Ulifanyaje kukabiliana na maumivu ya mapenzi?

Ulifanyaje kukabiliana na maumivu ya mapenzi?

Sio rahisi kumsahau demu halisi wa hisia zako
Japo ilikuwa ngumu kwa upande wangu kumsahau nilianza kujifunza mbinu mpya za mapenzi
Nilijitahidi sana kutengeneza cartoon ya aina ya mwanamke alie niache kisha nikatengeneza na cartoon ya bwana niliehic ndio alie mzuzua ya yule mwanaume niliifanya mbaya endapo ningeitatazama basi nilimdharau yule dem
mkuu mbinu hizo ulizitoa wapi...? je nini kilikuwa chanzo cha kutengana...?
 
nilifundishwa na mama na baba mama alianiabia nisiwe mwoga na jitaidi usimkosee mtu, baba akaniambia usikubalia kuonewa ..
asante nimejifunza kitu kwako...hope utawalea watoto wako kwa misingi hiyo..
 
Mnajuwa Nature is the RIGHT answear! siku zote ukiona sehemu kuna milima basi ujuwe kuna sehemu nyingine kuna mabonde, ukiona mtu ana faraja basi elewa kuna mwingine anayo huzuni, ukiona leo umepata wa kukupoza moyo fahamu kuna mtu ameumizwa kwa raha kama hiyo unayoipata kwa wakati huo upande wake. Nature huwa ina balance all of these things.Ukiumizwa jipe muda kwani ujuwe kuna mtu bora anajiandaa kuja kwako ila wewe unamchelesha kwa kung'ang'ania mtuuu ambaye tayari hayuko kichani kwako. VUMILIA ILI UPATE MEMA.
nimejifunza uvumilivu kupitia post yako....ila tafadhali tuambie ilikuaje ukaumizwa kama ulisha wahi kuumizwa...? je moyo wako uliwezaje kuvumilia maumivu hayo ya mapenzi?
 
Unajua Mara nyingi mahusiano yapo kama GARI chakavu huwezi kuchelewa kupata break down
Ukijifanya abiria wa daradara unahitaji kufika tu Mwisho wa safari yako unaweza kupanda magari mengi ni muhim kulikarabati gari lako kwa kiwango sawa na safari yako
 
Unajua Mara nyingi mahusiano yapo kama GARI chakavu huwezi kuchelewa kupata break down
Ukijifanya abiria wa daradara unahitaji kufika tu Mwisho wa safari yako unaweza kupanda magari mengi ni muhim kulikarabati gari lako kwa kiwango sawa na safari yako
mkuu maneno yako yapo ki mafumbo....naomba tufafanulie tunahitaji kujifunza kitu kupitia wewe...uliyakabiri vipi maumivu ya mapenzi?
 
Sitasahau 5/12/2014 cku ya ijumaa saa 5 ucku ckumbuki na dakika ngapi naongea nae namuuliza "ndio hunitaki tena? anajibu kwa kujiamini kabisa " sikutaki na sikupendi" hpo anaongea ypo ghetto kwa jamaa aliyetoa barua kwao enzi hzo nimemaliza chuo no direction miaka 3 nimesugua mtaani napga dili ndogo ndogo tu kilikuwa kpnd kigumu kiukweli ila kwa mwanaume rijali its not ishu sana huja na kupita alikaa mwaka 1 tu hakuna ndoa wala nn 2015 akantafuta anataka kurudi hpo keshapata taarifa nimeajiriwa mkoa flan yaani nnachomfanya hata ibilisi hapendi kuna watu tunajua visasi bhana!
Hebu funguka, unamfanya nini mtoto wa watu!
 
pole sana mkuu...nadhani hivi sasa umejifunza...hutoumia tena na ata ukiumia maumivu hayato kuwa makubwa kama hayo ya mwanzo
Kweli aseee maana juzi tu nimetoka kupgwa chini na mtoto flan hv wa chuo ah...hata nimeumia bc? najionea fresh tu ile ni km bikra tu ikitolewa ndio imetolewa huwezi pata tena maumivu km yle!
 
Yaani hawa mademu, hawahitaji kushow serious love..... We kuwa kama vile hutaki unataka na ajue hawezi kukubaisha... Lakini akishajua yeye ndo kila kitu atakuyumbisha... Mimi ndo maisha inafikia kipindi wananiuliza hivi kweli tutafika maana ninavyokupenda lyke naona haupo serious..... Ooohhh Karaghabaho mpende mtu sasa kama mama yako itakula kwako.....
 
Hebu funguka, unamfanya nini mtoto wa watu!

