Sio kila mahusiano yataishia Ndoa

Sio kila mahusiano yataishia Ndoa

Mwl Mwakujonga

JF-Expert Member
Joined
Jun 29, 2023
Posts
358
Reaction score
708
Sio kila mahusino lazima yafikie ndoa

Napokea simu kutoka kwa rafiki yangu ,ananiuliza umemfanya nini shem? Nikauliza kwani kunanini akaniuliza uko wapi? Nikamwambia niko maeneo ya chuo , akanimbia nakuja tuongee.

Tukiwa shule ya Alevel, wakati ndio ujana umeanza kubalee na unatamani sasa uanza angalau mahusiano

Kuna mwalimu alikuja wafield, mwalimu alikuwa yuko vizuri sana katika somo la hesabu , alitufundisha vizuri sana na kututia moyo na kutuhasa tusome kwa bidii na kutuhasa kutokuangaika na mapenzi

Yule mwalimu nilitokea kumwelewa sana, alitupa mahope akatwambia tukifika chuo tutakutana na warembo amboa hatijawai kukutana nao kwa hiyo tusipoteze fursa ya kusoma kwa kuangaika na mapenzi

Mafundishi yale laniingia kweli kweli nikakazana kusoma ili siku nikifika chuo nitafute mrembo wangu

Mungu sio athumani , nilichaguliwa kwenda chuo kikuu kilichopo Dar es salaam, na bahati nzuri chuo hicho nilipangiwa na rafiki yangu ambaye tumesoma wote advance

Shauku yangu ya kupata mwenza chuoni , haukuzaa matunda kwani maisha hayakuwa kama tulivyo ambiwa.

Miaka ikasogea rafiki yangu alikuwa wakwanza kupata rafiki wa kike na kule kupata rafiki wakike kulipunguza urafiki wetu.

Sio kwamba tulikuwa mbali hapana tulikuwa chumba kimoja kwa miaka yote na tulikuwa tunapata chakula pamoja kwa kipindi chote tukiwa chuoni

Changamoto ikaanza kuonekana si unajua wanapokula wapenzi kuna mambo yanakuwa mengi

Kutokana na mwenzangu kuwa na mpenzi wake na mimi niko single kukatengeneza ka wazo la kutafuta mwenzangu

Licha ya jitihada za rafimi yangu kunitafutia mpenzi , kutokuzaa matunda licha ya kuwa marafiki nilikuwa na standard zangu linapokuja swala la mahusiano

Mahusiano kwangu ayakuwa tu kwa ajili ya leo na kesho, yalikuwa ni kwa ajili ya maisha, kwani binafsi kuna mambo ambayo sikuwaikuyapenda tangu nikiwa mdogo ya kuwa na mtoto wa nje

Kweli nilifanikiwa kuwa na rafiki wa kike , urafiki ulikuwa mzuri sana tu na nilimshukuru Mungu kwa ajili yake

Miaka ilisogea , na mahusiano yakazidi kujengeka na matarajio ya kuwa pamoja baada ya shule kuongezeka nk

Ghafla mahusiano yakaanza kuingia changamoto ambazo hazikuwa ndogo, changamoto ambazo zilipelekea hata kuhatarisha uwezo wangu wa kusoma na kufocus na shule

Changamoto hizo ziliniweka njia panda nikafika mahali nikachagau pamoja na kwamba nilipenda nilitakiaa kufanya maamuzi ya kuchagua mahusiano au shule

Haikuwa rahisi kufanya maamuzi ingawa hapo mwanzo niliona ni rahisi lakini haikuwa rahisi

Namshukuru Mungu sio kila mahusiano ambayo unaweza kuyapitia yanaeweza kulata matokeo chanya

Kuna neno ambalo nilijifunza moyoni kwamba inawezekana yale mahusiano yalikuwa darasa kwangu ili siku moja nisije kuwa mgeni hata kusema i love u.

Namshukuru Mungu kila mmoja aliendelea na maisha yake na Mungu kwa kweli alikuwa mwaminifu kwa kila mmoja.

Nilichojifunza sio kila mahusiano lazima yatafika kwenye ndoa mengine yatakufundisha kusema i love you kwa mwenzako utakaye kutana naye baada ya hapo

Cha msingi futa machozi , Muombe Mungu akupo uponyaji wa nafsi ili siku utakapo kutana naye yule ambaye Mungu amekupangia usiwe na mawazo ya ulikotoka

Kosa kubwa ambalo linawakuta watu ni kutokusamehe wale ambao walikuwa nao katika mahusiano wasijue kwamba kusamehe ni sehemu moja wapo ya kupona katika mahusiano yaliyovunjika

Inawezekana ulimpenda sana na nikawaida hakuna mahusiano pasipo upendo ila upendo unajengwa na ujue kama kitu kinajengwa ujue kinaweza kubomolewa

Wataalamu wa ujenzi wanasema kujenga ni kazi kuliko kubomoa ila kwenye mahusiano kubomoa ni kazi kuliko kujenga kwa sababu unapobomoa unabomoa kwa maumivi.

Nilijifunza kwa tai , tai anapokuwa mzee anakosa nguvu ya kuruka mbali, anafanya maamuzi ya kwanza nikukaa kwenye mwamba na kuondoa mabawa yote na kucha kwa maumivu makali kwa sbababu anajua yale maumivu ni ya kitambo ila uponyaji ni wa milele

Tai akishatoa kucha na mabawa mara baada ya muda anakuwa kama kijana mabawa mapya yanatokea na kucha mpya, anakuwa na kasi na nguvu kama hapo mwanzo

Jifunze kwa tai ni kweli mahusiano yamefika mwisho, jikung'ute fanya kila unaloweza kukubali matokeo na kuanza upya

Nachokumbuka wakati mwingine mahusiano ni njia ya kukufundisha kujua hata kutoka out najua haukuwa kujiuliza mambo ambayo umejifunza kupitia ayoa mahusiano

Mwisho usimwombe vibaya mwenzako hata kama likuwa na sehemu ya kuvunjika kwa mahusino mwachie Mungu, na Mungu akusaidie
 
Chuo umeenda kutafuta mademu au kusoma?.
Ndio maana wengi mnafeli au mnatoka kapa


Kama ningekuwa mzazi nalipa ada ningeumia mno
 
Inapendeza kuwa na mahusiano mengi sana, kwani inasaidia kuchukua nyota za watu pia.
 
🎶 ulifeli sekondori kwendaga chuo 🎶

Point yako ni ipo hapo?
 
How have you been dearest. Tumepotezana,
Ongea na mdogo wetu asome mapenzi na shule wapi na wapi? 😀
am good, tumepotezana sana aiseee🙌🏾 i'll give you a call kesho


dogo anajikuta shurkhan subiri limkute jambo
 
am good, tumepotezana sana aiseee🙌🏾 i'll give you a call kesho


dogo anajikuta shurkhan subiri limkute jambo
I Will be waiting.

Ahaha likimkuta nyuzi kibao na wakataa ndoa. Mshika mawili moja hunponyoka
 
Back
Top Bottom