Niliumizwa kwa muda mrefu kidogo na yote ilikuwa ni kwa sababu nilikuwa nilimpenda nikimpenda ex wangu kwa dhati kabisa kwa kuwa ni mtu aliyenitoa mbali sana kwa kipindi akati niko kwenye wakati mgumu sana yeye pekee ndiye aliyenishika mkono bila kujali nini wala nini.sitaacha kuukumbuka wema wake mpka nafukiwa kaburini nasema kweli na Mungu ananiona ingawa aliniumiza mno kuliko mtu mwingine yeyote katika maisha yangu. amenipitisha kwenye maumivu makali ambayo sikuwah kutegemea kama nitakuja yapitia siku moja.jamn nikisema kumpenda mtu kwa dhati kabisa halafu anakuumiza nafikiri kwa anaejua hiyo situation anajua nini namaanisha.maana nilikuwa nae kwa miaka mingi kidogo na sikuwahi kuwa na mwanaume mwingine yeyote akati nipo nae.nilikuwa mwaminifu sana kwake kwa kuwa nilimpenda kuliko kawaida.ingawa ameniumiza lkni haki yake nampa.'amenionyesha mwanga mkubwa sana katika maisha.
Huwa sijutii kumfahamu hata kwa bahati mbaya.ingawa kabla sijafikia uamuzi wa kusema sijutii kumfahamu,nilikuwa nikimchukia kuliko mtu mwingine yeyote.unajua kwanini niliamua kuyafuta machukizo yote,nikwa sababu niliamua kukimbilia kanisan ingawa nilikuwa nikikumbana na changamoto za baadhi ya marafiki zangu kuwa niende kwa wagang wa kienyeji.kweli ilikuwa kidogo kuchanganyikiwa lkni niliamini Mungu pekee ndiye mwenye kunijua mimi na hatma yangu na kwanini nayapitia haya.na ili nizungumze na Mungu na kuyajibu maombi yangu ilikuwa ni lazima kumsamehe ingawa ilikuwa ni ngumu mnooo..lkni nilimsamehe.
Ninamshukuru sana kwa kuniumiza.*ninakushukuru sana kwa kuniumiza na kunipitisha katik yale maumivu*.wapendwa,maumivu yake yamenijenga mno!yamenifanya niwajue watu,yamenifanya nimjue Mungu kuliko nilivyokuwa nikimjua kuwa yupo katika maisha yetu anaishi ni sisi kumkaribisha tu.
Back to the point kuwa nilifanyaje kwa mwenye uzi..niliukimbilia msalaba.natumai nimekujibu.asante.