Namba yke huwa sisevu hadi leo hii so nkiona namba ngeni nauliza nani? akitaja tu jina nakata akitext sijibu ila bahati mbaya ndg zke naongea nao fresh hpo ndio huwa inazidi kumuumiza anaweza nipigia dada ake nkaongea nae akampa mama akawapa wadogo zao akisema tu "ongea na flan" nakata cm adhabu ndogo ndogo tu km hzo zilizofanya aufyate na nimsahau ila yataka roho ngumu maana toto lenyewe toto haswaaa hovyohovyo waweza jikuta umerudisha majeshi haaaaaahaaaaaaaa watoto wa pwani nuksi sana aseee!
 
Halafu hutakiwi kuwa na Chick moja huu ndio Ujinga utababaishwa mpako Ukome kuwa nazo nyingi...... Usituone watu mjini tuna Nokia vitochi na Smart phone, Nokia Vitochi ni kwa ajili yA kubadilishia line ambayo unawasiliana na wengine
 
Niliumizwa kwa muda mrefu kidogo na yote ilikuwa ni kwa sababu nilikuwa nilimpenda nikimpenda ex wangu kwa dhati kabisa kwa kuwa ni mtu aliyenitoa mbali sana kwa kipindi akati niko kwenye wakati mgumu sana yeye pekee ndiye aliyenishika mkono bila kujali nini wala nini.sitaacha kuukumbuka wema wake mpka nafukiwa kaburini nasema kweli na Mungu ananiona ingawa aliniumiza mno kuliko mtu mwingine yeyote katika maisha yangu. amenipitisha kwenye maumivu makali ambayo sikuwah kutegemea kama nitakuja yapitia siku moja.jamn nikisema kumpenda mtu kwa dhati kabisa halafu anakuumiza nafikiri kwa anaejua hiyo situation anajua nini namaanisha.maana nilikuwa nae kwa miaka mingi kidogo na sikuwahi kuwa na mwanaume mwingine yeyote akati nipo nae.nilikuwa mwaminifu sana kwake kwa kuwa nilimpenda kuliko kawaida.ingawa ameniumiza lkni haki yake nampa.'amenionyesha mwanga mkubwa sana katika maisha.


Huwa sijutii kumfahamu hata kwa bahati mbaya.ingawa kabla sijafikia uamuzi wa kusema sijutii kumfahamu,nilikuwa nikimchukia kuliko mtu mwingine yeyote.unajua kwanini niliamua kuyafuta machukizo yote,nikwa sababu niliamua kukimbilia kanisan ingawa nilikuwa nikikumbana na changamoto za baadhi ya marafiki zangu kuwa niende kwa wagang wa kienyeji.kweli ilikuwa kidogo kuchanganyikiwa lkni niliamini Mungu pekee ndiye mwenye kunijua mimi na hatma yangu na kwanini nayapitia haya.na ili nizungumze na Mungu na kuyajibu maombi yangu ilikuwa ni lazima kumsamehe ingawa ilikuwa ni ngumu mnooo..lkni nilimsamehe.


Ninamshukuru sana kwa kuniumiza.*ninakushukuru sana kwa kuniumiza na kunipitisha katik yale maumivu*.wapendwa,maumivu yake yamenijenga mno!yamenifanya niwajue watu,yamenifanya nimjue Mungu kuliko nilivyokuwa nikimjua kuwa yupo katika maisha yetu anaishi ni sisi kumkaribisha tu.


Back to the point kuwa nilifanyaje kwa mwenye uzi..niliukimbilia msalaba.natumai nimekujibu.asante.
 
kabisa na nitalianza mapema sana... kwanza akifikisha miaka miwili namwambia asikubali kupakatwa na mtu asiye mjua ni kosa na akifikisha miaka sita nitamwambia kwa nini nilimkataza
naomba nifafanulie hapo...kwanini utamwambia hayo...?
 
Yaani hawa mademu, hawahitaji kushow serious love..... We kuwa kama vile hutaki unataka na ajue hawezi kukubaisha... Lakini akishajua yeye ndo kila kitu atakuyumbisha... Mimi ndo maisha inafikia kipindi wananiuliza hivi kweli tutafika maana ninavyokupenda lyke naona haupo serious..... Ooohhh Karaghabaho mpende mtu sasa kama mama yako itakula kwako.....
sasa mkuu, kama uliwahi kuumizwa, naomba utuambie ulijinasuaje kwenye kidonda cha mapenzi....kidonda chako ulikitibu kwa namna gani? je kovu limebaki au umelifuta kabisa?
 
Halafu hutakiwi kuwa na Chick moja huu ndio Ujinga utababaishwa mpako Ukome kuwa nazo nyingi...... Usituone watu mjini tuna Nokia vitochi na Smart phone, Nokia Vitochi ni kwa ajili yA kubadilishia line ambayo unawasiliana na wengine
inavyoonekana ulishawahi kuumizwa mkuu...tuambie jinsi ulivyojinasua kutoka kwenye kifungo cha usaliti...nadhani kipo tutakachojifunza...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom