye.

Nilijua kwamba Juliet aliumia sana, lakini si ndiyo safi bwana, yeye si aliniumiza bila kunionea huruma, basi na mimi nilitakiwa nifanye hivyo.

Nilichokifanya chumbani, nikavua shati langu na kubaki na suruali tu huku nikimsikilizia aje chumbani.

Baada ya dakika tano, nikasikia mtu akija, nikajua yeye nilichokifanya ni kujiweka tayari, pale alipoingia tu, na mimi nisimama fastafasta na kuvua suruali yangu, nikabaki na chupi ya mwanamke.

Akashtuka sana, naweza kusema kwamba sijawahi kumuona akiwa na mshtuko wa namna hiyo, alichokifanya ni kunipa simu yangu huku akionekana kuumia mno, tayari kilio cha kwikwi kilianza kumkaba.
 
SEHEMU YA 28

“Kuna meseji ya.....” aliniambia lakini hata kabla hajamaliza sentesi yake, akaanza kulia kwa sauti ya juu huku akijiziba mdomo, akashindwa kuvumilia kukaa chumbani, akatoka na kuondoka zake, mi nikajiona kama bingwa, nikajilaza kitandani huku nikitabasamu, nikafungua sehemu ya meseji, kulikuwa na meseji mpya ambayo ilisomwa, ilitoka kwa Getrude niliyekuwa nikifanya naye madili.

“Mpenzi, una mahaba niue wewe, sasa ndiyo nini kuondoka na chu** yangu na kuniachia yako jamani? Au kwa sababu yangu ina mauamaua na inanukia vizuri? Jamani kesho niletee chu** yangu ili nikupe nyingine.

Mahaba yako sijawahi kuyaona,” ilisema meseji ile, kwa kuwa ilikuwa imesomwa, nikajua tu aliyesoma alikuwa Juliet.
“Yess! Hapo umecheza kama Pele, nitakuletea zawadi,” nilimwambia Getrude.

Nikatoka nje ya chumba kile huku nikitembea kwa mikogo, nilijiona bingwa. Sikujali mimba aliyokuwa nayo.

Nikaelekea sebuleni, Juliet hakuwepo. Nikaelekea jikoni, chumbani kwa mwanangu, nje, sehemu zote, Juliet hakuwepo, nikahisi kuchanganyikiwa.

Nilipoangalia mezani, nikakuta kikaratasi kikiwa na maneno machache tu yaliyosomeka ‘Nimeshindwa, bora nikapumzike kwa amani,” nikahisi kuchanganyikiwa. Alikuwa akimaanisha kwamba alikuwa akienda kujiua.
****

Akili yangu ilichanganyikiwa, kikaratasi nilichokisoma mezani kilinichanganya mno, nikaanza kukiangalia mara mbilimbili kwani kwa mara ya kwanza nilionekana kama kutokufahamu kile kilichokuwa kimeandikwa juu yake.

Maneno yalikuwa yaleyale kwamba ameshindwa na hivyo aliona bora kupumzika kwa amani.

Sikutaka kukaa nyumbani, nilichokifanya ni kutoka nje na moja kwa moja kumfuata Mchichi na kumuuliza sehemu alipokuwa ameelekea mke wangu, Juliet.

“Sijui ameelekea wapi, ametoka huku akiwa analia tu,” aliniambia Mchichi majibu ambayo hayakunisaidia kitu chochote kile.

“Amekwenda upande gani? Kulia, kushoto?” nilimuuliza.
“Sijajua, ila nadhani kushoto.”
Sikutaka kukaa ndani, nikafungua geti na kuondoka.

Hapo ndipo nikaanza kuona madhara juu ya yale niliyokuwa nikiyafanya, nilimuumiza sana Juliet lakini niliyaona hayo ndiyo yalikuwa malipo yake.
 
SEHEMU YA 29

Unakumbuka jinsi alivyoutesa moyo wangu? Unakumbuka jinsi alivyonifanya nilie kama mtoto huku hata kazi zangu zikiwa hazifanyiki kama inavyotakiwa kufanyika?

Najua unakumbuka, najua ulinionea huruma sana mpaka wengine kuniambia nimpe talaka lakini niliendelea kuwa naye huku nikiamini kwamba katika maisha, what goes around, comes around.

Nilianza kufutilia kila njia, Julet hakuonekana kabisa machoni mwangu. Wasiwasi wangu ukaendelea kuongezeka moyoni mwangu kwa kuamini kwamba inawezekana alikuwa amekwenda sehemu ya mbali kwa ajili ya kukamilisha mipango yake.

Wakati nikijifikiria hayo, nikapata wazo moja la kwenda ufukweni. Kwa kuwa nyumba yetu ya hapo Mbezi Beach haikuwa mbali na ufukwe, nikaanza kuelekea huko huku nikiwa na matumaini makubwa ya kumuona mke wangu.

Kila nilipokuwa nikipiga hatua, moyo wangu ulikuwa katika sala nzito za kutaka Mungu anifanikishe niweze kumpa mke wangu huko ufukweni.

Nadhani Mungu aliyasikia maombi yangu, nilipofika huko, nikamkuta amekaa mchangani huku uso wake akiwa ameupitisha katikati ya mapaja akilia.

Hakukuwa na watu wengi ufukweni hapo, nikaanza kupiga hatua za taratibu kumfuata, nilipomfikia, nikainama na kumshika begani, akauinua uso wake na kuniangalia, macho yake yalikuwa mekundu na machozi yalibubujika mashavuni mwake.

Moyoni mwangu nikafarijika, nikaridhika kwa asilimia mia moja kwamba kile nilichokuwa nikikihitaji kilikuwa kimefanyika, hivyo huo ulitakiwa kuwa mwanzo wa mimi na yeye kuungana na kuishi kama zamani. “Kwa nini unanifanya hivi Steve?” aliniuliza huku akilia.

Nafikiri kama asingekuwa katika hali aliyokuwa nayo, jibu ambalo nilitakiwa kumpa lingeweza kumfanya kuikimbilia bahari, ajitose na kisha ajimalizie huko.

Lakini kitu cha kwanza nikaiangalia hali yake kwanza, alikuwa mtu aliyehitaji faraja kubwa kwa wakati huo, kitendo cha kumpa jibu la shombo lingemuumiza zaidi.
 
SEHEMU YA 30

Nilitoka nyumbani kumfuata yeye, sasa ungekuwa ni ujinga mtu uliyemfuata unampata na kumpa jibu la shombo kwani kama unajua una jibu lako la shombo, kwa nini umtafute, si ungemuacha aendelee na maisha yake!

“Juliet....”
“Umeniumiza Steve, hivi hauioni hali niliyokuwa nayo?

Hivi uoni ni kipindi kigumu namna gani ninachokipitia mpaka uanze kunifanyia mambo haya? Kwa nini unanifanyia haya? Kwa nini hausubiri mpaka nijifungue ndiyo unifanyie mambo haya?

Nakwenda hospitali kila siku, nimepewa taarifa mbaya kwamba mtoto kakaa vibaya tumboni, kila nikitaka kukwambia, unakuja na mapya ya kuniumiza, lakini kwa nini unanifanyia hivi? Hivi uliamua kunisamehe ili kuniumiza?

Sawa, labda hilo lilikuwa lengo lako, sasa kwa nini hukusubiri mpaka nijifungue? Kama ni kosa nililifanya mimi, kwa nini matatizo hayo umsababishie hata mtoto wako asiyejua kitu chochote kile? Kwa nii Steve unamfanyia hivi mtoto wako?”

Muda wote ambao alikuwa akiniambia maneno hayo alikuwa akilia tu. Hata kama ungekuwa na moyo mgumu kiasi gani, kwa jisi alivyokuwa akiongea, ungemuonea huruma tu.

Maneno yake yaliuchimba moyo wangu, yaliutetemsha na kuumiza kupita kawaida. Nilichukulia kama game f’lani hivi lakini kwa mwenzangu ilikuwa ni hatua mojawapo ya kumsogeza karibu na kaburi.

“Juliet.....” nilimuita kwa sauti ya chini, akaitikia kwa kutikisa kichwa chake juu na chini. Nikasimama na kumnyooshea mkono na kisha kumuinua.

Nikaanza kumwangalia machoni mwake.
“Naomba nikukumbatie,” nilimwambia, akanikubalia.

Nikamkumbatia mke wangu, Juliet. Hilo lilikuwa kumbatio langu la kwanza kwake toka kipindi kile alichokuwa akiitibua akili yangu.

Nilijihisi wa tofauti kabisa siku hiyo, sikufichi, kiukweli, moyo wangu ukawa radhi kumsamehe Juliet kwa kila kitu kilichokuwa kimetokea, kuanzia siku hiyo, kila kitu kikaanza upya maishani mwetu mpaka mke wangu alipojifungua mtoto wa kiume tuliyempa jina la Jericho.
 
SEHEMU YA 31

KUMBUKUMBU: Hiyo ni kumbukumbuku muhimu ambayo nimekupa kuhusiana na mke wangu, tabia zake chafu zilizokuwa zimenikera na kuamua kumlipizia kisasi.

Maisha ya ndoa yapo hivyo, mara nyingi unakuwa unnamuamini mke au mume wako lakini kumbe upande wa nyuma anakubadilikia na kumpa penzi mtu mwingine kabisa.

Linapotokea hili, utakapoambiwa hutakiwi kupaniki kwani ni hali mbaya mno hasa inapomkuta mtu fulani, unakuwa na nguvu ya kufanya jambo lolote lile, hata kuua, kwako linaweza kuwa jambo jepesi mno.

Sikutaka kumuua rafiki yangu wala mke wangu, nilihitaji wajifunze kwamba katika maisha haya, linapotokea jambo fulani, kuua si suluhisho hata kidogo.

Niliwafanyia mambo mabaya ambayo ninaamini kwa yeyote yule aliyesoma basi atakuwa amejifunza kitu fulani.
Huu ndiyo mwisho wa simulizi hiyo fupi. Nashukuru sana kwa kuifuatilia,

Mwisho
 
Back
Top Bottom